utaifakwanza
JF-Expert Member
- Feb 1, 2013
- 14,193
- 2,815
wana JF
mwanzoni mwa mwaka huu kulikuwa na tetesi kwamba uchaguzi wa ndani wa viongozi wa CHADEMA utafanyika kuanzia mwezi wa nne 2013, cha ajabu hivi sasa ni mwisho wa june lakini kimya na hakuna kinachoendelea.
Demokrasia iko wapi ndani ya CHADEMA??? kuna rafiki yangu nlikuwa naongea naye kuhusu hili akasema uchaguzi wa nini wakati viongozi wapo?? je hilo jibu ni sahihi kwamba mfumo wa kifalme umerudi Tanzania? Tumezoea kumsikia Augostino Lyatonga Mrema akiwa mwenyekiti wa TLP tangu ahamie chama hicho miaka zaidi ya 15, John cheyo wa UDP na Prof Lipumba ni mwenyekiti wa kudumu wa CUF.
Je hivi vyama ni wale wale??
mwanzoni mwa mwaka huu kulikuwa na tetesi kwamba uchaguzi wa ndani wa viongozi wa CHADEMA utafanyika kuanzia mwezi wa nne 2013, cha ajabu hivi sasa ni mwisho wa june lakini kimya na hakuna kinachoendelea.
Demokrasia iko wapi ndani ya CHADEMA??? kuna rafiki yangu nlikuwa naongea naye kuhusu hili akasema uchaguzi wa nini wakati viongozi wapo?? je hilo jibu ni sahihi kwamba mfumo wa kifalme umerudi Tanzania? Tumezoea kumsikia Augostino Lyatonga Mrema akiwa mwenyekiti wa TLP tangu ahamie chama hicho miaka zaidi ya 15, John cheyo wa UDP na Prof Lipumba ni mwenyekiti wa kudumu wa CUF.
Je hivi vyama ni wale wale??
Mleta mada naomba nikupe jibu sahihi.
Viongozi walioko madarakani walichaguliwa mwaka 2009 na kipindi chao kinaisha mwaka 2014 tena mwishoni. Sasa uchaguzi kufanyika mwaka huu wa 2013 ni uamuzi wa busara wa viongozi wetu kuwahisha uchaguzi kwa ili kutobananisha uchaguzi wa ndani ya chama na uchaguzi wa serikali ya mtaa.
Kwa hiyo, wadau badala ya kuwashambulia viongozi wetu wangekuwa wanatumia mashambulio hayo kuandika vitu vya ukweli na pongezi nyingi kwa viongozi kupunguza muda wao wa uongzi kwa mwaka mmoja kwa malahi ya chama. Huu ndio ukweli wa 100%. Sina hakika kama viongozi wa ccm wanaliweza hilo.