Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Leo katika kipindi chake cha mapitio ya magazeti cha 06.50am asubuhi, kituo cha television cha ITV kinachomilikiwa na IPP Media kilifanya tukio ambalo sikulitegemea kwa kwa kituo hicho kinachojinadi ni cha makini.
Twajua kwa muda mrefu huwa hakipitii magazeti ya New Habari, lakini mengineyo yote huwa kinayapitia. Lakini leo asubuhi magazeti yote yaliyoandika habari za ukweli kuhusu tukio la jana la kudondoka jukwaani kwa JK hayakupitiwa. Magazeti yaliyopitiwa na kusomwa vichwa vyake vikuu vya habari vya mbele ni Nipashe, Habari Leo, Guardian, Sunday News, ambayo hayakuwa na habari ya tukio hilo kurasa za mbele.
ITV wanaficha nini? Kwa nini wanaficha ukweli? Mimi sillamikii sana kwa magazeti ya IPP kukosa kuandika habari za tukio hilo kurasa za mbele – lakini basi kituo hicho kingeruhusu watazamaji wapate habari za tukio kutoka kwenye magazeti ya wamiliki wengine.
Kwa upande mwingine nawapongeza Channel Ten katika kipindi chao cha mapitio ya magazeti leo kwa kuyapitia magazeti yote, pamoja na yale yaliyoandika habari za tukio kurasa za mbele. Magazeti haya ni Mwananchi, Majira, Tanzania Daima, Mtanzania na mengineyo.
Jirekebisheni ITV kwa kusema ukweli hasa katika kipindi hiki cha kampeni. Tuna wasiwasi mnaweza kufanya kama ya 1995 mlipoleta picha za mauaji ya Rwanda kutisha wananchi wasichague upinzani.
Twajua kwa muda mrefu huwa hakipitii magazeti ya New Habari, lakini mengineyo yote huwa kinayapitia. Lakini leo asubuhi magazeti yote yaliyoandika habari za ukweli kuhusu tukio la jana la kudondoka jukwaani kwa JK hayakupitiwa. Magazeti yaliyopitiwa na kusomwa vichwa vyake vikuu vya habari vya mbele ni Nipashe, Habari Leo, Guardian, Sunday News, ambayo hayakuwa na habari ya tukio hilo kurasa za mbele.
ITV wanaficha nini? Kwa nini wanaficha ukweli? Mimi sillamikii sana kwa magazeti ya IPP kukosa kuandika habari za tukio hilo kurasa za mbele – lakini basi kituo hicho kingeruhusu watazamaji wapate habari za tukio kutoka kwenye magazeti ya wamiliki wengine.
Kwa upande mwingine nawapongeza Channel Ten katika kipindi chao cha mapitio ya magazeti leo kwa kuyapitia magazeti yote, pamoja na yale yaliyoandika habari za tukio kurasa za mbele. Magazeti haya ni Mwananchi, Majira, Tanzania Daima, Mtanzania na mengineyo.
Jirekebisheni ITV kwa kusema ukweli hasa katika kipindi hiki cha kampeni. Tuna wasiwasi mnaweza kufanya kama ya 1995 mlipoleta picha za mauaji ya Rwanda kutisha wananchi wasichague upinzani.