Uchawi haupo, ni imani tu

Sasa unatumia Mbinu gani? Mana Mimi naamini uchawi upo Sasa Nataka niitoe iyo mind set, hafu nione matokeo yake.
Yaani mkuu,utafanikiwa sana kwasababu hutaogopa chochote wala yeyote,isipokuwa Mungu,watu utawaheshimu na siyo kuwaogopa,ktk maamuzi hutatetereka,utafanya tu kwa kujiamini bila kuogopa yeyote ili mradi upo ktk Haki na usawa na busara ikitumika.Kuhusu mbinu Sali sana,Sana maandiko matakatifu,izoeze akili yako kufikiri positive juu ya mambo mbalimbali.
 
kwanini uchawi usiwepo halafu imani iwepo ?

kwanini tena useme uchawi ni imani?
Namaanisha kuwa Uchawi km Uchawi kwa wenyewe haupo,isipokuwa akili za watu zinazowaza uchawi hupelekea kitu hicho kuaminika kuwa kipo kumbe si kweli,ni mambo ya kufikirika tu!,hamna lolote.
 
Namaanisha kuwa Uchawi km Uchawi kwa wenyewe haupo,isipokuwa akili za watu zinazowaza uchawi hupelekea kitu hicho kuaminika kuwa kipo kumbe si kweli,ni mambo ya kufikirika tu!,hamna lolote.
na kwanini ukatae imani za watu wengine?
acha wafu wazikane mkuu
 
Unasema uchawi haupo halafu unapeleka mbegu kwa padre......we ungejilimia tu freestyle
Baraka ya watu,vitu,n.k.ni kawaida kwa Imani yangu km Mkristo Mkatoliki,nafanya hivyo km ishara ya kumkabidhi Mungu jitihada zangu ili kupitia maombi ya Mtumishi wake niweze kufanikiwa.
 
Unakosea jambo moja la msingi sana: ni kwamba uchawi upo, ila hauwezi kuwadhuru walio na imani katika Yesu Kristo, kama ulivyo wewe. Ukweli ndugu yangu uchawi upo kabisa na ni matumizi ya nguvu za giza kama mapepo, majini nk wakishirikiana na wachawi. Hata wewe leo hii ukimwasi Yesu utalogwa kirahisi. Kwa hivyo usichanganye kati ya kutokuwepo kwa uchawi na wachawi kushindwa kumloga mtu ni vitu viwili tofauti sana. Hata Biblia inazungumzia habari za wachawi kufany miujiza yao ya kichawi kwa kutumia nguvu za giza.
Mkuu,nimesema Uchawi km uchawi haupo,kilichopo ni ile hali ya watu kuamini kuhusu uchawi,namna walivyoziseti akili zao.Uchawi ni kitu cha kufikirika tu ukikiwazia sana lazima kikupelekeshe mpeta mpeta,lkn km huna mawazo kuhusu huo uchawi mbona utapeta sana.
 
Ukihoji Watu kumi wakuambie shida zao kubwa mbili watakwambia ni umaskini wa pesa na maradhi yaani wanahitaji afya.hakuna atakayekutajia uchawi unamsumbua...uchawi ni kushindwa kuelezea mabadiliko Fulani Fulani ya ki chemistry yenye uwezekano wa kutokea ulimwenguni.hakuna uchawi hata kidogo isipokuwa Kuna Watu wanaojidanganya kuufanya uchwihuku wakisubiri matokeo na hayatokei hao no waabudu sanamu Bila wao kujua

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Amen.Asante mkuu kwa mchango wako.
 
Sadaka tunatuma wapi? Au comments zitahesabika kama sadaka
Mkuu mimi sipokei sadaka,ninachoweza kukuambia km umewiwa kutoa sadaka,basi chukua sadaka yako wapelekee wahitaji,naamini Mungu atapendezwa na jambo hilo.
 
Back
Top Bottom