Uchaguzi 2010: Masilahi Ya Taifa Kwanza!

Wazee kama Butiku wanafaa sana kuwa washauri kwa Rais aliye madarakani. Kinachowafanya wawe na ujasiri wa kuongea bila woga ni uzoefu na uelewa wao kwa kina kuhusu masuala ya Serikali. Inasikitisha sana kuona jinsi ambavyo viongozi wanaokuwa madarakani wanavyowapuuza wazee kama wale waliokuwepo kwenye lile Kongamano la Taasisi ya Mwalimu Nyerere. Wazee wale na wengine ambao wameishakuwa viongozi wa nchi hii katika ngazi mbalimbali wanao uzoefu wanajua lipi jema na lipi baya kwa nchi yetu. Wakizungumza kwa ujasiri wanazungumza kwa manufaa ya Taifa na si kwa manufaa yao binafsi. Sidhani kwamba mtu kama Mzee Butiku, Mzee Lusinde, Mzee Mwakawago, Mzee Salim, Mzee Warioba au mtu kama Mzee Msuya na wengine wa aina yao, wanaweza wakaweka maslahi yao mbele kuwaza kuwa na agenda ya kutaka u-Rais wa nchi zaidi ya kuangalia mustakabali wa Taifa letu!!

Hata hivyo, wakigombea u-rais wanaweza kuwa marais wazuri sana kwa sababu wanajua nchi yetu inahitaji nini. Kama Mwai Kibaki ni Rais kwa nini isiwe wao?

- Mkuu heshima mbele sana, Unayosema ndiyo hasa ninayosema kwamba wa-Tanzania hatuwezi kuwapuuza hawa Butiku na Quaresi, kwa sababu wananchi wengi tunaonekana kushindwa kuelewa the impact of what they did hasa politically, ukweli ni kwamba wamem-bring down to his knees Rais wa jamhuri yetu.

- I mean huyu Rais kila analoshauriwa na tuliowapa dhamana za uongozi kitaifa hataki kuwasikiliza, wabunge wakimshauri hataki kusikia lakini get this, safari hii amewasikia hawa wawili na kujibu tena kwa hasira sana na hata kuvunja safari yake ambayo alijigamba sana kwamba haina mbadala lazima atenda Denmark, sasa hatuwezi kuwachukulia lightly hawa Butiku na Quaresi!

- Wamesimama na kuhesabiwa tena katika hiki kipindi kigumu sana kujua nani ni nani kutokana na zile tabia zetu wabongo za ukinyonga, ninasema hawa wawili Butiku na Quaresi ni lazima wasimame kugombea something politically, tena Nationally, watu kama Jasusi mlio karibu na hawa wastaafu wetu tafadhali wapeni moyo kwamba kuna wananchi tunaoheshimu mchango wao na tunadhani wanastahili uongozi tena, maana kama ndio hivi ni afadhali twende na wastaafu, kuliko damu mpya inayoogpa kusimama na kuhesabiwa!

- Ni ushauri wangu mdogo na wa bure tu!

Respect.

FMEs!
 
Hivi kama leo JK atasema basi, nani anayeweza kufaa kukalia nafasi hiyo ya juu? Napata shida kuaona mbadala. Naona hizi weakness zilizopo zinaweza kutuletea fisadi katika makucha yake halisi.Hatima ya Taifa itakuwaje?

Tatizo lako unaangalia ndani ya CCM tu na humo unawaona akina Dr. Nchimbi, Dr. Matayo, Dr.Makongoro, Dr. Membe, Dr. ...!!!!

Look at the big picture my friend. TZ in watu 35 000 000 siyo tu hao madoctor feki wa siasa.
 
Wanaogopa kufa ghafla!!!!!!

- Duh! mkuu vipi tena yaani mtu akisema ukweli anaishia kufa? Kwa vipi hiyo? Hawa wakuu ni lazima wachukue fomu za uongozi, wataleta changamoto nzito sana katika mchakato na hasa majina yao yakifika CC, maana Quaresi ni mtu wa Mkapa na Butiku ni mtu wa Mwalimu, patakuwa patamu sana hapo!

Respect.


FMEs!
 
Wakuu tumeanza kuona vioja sasa, badala ya hoja. FMES ameanzisha uzi mzuri sana kuhusu kuelekea 2010. Kama nilivyomwelewa ni kuwa anataka tukumbuku kwamba tunatakiwa kuchagua kiongozi atakayesimamia maslahi ya taifa kwanza, sio dini, sio kabila na sio maslahi binafsi au ya kikundi fulani. Kwa upande mmoja tunaanza kuwaangalia watu hao kwa kusikiliza HOJA zao. Hoja ya kwanza KIOJA cha kwanza tulichosikia ni kuwa JK ndiye rais anyefaa kugombea 2010 na wengine wakigombea watakufa ghalfa (This is probably a juju or majini thing, typical of slogan ya Nyani Ngabu, ndivyo tulivyo) sijui kigezo gani kilichotumika na kumuona kuwa yeye ni mgombea pekee. Na sijui ni inakuwaje years after years serikali inaacha tu mambo ya ajabu ajabu namna hii kuwekwa hata kwenye vyombo vya habari na kuingia kwenye akili za watu, au kwa nini serikali yetu inaacha ushirikina, juju na uchawi viwe msingi wa kufikiri kwa watanzania.

I wonder ni nani aliyekuja na hoja hii, na whether waandishi waliotufikishia waliuliza ni kigezo gani kitamfanya JK awe mgombea anayefaa zaidi, na ni nini kitawaua wagombea wengine. Na nini kitawafanya wapinga ufisadi waungane na mafisadi, na wote kuwa kwenye kundi moja linaloongozwa na mafisadi.

Lakini hapa hakuna la kumlaumu JK mwenyewe, maana yeye hajasema kitu public so far, tujaribu tu kuangalia hoja tunazotoa sisi watanzania kuhusu nani anatufaa na kwa nini tunadhani anatufaa. Tuone kama kweli sisi tuna akili au hatuna akili.

Tunajua tatizo liko wapi, tuangalie kama akili zetu zinatupeleka kwenye kutatua tatizo, au kuleta uswahiliswahili.
 
katika uchaguzi ujao Dr. Slaa ndiye mtu anayefaa zaidi kuwa mgombea toka kambi ya upinzani. Naamini Watanzania wote tutamuunga mkono na kuhakikisha anashinda.
 
- Wakuu uchaguzi mkuu wa taifa uko kwenye kona, Mzee Mandela aliwahi kusema kwamba kwenye ishu muhimu za taifa kama hizi kuwa kimyaa au kuwa neutral ni dalili za kuwa coward.

- Kwa wale tulio na influence ya namna moja au nyingine kwa taifa, ni vyema tukaweka wazi msimamo wetu kwa public kuhusu wagombea ambao tunaamini kwamba wanafaa katika kutusaidia taifa, nimekuwepo JF kwa muda mrefu sana sasa nikiwa na lengo moja tu, nalo ni siku moja kuliona taifa langu likiongozwa kwa kuheshimu sheria.

- Kwa hiyo leo nitaanza rasmi kuwataja wagombea ninaona wanafa kwa masilahi ya taifa letu, na sababu.

Respect.

FMEs!


CCM ndiyo itaongoza nchi hii for next 5 years, Hao viongozi wanapita kwenye chujio la NEC kwanza kama sikosei, NEC nayo imejaa uchafu mtupu sasa unategemea kupata viongozi bora?

Walio wasafi ndani ya NEC hawana nguvu yoyote, cha msingi hadi hapo CCM itakaposambaratika ndipo kutazaliwa demokrasia ya kweli inji hii, kwa sasa hesabu maumivu mengine hadi 2015.
 
Mimi naamini tatizo letu si ufisadi wala rushwa. Hizi ni "symptoms" tu.

Naamini kwamba tatizo letu ni watanzania tulio wengi mno (critical mass)tuna elimu ndogo sana. Uelewa wetu ni mdogo sana. Tunadanganyika kirahisi sana.

Kama kweli kundi la watu kumi (tunaowaita mafisadi papa) wanaweza wakaiba mabilioni ya fedha na watu karibia milioni 40 wakabaki wanaangalia tu wasijue lakufanya, mimi hapa naona tatizo liko kwa hao watu milioni 40. Wanastahili kilichowapata!!

Tatizo sio raisi wala baraza la mawaziri. Hawa wamewekwa tu hapo kufurahisha wale wanaodanganyika kirahisi, na ambao kwa bahati mbaya ndio wengi kupindukia.

Ili kuleta mabadiliko, inabidi watanzania tuelimishane kwa njia zote (mfano mzuri ni kupitia JF). Si tu kupashana nani kaiba nini, lakini tuelimishane jinsi ya kujiinua kiuchumi kwa kuongeza uzalishaji. Tuelimishane mbinu za kujinufaisha kwa kutumia akili, nguvu na rasilimali zetu wenyewe.

Tukishakua taifa la wananchi (critical mass) wenye elimu, uelewa na wazalishaji hapo ndipo walio wengi tunaweza tukaleta mabadiliko.

Ni kama jamii isiyo na uelewa inayosumbuliwa na maradhi. Kama hamna uelewa, polio na malaria zitawaangamiza huku wao wakitaftana mchawi, kuua ma-albino na vikongwe huku tatizo la magonjwa likiongezeka kwa kasi. Lakini wakigundua chanjo ya polio, vyandarua na dawa za malaria, haya magonjwa na maradhi yanayowasibu yanatoweka yenyewe.

Rushwa, ufisadi na uhalifu mwingine ni kama maradhi. Elimu na uelewa ndo chanjo yetu. Tukielimika, ufisadi na mambo mengine mabaya yatatokomea yenyewe. Utawala wa sheria na haki UTAKUJA WENYEWE. HAKUNA HAKI PASIPO NA MAARIFA!!

Bila elimu na uelewa yote ni bure. Tutaendelea tu kudanganywa.
 
Mimi naamini tatizo letu si ufisadi wala rushwa. Hizi ni "symptoms" tu.

Naamini kwamba tatizo letu ni watanzania tulio wengi mno (critical mass)tuna elimu ndogo sana. Uelewa wetu ni mdogo sana. Tunadanganyika kirahisi sana.

Kama kweli kundi la watu kumi (tunaowaita mafisadi papa) wanaweza wakaiba mabilioni ya fedha na watu karibia milioni 40 wakabaki wanaangalia tu wasijue lakufanya, mimi hapa naona tatizo liko kwa hao watu milioni 40. Wanastahili kilichowapata!!

Tatizo sio raisi wala baraza la mawaziri. Hawa wamewekwa tu hapo kufurahisha wale wanaodanganyika kirahisi, na ambao kwa bahati mbaya ndio wengi kupindukia.

Ili kuleta mabadiliko, inabidi watanzania tuelimishane kwa njia zote (mfano mzuri ni kupitia JF). Si tu kupashana nani kaiba nini, lakini tuelimishane jinsi ya kujiinua kiuchumi kwa kuongeza uzalishaji. Tuelimishane mbinu za kujinufaisha kwa kutumia akili, nguvu na rasilimali zetu wenyewe.

Tukishakua taifa la wananchi (critical mass) wenye elimu, uelewa na wazalishaji hapo ndipo walio wengi tunaweza tukaleta mabadiliko.

Ni kama jamii isiyo na uelewa inayosumbuliwa na maradhi. Kama hamna uelewa, polio na malaria zitawaangamiza huku wao wakitaftana mchawi, kuua ma-albino na vikongwe huku tatizo la magonjwa likiongezeka kwa kasi. Lakini wakigundua chanjo ya polio, vyandarua na dawa za malaria, haya magonjwa na maradhi yanayowasibu yanatoweka yenyewe.

Rushwa, ufisadi na uhalifu mwingine ni kama maradhi. Elimu na uelewa ndo chanjo yetu. Tukielimika, ufisadi na mambo mengine mabaya yatatokomea yenyewe. Utawala wa sheria na haki UTAKUJA WENYEWE. HAKUNA HAKI PASIPO NA MAARIFA!!

Bila elimu na uelewa yote ni bure. Tutaendelea tu kudanganywa.

- Sawa sawa mkuu tupo pamoja kaka hapo!

Respect.


FMEs!
 
- Wakuu uchaguzi mkuu wa taifa uko kwenye kona, Mzee Mandela aliwahi kusema kwamba kwenye ishu muhimu za taifa kama hizi kuwa kimyaa au kuwa neutral ni dalili za kuwa coward.

- Kwa wale tulio na influence ya namna moja au nyingine kwa taifa, ni vyema tukaweka wazi msimamo wetu kwa public kuhusu wagombea ambao tunaamini kwamba wanafaa katika kutusaidia taifa, nimekuwepo JF kwa muda mrefu sana sasa nikiwa na lengo moja tu, nalo ni siku moja kuliona taifa langu likiongozwa kwa kuheshimu sheria.

- Kwa hiyo leo nitaanza rasmi kuwataja wagombea ninaona wanafa kwa masilahi ya taifa letu, na sababu.

Respect.


FMEs!
RIP Tribute to Mwana JF Mwenzetu William Malecela Le Mutuz, Alikuwa Mtu wa Watu
P
 
Record ya JPM kuhusu vita ya ufisadi iko wazi, pia nadhani inaeleweka ametupiwa kwenye insignificant ministry ili kumpunguza kasi yake.

Uogawangu kuhusu huyu jamaa, ni too practical, anataka vitendo bila kuchelewa, asingeweza kuvumilia delayings tactic kwa kisingizio cha utawala wa sheria, hivyo ana risk ya kuwa dictator kama ambayo Mrema alivyo.
Najisoma na kujikumbusha if ya zamani, nafurahi, haya niliyasema 2009!.
RIP WJSM
P
 
Back
Top Bottom