Elections 2010 Uchaguzi mdogo Igunga: Kipimo tosha kwa vyama hasimu

Tabora kwa ujumla imekuwa ngome ya CCM kwa muda mrefu, na ukiangalia hakuna jimbo lolote lililowahi kuchukuliwa na chama chochote zaidi ya CCM. pamoja na miundombinu duni na huduma mbovu katika mkoa wa Tabora bado watu wake wamekuwa hawana mawazo mbadala zaid ya kuchagua CCM. Tabora ni moja ya mikoa iliyonyuma sana katika huduma nyingi za kijamii na maendeleo kwa ujumla huu ni mkoa kati ya mikoa maskin katika nchi hii, lakini kuna mambo mengi yanatokea lakin nina mashaka kama wana Tabora wako tayari kuchagua vyama pinzani hili linatokana na sababu mbalimbali ikiwamo uduni wa elimu na umasikini hasa sehemu za vijijini. Lakin hilo halina maana kuwa vyama vya upinzani hawawezi kushinda najaribu kutoa mtizamo wangu.ninachowashauri vyama vyingine vitafute au viweke wagombe wenye sifa na upeo na wanaokubalika na wananchi vinginevyo jimbo hili litarudi mikononi mwa CCM. Katika kampeni za mwaka jana CCM ilishinda majimbo yote kwa urahisi kwakuwa vyama vingine vilikuwa na wagombea wengi wasio na sifa na upeo mkubwa na walikuwa hawakubaliki.Nilikuwa Tabora muda huo.

Ni mtizamo tu.
Mtazamo wako uko sahihi,uchaguzi huu utatoa picha kama kweli hawa ndugu zetu wanyamwezi/sukuma wamebadilika kama ilivyokuwa kanda ya ziwa.Hakika umaskini na elimu ni chanzo cha mgando wa fikra.
 
Kwa vyovyote itakavyokuwa Igunga patachimbika vibaya.Na maajabu ni kwamba ni miongoni mwa mikoa ambayo hutoa wabunge wengi wenye asili ya kiasia.
 
kumbukumbu zinaonyesha siyo kweli tabora hakujawahi kuwa na upinzani,muulize spika aliyepita/chakachuliwa mzee 6 atakupa stori kwa jimbo la Urambo Mashariki mwaka 1995
 
kumbukumbu zinaonyesha siyo kweli tabora hakujawahi kuwa na upinzani,muulize spika aliyepita/chakachuliwa mzee 6 atakupa stori kwa jimbo la Urambo Mashariki mwaka 1995
Lakini si ni mara moja tu mkuu wakati NCCR ikiwa na nguvu?Kwa mkoa wenye majimbo mengi kama huo ilitakiwa wengi wawe walishalamba sakafu.,Kila la heri upinzani.
 
Kwa mujibu wa gazeti la Mwanahalisi ya lililo sokoni ni kwamba Ristam yuko Igunga kuwapa tafu chama twawala.
 
Rostam kupiga tafu chama tawala sio kwamaba anapenda bali imemlazimu ameshinikizwa la sivyo biashara zake zitayumbishwa.
 
Rostam kupiga tafu chama tawala sio kwamaba anapenda bali imemlazimu ameshinikizwa la sivyo biashara zake zitayumbishwa.
Wakati anawaaga wazee na wananchi wa IGUNGA alisema "ATABAKI KUWA MWANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI" moja ya majukumu ya KADA wa CHAMa CHOCHOTE CHA SIASA NI kukipigania CHAMA CHAKE DHIDI ya WAPINZANI.
TABORA ina historia tofauti za kisiasa katika nchi hii. Uchaguzi wa mwaka jana Pamoja na tuhuma nzito (za ufisadi)kwa Rostam naamini ni miongoni mwa wabunge waliopata kura nyingi. CHADEMA ili kushinda IGUNGA fanyeni kampeni za KISAYANSI. MH WENJE WA NYAMAGANA AWASAIDIE NI MIONGONI MWA WANASIASA WAJANJA SANA JAPO KIJANA MDOGO. Wanyamwezi hawapendi matusi, wala fujo ni kama ndugu zao Wasukuma. Siasa za manguvu zipo MARA.
 
Wakati anawaaga wazee na wananchi wa IGUNGA alisema "ATABAKI KUWA MWANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI" moja ya majukumu ya KADA wa CHAMa CHOCHOTE CHA SIASA NI kukipigania CHAMA CHAKE DHIDI ya WAPINZANI.
TABORA ina historia tofauti za kisiasa katika nchi hii. Uchaguzi wa mwaka jana Pamoja na tuhuma nzito (za ufisadi)kwa Rostam naamini ni miongoni mwa wabunge waliopata kura nyingi. CHADEMA ili kushinda IGUNGA fanyeni kampeni za KISAYANSI. MH WENJE WA NYAMAGANA AWASAIDIE NI MIONGONI MWA WANASIASA WAJANJA SANA JAPO KIJANA MDOGO. Wanyamwezi hawapendi matusi, wala fujo ni kama ndugu zao Wasukuma. Siasa za manguvu zipo MARA.
Kweli,lakini wasukuma wamebadilika sana siku hizi.
 
Mlioko huko au wenye vyanzo vya uhakika vipi dalili ya vyama kupata ushindi?
 
Wadau niwadokeze tuu mtazamo wangu kama cdm ikishinda igunga kama inavyoelezwa na wadau kuna uwezekano mkubwa wa chama hiki kuchukua dola 2015. Upi mtazamo wenu?
 
Back
Top Bottom