Uchambuzi wa mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga SC na kampuni ya Sportpesa

Mr mutuu

JF-Expert Member
Jan 27, 2023
2,000
9,940
Wasaalam,

Kila siku tumekua tukisema hakuna kitu kibaya kama kufanya mikataba ya kisirisiri, tatizo Hili kubwa halipo kwenye mpira tu Bali hata kwenye mikataba ya kiserikali, wananchi ndio tuna dhamana na nchi yetu na ndio walipa Kodi lakini watu wachache wanaingia mikataba au mikopo kisirisiri bila kuwapo na uwazi hata kidogo, utaskia tumeingia mkataba na nchi flani wenye dhamani ya trillion kadhaa, au tumechukua mabilioni kadhaa ya mkopo kutoka nchi flani huku sisi walipaji wa Hio mikopo hatujui vipengele Wala masharti ya mkopo huo


Tukirudi kwenye swala la Yanga, Mimi napenda kua neutral kwenye swala Hili, sielewi nani hasa ndio mwenye makosa kati ya club au Sportpesa!

Siri ambayo wengi hawaijui ni kua kwenye mashindano ya CAF yoyote, iwe CAF champions league au CAF confederation cup Simba SC au Yanga SC hawawezi kuitumia logo ya mdhamini wao mkuu Sportpesa!

Hii inatokana na kua muandaaji wa mashindano hayo 'CAF' tayari ana mkataba na kampuni ya kubet kutoka Russia 1xbet kama mmoja wa official sponsors wa michuano yoyote ya CAF! Kwa io huyu 1xbet ni part wa main sponsors kama walivyo Total energies!

Mkataba ambao 1xbet waliingia na CAF ni kua hakuna timu inayodhaminiwa na kampuni yoyote ya betting itatumia logo ya kampuni hizo kwenye michuano ya CAF ndio maana tunaona Simba SC alikua anatumia 'Visit Tanzania' kwenye michuano ya CAF..

Sportpesa sio wageni kwenye migogoro hii maana mwaka 2019 utata ulianza pale club ya Gor mahia walipozuiliwa kuitumia logo ya Sportpesa aliyekua mdhamini wao kipindi hicho, hii ilitokana na malalamiko kutoka 1xbet kua hataki Kuona wapinzani wake(kampuni za kubet) wakijibrand kupitia michuano anayoidhamini.. kitu kilochopelekea Gor mahia kucheza mechi ya marudio na zamalek na shirt zisizokua na logo mechi iliyofanyika Kenya na Gor mahia kushinda goli 4-2

Gor mahia alitafuta wadhamini wengine bila mafanikio ikabidi wawe wanacheza mechi zao bila kutumia logo yoyote!


Screenshot_20230202-122343~2.jpg
Wachezaji wa Gor mahia kwenye michuano ya ndani

Screenshot_20230202-122416~2.jpg


Wachezaji wa Gor mahia kwenye michuano ya CAF

Swali ninalojiuliza.. kama Sportpesa walikua wameshawahi kupitia mgogoro huu 2019, mpaka Leo kwenye mkataba wao na Yanga au Simba Hilo swala watakua hawakuliweka sawa ili kuzuia Hili liliotokea sasa ivi? Au Kuna loopholes waliziacha Yanga wakaliona Hili wakaamua kupitia hapohapo


Kuna mtu atauliza mbona mechi za mtoano kama Yanga aliocheza na Al hilal mbona walitumia logo ya Sportpesa, jibu ni kua hizo mechi CAF Hana mamlala nazo na ndio maana hata haki za matangazo ya kurusha mechi alikua anamiliki timu ya nyumbani,

Kuna nchi kama Austria ambao wanaruhusu sponsor mbalimbali kwa timu Moja ila wakienda kucheza UEFA basi inawabidi wawe na sponsor mmoja tu kwa jersey
Screenshot_20230202-124258~2.jpg

hao ni wachezaji wa timu Moja 'wien' ya Austria wakiwa wamevaa shirt zenye sponsor tofauti

Nimeleta hii ili mjue kua swala la sponsor kwenye shirt Kila nchi Ina makubaliano yake, ila ukienda kwenye michuano flani basi lazima ufuate Sheria za huko! Mfano kama england wao wanatumia sponsor mmoja tu kwenye mashindano yote! Mwaka 2010 Kuna timu iliomba kua na sponsor tofauti, yaani epl wamtumie huyu na fa wamtumie mwingine ila wakakataliwa maana Sheria Kule zipo wapi sponsor mmoja kwa mashindano yote


Ukakasi unakuja Yanga hawezi kuvaa logo ya Sportpesa kwenye CAF, Yanga nao hawataki kuvaa visit Tanzania kama ambavyo Sportpesa walidhani, sijajua kwanini ila nahisi Itakua mambo ya ki maslahi tu maana sidhani kama Simba alivaa Bure pia, kama hawakusema walipewa chochote basi Kuna watu walipiga pesa hapa, maana Kuna kitengo Cha kutangaza utalii kina bajeti zake kubwa tu, rejea Rwanda wanalipa mabilioni kwa arsenal na psg wakivaa 'visit Rwanda'

Sababu kubwa ya epl kukataa timu kuvaa logo tofauti hata kwenye michuano ya kimataifa ni kua italeta ukakasi sana! Na Hili ndo litakuja kujitokeza kwa Yanga! Mfano Yanga wanavyofanya promotion zao au wakihudhuria shughuli nyingine za kijamii watatumia shirt zenye logo ipi? Tumeshaona jersey zenye logo nyingine zishaanza kuuzwa Hili nalo halijakaa sawa kwa Sportpesa kibiashara!!

Rushwa kwa wachezaji itajipenyeza kwa Kasi maana Kila kampuni sasa kati ya Sportpesa au haier italazimika kuwahonga either wachezaji au watu wenye influence kuzivaa jezi zenye logo zao wakiwa hawapo uwanjani au kuzipost kwenye social media ili wajitangaze zaidi


CAF wao hawawezi kumpangia Yanga logo atayovaa kama Haingilii maslahi Yao na kama hajavunja masharti na mdhamini wao Sportpesa! Sasa na jukumu la Yanga na Sportpesa kuacha usiri na kutuambia 'live' je mkataba baina Yao unasemaje? Kama Sportpesa walijua Yanga hawezi kuvaa logo yao kimataifa je walimbana asije akavaa nyingine?au wali assume atavaa visit Tanzania kama Simba so hawakuligusia Hili?kama walijisahu basi Hio ni loophole Yanga atakua kapita nayo


Ifike muda waweke usiri pembeni waletee mikataba mezani tujue kipi ni kipi, maana wananchi washaanza kununua jersey ili Hali Kuna Hali ya sintofahamu
 
Jibu kwa hoja, wewe kumbuka ni kati ya member wakongwe huku ila unajishushia heshima kwa majibu kama haya
Hebu ainisha hizo hoja,naona kama uneongea-ongea tu. Unauliza kama Sportpesa walimbana Yanga asivae logo nyingine kimataifa. Wakati unaelewa kabisa hizo ndiyo claims za Sportpesa kuvaa logo aliyozuiwa bila ridhaa yao, na Yanga ndiyo ilichokiomba Sportpesa na ikakataliwa. Na Yanga haijapingana na hilo mpaka leo.

Sasa hapo tunajadili nini. Mngeacha kuzunguka badala yake muitake Yanga kuacha uhuni na kuzingatia masharti ya mkataba wake na SportPesa. Mashabiki mna wajibu wa kuwawajibisha viongozi.
 
Hebu ainisha hizo hoja,naona kama uneongea-ongea tu. Unauliza kama Sportpesa walimbana Yanga asivae logo nyingine kimataifa. Wakati unaelewa kabisa hizo ndiyo claims za Sportpesa kuvaa logo aliyozuiwa bila ridhaa yao, na Yanga ndiyo ilichokiomba Sportpesa na ikakataliwa.

Sasa hapo tunajadili nini
Kama Kuna kipengele hicho basi wakiweke wazi, na Kila mkataba unakua na measures ambazo mmekubaliana pande zote pindi iwapo mmoja akikiuka

Nilitegemea Sportpesa wachukue hizo measures sio kuja kulia mitandaoni
 
Kama Kuna kipengele hicho basi wakiweke wazi, na Kila mkataba unakua na measures ambazo mmekubaliana pande zote pindi iwapo mmoja akikiuka

Nilitegemea Sportpesa wachukue hizo measures sio kuja kulia mitandaoni
Pengine husomi hata claims za Sportpesa. Mbona wameeleza yote hayo na wamesisitiza kuchukua hatua. Ushabiki umekufanya uone Sportpesa inalialia. Badala ya haki ya kutoa taarifa kwa vyombo vya habari.
Hatimaye rangi yako halisi imejidhihirisha. Upo upande gani

Maelezo ya SportPesa

Sisi tunajua kuwa hatua ya makundi hatuwezi kukaa kwenye jezi za Yanga na tulijadiliana cha kufanya ikiwamo kuwapa LiveScore ambayo walisema inahusika na beting na imekataliwa na CAF, tukaomba ushahidi wa maandishi kwa kujua hii inaonyesha matokeo ya mechi na sio kubeti,” amesema Sabrina na kufafanua kuwa, wakati wakisubiri kujua cha kufanya wakaona wenzao usiku wakizindua jezi na kumtangaza mdhamini mpya.

Amesema, tayari wameanza kuchukua Hatua ya kuhifadhi haki yake kutoka kwa mamlaka, kwa kuzingatia wana mkataba na haki ya kuwa kifuani mwa jezi za Yanga kwa miaka ya soka ya 2022 -2025.
 
Kama Kuna kipengele hicho basi wakiweke wazi, na Kila mkataba unakua na measures ambazo mmekubaliana pande zote pindi iwapo mmoja akikiuka

Nilitegemea Sportpesa wachukue hizo measures sio kuja kulia mitandaoni
Una.uhakika gani kama hawachukui hatua? Unachokiona mitandaoni ni sehemu ndogo sana ya kinachoendelea katika huu mgogoro kwa sasa.Muda utaongea na utarudi hapa kutuambia kama Sportpesa walikuwa wanalia tu mitandaoni.
 
Sijaona uchambuzi wowote.

Nilitegemea kuona vifungu vya Kimkataba baina ya Sportpesa na Yanga vinavyoainisha ni namna gani scenario kama hiyo inavyopaswa kuwa.
Vinginevyo ni kelele nyingi tu zisizo na maana..

Yanga kavunja makubaliano. Kama kulikuwa na loophole ya kujipitisha, basi wasingewaconsult Sportpesa.

Kwenda kuonana na Sportpesa inaonyesha wazi kuwa kuna kipengele katika mkataba wao kinawabana..

Kwa nini Sportpesa hataki kampuni ya Haier iwekwe kifuani. Sababu ni moja tu, Yanga haitaitangaza Sportpesa ipasavyo.

Ukweli ni kuwa, jezi zenye logo ya Haier zitauzika zaidi kuliko jezi zenye logo ya Sportpesa. Kwa sababu ipo idadi kubwa tu ya watu wasiovaa jezi zenye logo za kampuni za kubashiri.

Lakini pia, jezi za michuano ya Kimataifa zinaonekana kuwa na mvuto zaidi kuliko zile za Michuano ya ndani.

Hilo halitoshi, watu wana mindset za kujaribu vitu vipya zaidi. Sportpesa ishavaliwa sana, mtu ana jezi zao nyingi. Kuja kwa kampuni nyingine, kunampa mtu fursa ya kununua jezi ya tofauti na hivyo kuitangaza kampuni husika zaidi.

Ni sawa na kusema Sportpesa alilipa kiasi kikubwa cha fedha huku Haier akilipa kiwango kidogo, huku wote wakipewa haki sawa za kujitangaza.

Sawa, utasema siyo wapinzani (Haier na SP). Lakini kampuni nyingine haipaswi kunufaika kwa sababu ya mkataba wa michuano mingine.
Sportpesa waliwapa Option ya Visit Tanzania, kwa sababu yenyewe si kampuni. Na wala haimnufaishi mtu mwingine yeyote isipokuwa Taifa zima.

Tusubiri tuone.
 
Sijaona uchambuzi wowote.

Nilitegemea kuona vifungu vya Kimkataba baina ya Sportpesa na Yanga vinavyoainisha ni namna gani scenario kama hiyo inavyopaswa kuwa.
Vinginevyo ni kelele nyingi tu zisizo na maana..

Yanga kavunja makubaliano. Kama kulikuwa na loophole ya kujipitisha, basi wasingewaconsult Sportpesa.

Kwenda kuonana na Sportpesa inaonyesha wazi kuwa kuna kipengele katika mkataba wao kinawabana..

Kwa nini Sportpesa hataki kampuni ya Haier iwekwe kifuani. Sababu ni moja tu, Yanga haitaitangaza Sportpesa ipasavyo.

Ukweli ni kuwa, jezi zenye logo ya Haier zitauzika zaidi kuliko jezi zenye logo ya Sportpesa. Kwa sababu ipo idadi kubwa tu ya watu wasiovaa jezi zenye logo za kampuni za kubashiri.

Lakini pia, jezi za michuano ya Kimataifa zinaonekana kuwa na mvuto zaidi kuliko zile za Michuano ya ndani.

Hilo halitoshi, watu wana mindset za kujaribu vitu vipya zaidi. Sportpesa ishavaliwa sana, mtu ana jezi zao nyingi. Kuja kwa kampuni nyingine, kunampa mtu fursa ya kununua jezi ya tofauti na hivyo kuitangaza kampuni husika zaidi.

Ni sawa na kusema Sportpesa alilipa kiasi kikubwa cha fedha huku Haier akilipa kiwango kidogo, huku wote wakipewa haki sawa za kujitangaza.
BABU HUU UZI UMEUMALIZA VIZURI SANA. TUFANYE MAMBO MENGINE SASA
 
Wasaalam,

Kila siku tumekua tukisema hakuna kitu kibaya kama kufanya mikataba ya kisirisiri, tatizo Hili kubwa halipo kwenye mpira tu Bali hata kwenye mikataba ya kiserikali, wananchi ndio tuna dhamana na nchi yetu na ndio walipa Kodi lakini watu wachache wanaingia mikataba au mikopo kisirisiri bila kuwapo na uwazi hata kidogo, utaskia tumeingia mkataba na nchi flani wenye dhamani ya trillion kadhaa, au tumechukua mabilioni kadhaa ya mkopo kutoka nchi flani huku sisi walipaji wa Hio mikopo hatujui vipengele Wala masharti ya mkopo huo


Tukirudi kwenye swala la Yanga, Mimi napenda kua neutral kwenye swala Hili, sielewi nani hasa ndio mwenye makosa kati ya club au Sportpesa!

Siri ambayo wengi hawaijui ni kua kwenye mashindano ya CAF yoyote, iwe CAF champions league au CAF confederation cup Simba SC au Yanga SC hawawezi kuitumia logo ya mdhamini wao mkuu Sportpesa!

Hii inatokana na kua muandaaji wa mashindano hayo 'CAF' tayari ana mkataba na kampuni ya kubet kutoka Russia 1xbet kama mmoja wa official sponsors wa michuano yoyote ya CAF! Kwa io huyu 1xbet ni part wa main sponsors kama walivyo Total energies!

Mkataba ambao 1xbet waliingia na CAF ni kua hakuna timu inayodhaminiwa na kampuni yoyote ya betting itatumia logo ya kampuni hizo kwenye michuano ya CAF ndio maana tunaona Simba SC alikua anatumia 'Visit Tanzania' kwenye michuano ya CAF..

Sportpesa sio wageni kwenye migogoro hii maana mwaka 2019 utata ulianza pale club ya Gor mahia walipozuiliwa kuitumia logo ya Sportpesa aliyekua mdhamini wao kipindi hicho, hii ilitokana na malalamiko kutoka 1xbet kua hataki Kuona wapinzani wake(kampuni za kubet) wakijibrand kupitia michuano anayoidhamini.. kitu kilochopelekea Gor mahia kucheza mechi ya marudio na zamalek na shirt zisizokua na logo mechi iliyofanyika Kenya na Gor mahia kushinda goli 4-2

Gor mahia alitafuta wadhamini wengine bila mafanikio ikabidi wawe wanacheza mechi zao bila kutumia logo yoyote!


View attachment 2503554Wachezaji wa Gor mahia kwenye michuano ya ndani

View attachment 2503556


Wachezaji wa Gor mahia kwenye michuano ya CAF

Swali ninalojiuliza.. kama Sportpesa walikua wameshawahi kupitia mgogoro huu 2019, mpaka Leo kwenye mkataba wao na Yanga au Simba Hilo swala watakua hawakuliweka sawa ili kuzuia Hili liliotokea sasa ivi? Au Kuna loopholes waliziacha Yanga wakaliona Hili wakaamua kupitia hapohapo


Kuna mtu atauliza mbona mechi za mtoano kama Yanga aliocheza na Al hilal mbona walitumia logo ya Sportpesa, jibu ni kua hizo mechi CAF Hana mamlala nazo na ndio maana hata haki za matangazo ya kurusha mechi alikua anamiliki timu ya nyumbani,

Kuna nchi kama Austria ambao wanaruhusu sponsor mbalimbali kwa timu Moja ila wakienda kucheza UEFA basi inawabidi wawe na sponsor mmoja tu kwa jersey
View attachment 2503560
hao ni wachezaji wa timu Moja 'wien' ya Austria wakiwa wamevaa shirt zenye sponsor tofauti

Nimeleta hii ili mjue kua swala la sponsor kwenye shirt Kila nchi Ina makubaliano yake, ila ukienda kwenye michuano flani basi lazima ufuate Sheria za huko! Mfano kama england wao wanatumia sponsor mmoja tu kwenye mashindano yote! Mwaka 2010 Kuna timu iliomba kua na sponsor tofauti, yaani epl wamtumie huyu na fa wamtumie mwingine ila wakakataliwa maana Sheria Kule zipo wapi sponsor mmoja kwa mashindano yote


Ukakasi unakuja Yanga hawezi kuvaa logo ya Sportpesa kwenye CAF, Yanga nao hawataki kuvaa visit Tanzania kama ambavyo Sportpesa walidhani, sijajua kwanini ila nahisi Itakua mambo ya ki maslahi tu maana sidhani kama Simba alivaa Bure pia, kama hawakusema walipewa chochote basi Kuna watu walipiga pesa hapa, maana Kuna kitengo Cha kutangaza utalii kina bajeti zake kubwa tu, rejea Rwanda wanalipa mabilioni kwa arsenal na psg wakivaa 'visit Rwanda'

Sababu kubwa ya epl kukataa timu kuvaa logo tofauti hata kwenye michuano ya kimataifa ni kua italeta ukakasi sana! Na Hili ndo litakuja kujitokeza kwa Yanga! Mfano Yanga wanavyofanya promotion zao au wakihudhuria shughuli nyingine za kijamii watatumia shirt zenye logo ipi? Tumeshaona jersey zenye logo nyingine zishaanza kuuzwa Hili nalo halijakaa sawa kwa Sportpesa kibiashara!!

Rushwa kwa wachezaji itajipenyeza kwa Kasi maana Kila kampuni sasa kati ya Sportpesa au haier italazimika kuwahonga either wachezaji au watu wenye influence kuzivaa jezi zenye logo zao wakiwa hawapo uwanjani au kuzipost kwenye social media ili wajitangaze zaidi


CAF wao hawawezi kumpangia Yanga logo atayovaa kama Haingilii maslahi Yao na kama hajavunja masharti na mdhamini wao Sportpesa! Sasa na jukumu la Yanga na Sportpesa kuacha usiri na kutuambia 'live' je mkataba baina Yao unasemaje? Kama Sportpesa walijua Yanga hawezi kuvaa logo yao kimataifa je walimbana asije akavaa nyingine?au wali assume atavaa visit Tanzania kama Simba so hawakuligusia Hili?kama walijisahu basi Hio ni loophole Yanga atakua kapita nayo


Ifike muda waweke usiri pembeni waletee mikataba mezani tujue kipi ni kipi, maana wananchi washaanza kununua jersey ili Hali Kuna Hali ya sintofahamu
Umeeleza vizuri sana, mkataba unahusu pande mbili, na kila upande unatakiwa kuheshimu makubaliano.
Mpaka sasa wote yanga na sportpesa wanajitetea kwa hoja nyepesi kwa jamii, lakini ninaamini wao wanajua wapi kuna tatizo.

Ninaamini hili swala litaisha kibusara zaidi kuliko kisheria, kwasababu bado wana mkataba na kila mmoja anamhitaji mwenzake.
 
Umeeleza vizuri sana, mkataba unahusu pande mbili, na kila upande unatakiwa kuheshimu makubaliano.
Mpaka sasa wote yanga na sportpesa wanajitetea kwa hoja nyepesi kwa jamii, lakini ninaamini wao wanajua wapi kuna tatizo.

Ninaamini hili swala litaisha kibusara zaidi kuliko kisheria, kwasababu bado wana mkataba na kila mmoja anamhitaji mwenzake.
Kitu nilichojifunza kuhusu mashabiki wa simba., kwa msimu washajua hakuna uwezekano wa wao kuchukua kombe lolote mbele ya yanga hapa ndani kwa sababu wamezidiwa kiubora na miaka ya karibuni wamekua hawapati matokeo mazuri kila wanapokutana na yanga na uko CAF hawana timu ya kuchukua huo ubingwa jamaa wanajua msimu huu watamaliza watupu kwaiyo faraja yao pekee ni kushabikia kila ambacho wanaona akipo sawa upande wa yanga ili kujipa relief ya moyo(wanalazimisha furaha feki) walijifanya mawakili wa feisal TFF ikatoa tamko feisal ni mchezaji wa yanga wameumbuka, sasa hivi wamekua mawakili wa sportpesa tusubiri tuone mwisho wa hili suala litakuaje. Ushauri wangu kwa makolo wote wanapaswa kukubali tu kwa sasa yanga ndie top elite wa soka hapa nchini na wajipe muda wa kujua walikwama wapi walekebishe makosa hizi husda na kulazimisha furaha wanapoona kuna misukosuko kwa mpinzani haitawasaidia chochote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom