Mbegu aliyopanda Maalim, ni mbaya mno. Hata kama hatogombea malalamiko hayatoweza kwisha. Kwani jamaa wa kisiwa cha pili wanaamini kuwa wao ni wengi na wanaweza kushinda chaguzi yoyote ile hapo kisiwani.
Kwa upande mwingine, kinachoangaliwa sasa huko visiwani ni mashindano kati ya kisiwa cha pili na kisiwa cha kwanza, nani zaidi? Hakuna sera wala kampeni ambayo itaweza kubadilisha hilo kwa sasa. Hata iundwe tume huru ya aina yake haitoweza kubadili hilo.
Tume zote zilizopita zimekuwa na wajumbe toka vyama vyote vishiriki uchaguzi, hata hivyo mikwaruzo imeendelea kuwepo vilevile.
Nimeitafuta hio mbegu mbaya ya Seif siioni hapa, lakini CCM ndio wenye mbegu mbaya wanaposema mtu wa kisiwa cha pili haongozi maisha ZANZIBAR, nakumbuka hata katika kampeni zao wakisema
"kama wataka Ikulu, kajenge yako Mtambwe" akiambiwa Seif maneno hayo.
Hivi kuna mbegu mbaya zaidi ya hiyo?
Nakumbuka hata mwakilishi wa CCM (Asha Bakari Makame) ndani ya BARAZA LA WAWAKILISHI alisema:
nchi haikupatikana kwa makaratasi (kura), wao walipigana, so hawatoi nchi.
Hakuna mashindano kati ya visiwa hivi, ila ni sumu ya CCM tu kugawa wananchi wanaposema 'CUF wakipata watavunja MUUNGANO then wataleta WAARABU' kwa vile tu wanataka Serikali tatu, ndio hapo watu wawili watatu wa Unguja wamepigwa changa la macho.
CUF naamini inakuja na sera muafaka na ndio maana inashinda chaguzi zote ila mizengwe tu inatumika kuwachinja. CCM just amani na utulivu then wanajisifia mambo yaliyofanywa na Serikali ya kwanza baada ya Mapinduzi, kwisha sera hapo! Ukiwauliza baada ya 1972, just wanang'aa macho tu, jibu hakuna.
Tume za Uchaguzi zoote feki, hata kuwe na hao wapinzani wawili kama wajumbe haisaidii chochote, kwani hao waliopita mbona walisema kabla ya matokeo ya kuwa taratibu muhimu za kiuchaguzi zimekiukwa, then ikawaje? haikuwa chochote na CCM mbele kwa mbele.
CCM na Serikali ya Zanzibar vyote vinaendeshwa Dodoma, from uchaguzi na uteuzi wa viongozi, hata maamuzi makubwa ya kiserikali kutoka huko pia. Tume ya Uchaguzi nayo inaendeshwa na CCM, maana wao ndio wameiweka.
Mabadiliko ya kisiasa na demokrasia ya kweli yatachukuwa nafasi yake Zanzibar siku tu CCM itapigwa mweleka Bara, ichukue nafasi ya opposition katika Bunge. Bila ya hivyo wacha tuendelee na miafaka kila baada ya miaka mitano.
Mtu wa Pwani ya 1995 ndo hayohayo ya 2010.
Time will tell