Ikulumaliyawananch
JF-Expert Member
- Mar 14, 2018
- 339
- 533
watanzania ni wagumu kupambanunuwa mambo kwelikweli. Nimekuwa nikisikia watanzania wengi wakiwemo wanasiasa wakilaumu wasimamizi wa uchaguzi kwa kuharibu uchaguzi.
Na wengine wakitaka raisi Magufuli atowe tamko la kukemea uchafuzi huo na kuchukuwa hatua dhidi ya walio husika na uhalibifu wa uchaguzi.
Kitu ambacho kinanifanya nijiulize uwezo wetu wa kufikiri uko sawa au ni asiri ya unafiki wa kuogopa kusema ukweli unao tusumbuwa? Inawezakanaje katika miaka minne ya Magufuli hawakuweza kuona mipango yake ya kuharibu na kupora nguvu ya uma kuchaguwa viongozi ?
Yaani mtu apange kwa miaka minne tena hadharani mipango yake na kila mtu akiona halafu mipango imekamirika kama ilivyo pagwa halafu unaenda kwake kumwambia kuwa aharibu alicho kikamilisha kwa sababu sio kizuri kwako?
Kwa uwazi bila unafiki ni kwamba hiki kilicho tokea kwenye mchakato wa uchaguzi wa Serikali za mitaa hakikutokea kwa bahati mbaya wala hao watendaji wa kata na vitogoji walio amuwa kufunga office wakati wa kurejesha form hawakujiamlia kufanya hivyo wala hawakuwekwa kwenye nafasi zao kwa bahati mbaya.
Hawa watendajii walipewa instructions na wamefuwata maelekezo kwa ufasaha mkubwa sana. sasa kulaumu mtu aliye fuwata maelekezo kwa umakini unakuwa unamuonea. Au kumwambia mtu aliye andaa maelekezo kuwa maelekezo yake yameeleweka vizuri na walio pewa maelekezo wameyafanyia kazi vizuri.
Wapizanii na watanzania watakuwa ni kituko kama watakubali suluhisho litakalo pendekezwa na aliye panga kwa miaka minne kupora wananchi mamraka yao ya kuchaguwa viogozi wanaowataka na kujipa mwenyewe uwezo wa kuteuwa viongozi wote anao wataka yeye na si vingenevyo. hapa suluhisho ni katiba mpya na tume huru.
Jinsi ya kupata vitu hivi viwili sio kwa kumbembeleza Magufuli na serikali yake, bali ni kuvidayi kwa gharama yoyote bila hofu wala woga.
Na hapa ndio tutakapo wakumbusha watawala kuwa Tanzania ni mali ya watanzania na sio ya watawala. haiwezekani mtawala anafikia hatuwa ya kudharau wananchi kiasi hiki halafu tukaendelea kucheka naye.
Anatumia kodi zetu kutuchagulia nani aongoze maisha yetu kama vile maisha yetu ni kama magari yake anaweka dreva anaye mtaka yeye. Tukiendelea kucheka na watawala wa aina hii ipo siku tutapangiwa mda wa kulala na mda wa kuongea.
Na wengine wakitaka raisi Magufuli atowe tamko la kukemea uchafuzi huo na kuchukuwa hatua dhidi ya walio husika na uhalibifu wa uchaguzi.
Kitu ambacho kinanifanya nijiulize uwezo wetu wa kufikiri uko sawa au ni asiri ya unafiki wa kuogopa kusema ukweli unao tusumbuwa? Inawezakanaje katika miaka minne ya Magufuli hawakuweza kuona mipango yake ya kuharibu na kupora nguvu ya uma kuchaguwa viongozi ?
Yaani mtu apange kwa miaka minne tena hadharani mipango yake na kila mtu akiona halafu mipango imekamirika kama ilivyo pagwa halafu unaenda kwake kumwambia kuwa aharibu alicho kikamilisha kwa sababu sio kizuri kwako?
Kwa uwazi bila unafiki ni kwamba hiki kilicho tokea kwenye mchakato wa uchaguzi wa Serikali za mitaa hakikutokea kwa bahati mbaya wala hao watendaji wa kata na vitogoji walio amuwa kufunga office wakati wa kurejesha form hawakujiamlia kufanya hivyo wala hawakuwekwa kwenye nafasi zao kwa bahati mbaya.
Hawa watendajii walipewa instructions na wamefuwata maelekezo kwa ufasaha mkubwa sana. sasa kulaumu mtu aliye fuwata maelekezo kwa umakini unakuwa unamuonea. Au kumwambia mtu aliye andaa maelekezo kuwa maelekezo yake yameeleweka vizuri na walio pewa maelekezo wameyafanyia kazi vizuri.
Wapizanii na watanzania watakuwa ni kituko kama watakubali suluhisho litakalo pendekezwa na aliye panga kwa miaka minne kupora wananchi mamraka yao ya kuchaguwa viogozi wanaowataka na kujipa mwenyewe uwezo wa kuteuwa viongozi wote anao wataka yeye na si vingenevyo. hapa suluhisho ni katiba mpya na tume huru.
Jinsi ya kupata vitu hivi viwili sio kwa kumbembeleza Magufuli na serikali yake, bali ni kuvidayi kwa gharama yoyote bila hofu wala woga.
Na hapa ndio tutakapo wakumbusha watawala kuwa Tanzania ni mali ya watanzania na sio ya watawala. haiwezekani mtawala anafikia hatuwa ya kudharau wananchi kiasi hiki halafu tukaendelea kucheka naye.
Anatumia kodi zetu kutuchagulia nani aongoze maisha yetu kama vile maisha yetu ni kama magari yake anaweka dreva anaye mtaka yeye. Tukiendelea kucheka na watawala wa aina hii ipo siku tutapangiwa mda wa kulala na mda wa kuongea.