Uchawi haupo, ni imani tu

Uchawi haupo, ni imani tu

Linaingia sema tu haijui Bibilia vizuri, angepinga uwepo wa Uchawi bila kuitaja dini, nisingepingana nae, ila Dini hata hiyo anayoiamini inatambua uchawi upo, na Kinga yake ni Yesu.
Hivyo kukataa kwake ni kuipinga Bibilia
Angalie hizo picha alafu aweke coment.View attachment 1586161View attachment 1586162View attachment 1586163View attachment 1586165View attachment 1586166
Ndugu,km umesoma vizuri uzi wangu nadhani umejieleza vizuri,kuwa Uchawi haupo kwa wenyewe, bali upo ktk mindset za watu, labda natumia lugha ngumu kidogo,hivyo mnashindwa kunielewa.Hebu nifafanue kidogo,ni hivi Ukiamini kuwa Uchawi upo utakuwepo tu,si umeamini?!!!.Lkn ukiamini kuwa haupo ila ni sarakasi za kihuni tu nakwambia hivi hutapatwa na chochote.Hata ktk maandiko matakatifu Uchawi unaotajwa humo ulitokana na kuamini,Imani ina nguvu sana,haijalishi iwe mbaya au nzuri,kazi kwako.
 
Sasa wewe umaamini Yesu wa nini sasa kama hamna uchawi? Hata yeye hakuna haja ya kumuamini kwa sababu anaamini mapepo na majini yapo na ndio uchawi wenyewe.
Soma vizuri uzi wangu utanielewa namaanisha nini.Inawezekana umesoma haraka haraka sana,Wewe soma taratibu.
 
Baraka ya watu,vitu,n.k.ni kawaida kwa Imani yangu km Mkristo Mkatoliki,nafanya hivyo km ishara ya kumkabidhi Mungu jitihada zangu ili kupitia maombi ya Mtumishi wake niweze kufanikiwa.
Kama unaamini baraka za Mungu basi ni kwamba unajua kuna upande wa pili unaoondoa hizo baraka
 
Yesu anao moto gani??, mbona alishindwa kuwawashia wale waliomtungika msalabani???. Akabaki kulia tu; ewe Baba ewe Baba mbona waniacha??
Hii siyo mzuri, acha mtu na imani yake
 
Ndugu,km umesoma vizuri uzi wangu nadhani umejieleza vizuri,kuwa Uchawi haupo kwa wenyewe, bali upo ktk mindset za watu, labda natumia lugha ngumu kidogo,hivyo mnashindwa kunielewa.Hebu nifafanue kidogo,ni hivi Ukiamini kuwa Uchawi upo utakuwepo tu,si umeamini?!!!.Lkn ukiamini kuwa haupo ila ni sarakasi za kihuni tu nakwambia hivi hutapatwa na chochote.Hata ktk maandiko matakatifu Uchawi unaotajwa humo ulitokana na kuamini,Imani ina nguvu sana,haijalishi iwe mbaya au nzuri,kazi kwako.
Kwenda nawe hoja kwa hoja ni kitwanga maji kwenyenu
 
Biblia yenyewe inakubari Uchawi Upo! Wewe ni nani mpaka Ukatae!???

Point ya msingi ni kuwa UCHAWI UPO ILA UKIAMINI JINA LA YESU LIPO JUU YA UCHAWI, UGANGA NA MAJINI!!!
that's it!
 
Yesu anao moto gani??, mbona alishindwa kuwawashia wale waliomtungika msalabani???. Akabaki kulia tu; ewe Baba ewe Baba mbona waniacha??
Sawa bhana naona umedhamiria kukufuru,lkn Yeye ninayemwabudu siku zote atatudhihirishia kuwa ndiye mwenye nguvu,uweza,mamlaka na enzi.Wewe endelea kudharau lkn nakwambia hivi njoo na kauchawi kako uone jinsi yatakavyokutokea puani.Yesu ni Mungu anaweza yote, anajua yote,hbr ya yeye kulia msalabani ni fumbo la Imani linaloweza kuelezeka kiimani zaidi kuliko kwa akili za kibinadamu,Mungu akusaidie uweze kuelewa fumbo hilo la mateso,kifo na ufufuko wa Yesu Kristo.
 
Biblia yenyewe inakubari Uchawi Upo! Wewe ni nani mpaka Ukatae!???

Point ya msingi ni kuwa UCHAWI UPO ILA UKIAMINI JINA LA YESU LIPO JUU YA UCHAWI, UGANGA NA MAJINI!!!
that's it!
Mkuu ukishaamini kuwa Uchawi upo,hilo ni tatizo,wewe amini kuwa Haupo,utaishi kwa raga mustarehe.
 
Kama unaamini baraka za Mungu basi ni kwamba unajua kuna upande wa pili unaoondoa hizo baraka
Baraka za Mungu haziondolewi na kitu chochote isipokuwa mtu mwenyewe aliyezipokea atakapokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu hapo ndipo Baraka za Mungu zinaondoka.Uchawi hauna ngebe hizo.
 
Heshima zenu mabibi na mabwana...!!!!,Kuna hii hoja ya Uchawi kuwa upo,lkn mimi nasema hivi Uchawi haupo,kilichopo ni Imani tu za ushirikina ambazo kimsingi hujengwa tu ktk akili ya mtu,yaani mind set.Sasa unabisha??.Tuliza kimukhe mukhe nikupe mambo wewe.

Nakwambiaje Uchawi haupo ila ubongo wako tu ulivyouset. Ni sawa na kuamini kuwa wewe huna akili,nakwambia itakuwa hivyo hivyo.Sasa unataka kujua hoja yangu imelala wapi? Hebu nisimulie matukio yafuatayo uone jinsi ambavyo Uchawi haupo kabisa.

Mwaka 2009,nilikuwa Rukwa,kwaajili ya Field ya muda mrefu ktk Wilaya ya Nkasi,kutokana na muda kuwa mrefu nikalima mahindi ekari moja,Kabla ya kupanda mama mwenye nyumba (nilipopanga)akanishauri kuwa anipe dawa ya kienyeji ili niichanganye na mbegu ili kuweka ulinzi dhidi ya Chuma ulete au wakupaji wa mazao,nikakataa nikasema shamba langu litalindwa na damu ya Yesu,akanicheka sana lkn kwenye mavuno nikamzidi.

Mwezi mmoja baadaye niliamuru ng'ombe mzima afukiwe (Km Afisa kilimo na mifugo)kwasababu hakuwa anafaa kuliwa,wazee wakanifata wakanisii sana kuwa nisifanye hivyo kwa ujumla kamati nzima ya Serikali ya kijiji walinifuata nikawakatalia,yule mwenye ng'ombe alilia sana na alikuwa mzee,wakasema watafanya yao,lkn sikutishika.

Nakwambia hadi leo hakuna jambo lolote baya la kipekee lililonipata.Sasa kuna sababu gani ya mimi kuamini uchawi??.Ni upuuzi tu.

Nilipoajiriwa,nilikwenda Ngara,huko nikajishughulisha na kilimo cha Maharage,Nyanya na Mpunga,jamaa mmoja tuliyekuwa tunalima naye alikuwa anaogopeka kijijini pale kuwa ni bonge la chuma ulete,baba yake aliogopwa na wakazi wa pale kwa uchawi wa kila namna,jamaa yule akanishawishi kuwa anipe dawa niichanganye na mbegu ili kuzuia chuma ulete aka wakupaji wa mazao,huyu naye nikamtolea nje,nilimwambia mimi siogopi kitu,mbegu zangu nitazipeleka tu Kanisani kwaajili ya Baraka ya Padre,hiyo dawa aitumie yeye mwenyewe,nakwambia ktk mavuno nilikuwa nampiga gepu kubwa sana kwa eneo linalofanana ukubwa,jamaa akaniambia aisee,wewe jamaa una Imani kubwa!!!!,Mimi nilimsihi kumwamini Mungu na kutumia utaalamu ktk kilimo wala haina haja ya kuhangaika na dawa za kienyeji,ni kupoteza muda tu.

Siku nyingine kuna mama mmoja alishikwa na Mapepo km Kiongozi wa jumuiya nikaenda na wenzangu kumuombea,Jamaa mwingine(hakuwa Mkristo)aliyeamini sana ktk uchawi,alikuja na dawa kwaajili ya kumsaidia yule mama,lkn akiwa anakuja alikamatwa na mapepo yaliyotoka kwa yule mama yakampiga sana hadi jamaa akazirai,yakisema unaenda wapi?,wewe hutuwezi tulikuwa tunatafuta kwa kwenda sasa tumepata,wakati huo sisi tunaendelea na maombi,kwa hiyo mapepo yamemtoka mgonjwa na kumqingia yule jamaa aliyeamini uchawi.

Ndugu zangu Nina shuhuda nyingi za kutosha kusema kuwa "UCHAWI HAUPO" ila ni jinsi ulivyoiseti halmashauri ya Ubongo wako.Nakumbuka siku za nyuma kuna jamaa hapa JF aliwahi kusema "ikiwa kuna mtu anayejua kuroga amroge,akaleta mrejesho kuwa hakuna aliyejitikeza kumroga", Kumbe uchawi haupo ni fikra zetu tu.

HITIMISHO.
Ukimwamini Yesu na nguvu zake huna sababu ya kuhofu na kudhani kuwa UCHAWI upo,Kuamini uchawi ni matokeo ya kutokuwa na Imani kwa Mungu aishiye milele.Uchawi una madhara mengi ktk jamii sina haja ya kuyataja maana yaliyotokea Shinyanga kila mmoja ni shahidi,Uchawi unasababisha watu wasifanye maendeleo,na hatari zaidi kuliko yote,Uchawi unafanya watu kuwahusu binadamu wenzao ambao wanawadhani kuwa wachawi.Km kweli kuna MTU ni Mchawi humu JF aniroge mimi tuone.

Imani ni nini?

Imani ni hakika ya mambo yatarajiwayo. Ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Resubmit!.
 
Back
Top Bottom