Uchafu mwingine wa Nishati na Madini

kuanzia kesho naomba spika asisome ile sala ya kinafiki wakati anaanza bunge asubuhi
 
Mwisho hizo simu umeziweka za nini? Huko ni kwenda kinyume cha "right to privacy"!.

Hatuwezi kusita kufichua maovu kisa tunaingilia Privacy za watu. Kumbuka hata Zakia Meghji alivyokuwa anakataa kutoa taarifa za BoT kuhusu wizi wa EPA kwa kisingizio taarifa zinahusu Idara ya Usalama wa Taifa!

TUMBIRI (PhD, University of HULL - United Kingdom),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Mkuu Slobodan Milosovic, kwanza karibu jamvini, maana naona ndio kwanza umejiunga le. Pili asante kwa taarifa muhimu na nyeti kama hizi na mwisho hizo simu umeziweka za nini?!, huko ni kwenda kinyume cha "right to privacy"!.

Mkuu, Which Right to privacy??? Kwa hiyo waliokuwa wanaandika habari za uchunguzi kama Mwanahalisi huwa wanakosea?
 
Mkuu Pasco, privacy iko kwa maswala binafsi ya kina Masele. Hakuwezi kuwa na privacy kwenye dhahabu yetu. Haya ndiyo yalifanya kina Karamagi wanasaini mikataba mahotelini na wabunge wanaambiwa hizo ni siri za serikali hivyo hawaruhusiwi kuziona.
Mkuu Gagnija, JF as a reputable social media outlet, has an obligation to respect "the right to privacy" za watu, mobile number is among the privacy za watu, hivyo kuijua mobile number ya mtu, haikupi right ya kuiexpose hiyo number in public bila ridhaa ya mwenye number, this is a violation of "the right to privacy".

Najua modes hawawezi kufuatilia kila kitu, ila sisi wanachama watiifu wa jf, pale tunapoona tunakwenda over and above, tunasaidiana kushtuana ili turejee kwenye mstari.
 
Mbona Naibu Waziri wa Nishati na Madini ni Mhe. George Simbachawene.

Mkuu Wizara hii ya nishati na madini ina manaibu wawili, mmoja ni SIMBACHAWENE anaeshughulikia NIshati kwa maana ya Tanesco na mwingine ni Stephen Masele anaeshughulika na Madini tu...
 
Mkuu karibu JF kwa hii ID yako mpya.... Ivi watanzania hatujifunzi tu...??? Hwa jamaa wataacha lini huu wizi? Nakubaliana na Johnson Mbwambo hapa chini... Msome...

mbwambo.jpg


Tafakuri Jadidi

Baba fisadi, mtoto fisadi, mjukuu fisadi!

Johnson Mbwambo

Toleo la 253
8 Aug 2012

SASA ni dhahiri mwezi hauwezi kupita bila nchi yetu kutikiswa na skandali kubwa ya ufisadi. Unaweza kusema kila mwezi una aina yake ya skandali ya ufisadi.

Mwezi uliopita (kwa mfano) ilikuwa ni skandali ya mafisadi (wakiwemo viongozi wastaafu) waliojilimbikizia mabilioni ya shilingi katika benki za Uswisi.

Mwezi huu ni skandali ya ufisadi wa ununuzi wa mafuta iliyoikumba Tanesco, skandali ambayo pia inawahusu wabunge kadhaa wanaotuhumiwa kuhongwa fedha za rushwa na makampuni ya mafuta.

Sina hakika mwezi ujao ni skandali ya aina gani itaitikisa tena nchi yetu, lakini nina hakika kwamba itakuwepo tu; maana hii sasa inaonekana kuwa ndio staili ya maisha yetu tuliyojichagulia.

Sijui wenzangu mnaitafsiri vipi hali hii ya kusikitisha ya nchi yetu, lakini kwangu mimi hali hii inaashiria jambo moja kubwa; nalo ni kwamba tumeanza kuwa sugu katika masuala ya ufisadi. Na hii si ishara njema hata kidogo kwa nchi yetu.

Nasema tumeanza kujenga usugu kwa sababu skandali hizi za ufisadi hufuatana – moja baada ya nyingine, na hiyo maana yake ni kwamba kufichuliwa kwa skandali moja hakuwatii hofu mafisadi wengine kukamilisha (au kusuka) zao.

Na hali hii imeanza kuwa ni ya kukatisha tamaa kwa sababu wabunge (watunga sheria (zikiwemo za kupambana na ufisadi) sasa ndio vinara wa uovu huo.

Kwa maneno mengine, wabunge ambao ndio tegemeo la wananchi katika kuiwajibisha serikali ipambane vyema na ufisadi ndio sasa wamegeuka kuwa vinara wa ufisadi.

Tena wanaufanya ufisadi huo katika hali inayodhalilisha uwezo wa kufikiri wa wananchi; hususan wapiga kura wao. Wale wabunge ambao walionekana wakali bungeni wakiichachafya serikali kuhusu ufisadi huu na ule kumbe wenyewe ndio vinara wa ufisadi.

Wabunge hawa watatema cheche ndani ya bunge, lakini wakitoka nje ya bunge wanazifuata halmashauri za wilaya au mashirika ya umma (mfano Tanesco) au kampuni za mafuta au madini kuomba rushwa ili "watetee" hili na lile ndani ya bunge, na wasipopewa hutisha kuwa "watawawashia moto" ndani ya bunge!"

Kwa hiyo, naweza kusema ya kuwa sasa vita dhidi ya ufisadi katika Tanzania haina tena wapiganaji au majemadari wakuaminika. Wale tuliowadhania ni majemedari wa vita hiyo kumbe ilikuwa ni "danganya toto" tu.

Sasa imedhihirika kwamba, wakipiga kelele dhidi ya ufisadi si kwa sababu wanauchukia kweli kweli au si kwa sababu wao ni watu waadilifu; bali ni kwa sababu wanataka wasikike na waogopwe ili waweze kuzitisha halmashauri, mashirika ya umma, makampuni ya madini, makampuni ya mafuta, makampuni ya utalii nk. ili waweze kukatiwa pesa za rushwa!

Katika siku za karibuni, kwa mfano, tumesikia habari za mbunge kijana aliyedhaniwa ni mwadilifu na machachari akitumiwa kupoza skandali ya ufisadi katika Tanesco.

Aidha, tumesikia habari za wabunge kadhaa walioziendea halmashauri za wilaya na kuziomba rushwa! Mmoja tayari ana kesi mahakamani kwa kuomba rushwa ya Sh. milioni moja.

Wengi wetu bado tunazikumbuka habari za Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, aliyewakatia wabunge posho za rushwa ili waitetee wizara yake wakati wa mawasilisho ya bajeti!

Kwa ufupi, tumesikia kila aina ya ripoti za skandali za ufisadi zilizowahusu wabunge wetu. Na kama nilivyoeleza mwanzo, kufichuliwa kwa moja hakukuwatia hofu wabunge wengine kuendelea na zao!

Nje ya Bunge - yaani katika serikali, makampuni ya umma na binafsi, NGOs, sekta za madini, utalii nk, hali ndio mbaya zaidi. Na tena huko ndio kwenye rushwa kubwa kubwa.

Nisisitize tena kwamba vita hii dhidi ya ufisadi sasa haina wapiganaji wa kweli wala majemedari wa kweli. Kwa hakika, sasa naanza kupata shaka kama kweli vita hii ilipata kuwanao baada ya Mwalimu Nyerere na Edward Sokoine kututoka.

Hawa wa sasa waliojitokeza katika miaka ya karibuni na tukawaamini kuwa ni wapambanaji wa kweli wa vita hii, imedhihirika kuwa walichokuwa wakifanya ni "danganya toto" tu.

Chukulia mfano wa jemadari mkuu kabisa, Rais Jakaya Kikwete. Huyu hatujamsikia kwa muda mrefu akifungua kinywa chake kukemea ufisadi huu mkubwa au hata kuchukua hatua zozote kubwa (maamuzi magumu) kupambana na hawa tunaowaita mafisadi papa.

Hatukumsikia Kikwete akifungua kinywa chake hata pale ripoti ya benki kuu ya Uswisi ilipoitaja Tanzania kuwa ni moja ya nchi ambayo viongozi wake wameficha mabilioni ya fedha kwenye akaunti za benki za nchi hiyo.

Kwa hiyo, ninaposema ya kuwa vita hii dhidi ya ufisadi katika Tanzania haina wapiganaji wa kweli wala majemedari wa kweli, maana yangu ni hiyo.

Kwa upande mwingine, hata Takukuru nayo imeshindwa kuushawishi umma kama inapigana kweli kweli vita hii. Masra nyingi imeisdhia kupambana na vijidagaa wa ufisadi na si mafisadi papa ambao ndio kansa inayolitafuna taifa hili.

Miezi kadhaa iliyopita niliandika katika safu hii kwamba Takukuru haina uwezo wa kufuatilia na kuwafikisha mahakamani mafisadi hao walioficha mabilioni ya fedha katika benki hizo za Uswisi. Nilishauri kitafutwe chombo cha nje (mathalan Interpol) kutufanyia kazi hiyo.
Lakini bosi mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hoseah, hakufurahishwa na kauli yangu hiyo, na katika mahojiano na televisheni moja alinishutumu kwamba sielewi vyema utendaji wa asasi hiyo na kunitaka nifike ofisini kwake ‘anielemishe'.

Katika mahojiano hayo, Dk. Hoseah aliwapa matumaini Watanzania kwamba asasi yake itahitimisha vyema suala hilo la mapesa yaliyofichwa Uswisi. Hata hivyo, mpaka sasa miezi miwili imeshakatika na bado hakuna ripoti yoyote ya maendeleo ya suala hilo ambayo imetolewa kwa umma na Takukuru!

Na ndio maana msimamo wangu ni ule ule kwamba asasi yetu hiyo haina ubavu wa kulishughulikia suala hilo zito la ufisadi wa kimataifa na kufikia mwisho mwema!

Kama asasi hiyo ingekuwa na uwezo huo, pengine ingekuwa tayari imefikia mwisho mwema katika suala lile la kashfa ya ufisadi wa rada ambalo limefikia hata hatua ya kuandikiwa kitabu na mchunguzi mmoja wa kimataifa!

Nionavyo mimi, Takukuru husikika zaidi pale tu skandali kubwa zinapoibuliwa na wengine na si yenyewe kuwa ya kwanza kuziibua skandali hizo.

Kwa mfano, ilipoibuliwa skandali ile ya Jairo, Takukuru iliibuka na kusema kuwa itachunguza. Lakini pia mawaziri kadhaa walipong'olewa uwaziri baada ya wabunge kuwatuhumu kuhusika na rushwa, ndipo Takukuru ilipotoa tamko kwamba itawahoji kwa lengo la kuwafikisha mahakamani wale ambao ushahidi dhidi yao ni mzito. Mpaka sasa hakuna aliyefikishwa mahakamani.

Na hata majuzi ilipoibuliwa hii skandali ya ufisadi ya ununuzi wa mafuta katika Tanesco ndipo tumeisikia Takukuru ikitamka kuwa itachunguza suala hili kwa kuwahoji watuhumiwa.

Kwa mwenendo huo, mtu unashawishika kujiuliza kuwa Takukuru inakuwa wapi muda wote huo na ishindwe kuwa ya kwanza kuibua skandali hizo? Kwa nini inajitokeza tu kuchunguza pale skandali hizo zinapoibuliwa na wengine? Na mbona pia umma hauoni mwisho mwema au matokeo mema ya uchunguzi wao huo?

Si nia yangu kuilaumu Takukuru. Kwa hakika, kuilaumu Takukuru kwa utendaji usioridhisha katika nchi ambayo imeota usugu wa ufisadi hadi vyombo vya juu vya maamuzi, ni kutoitendea haki.

Tumeukumbatia utamaduni wa ufisadi kwenye kona zetu zote za maisha, na tumeikumbatia tabia ya kutowashitaki mafisadi (impunity culture) kiasi kwamba tatizo hili sasa limekuwa dubwana kubwa linaloelekea kutushinda nguvu.

Jamii imeoza kuanzia ngazi ya familia: Baba fisadi, mtoto fisadi na mjukuu fisadi! Hakika, baba fisadi hatamuuliza kijana wake amepata wapi fedha za kununua gari la kifahari aina ya Hammer.

Na mtoto naye mwenye Hammer hatamuuliza mtoto wake amepata wapi fedha za kununua Range Rover new model au Vogue katika miaka yake michache tu kazini!

Vivyo hivyo mtawala aliyeingia madarakani kwa njia za ufisadi hawezi kukasirika akisikia waziri wake anashiriki vitendo vya kifisadi. Na wala kope zake haziwezi kupepesa akisikia wabunge kutoka chama chake wanapita huku na kule kuomba rushwa kwenye makampouni ya mafuta, madini nk!

Ndio maana ufisadi umekita Tanzania. Hakuna aliye msafi wa kumkemea mwenzake. Na tusipozinduka, ufisadi ndio utakuwa urithi wetu kwa vizazi vijavyo; maana kibaya kamwe hakizai chema.

Katika injili ya Luka Mtakatifu (6:43-44) imeandikwa hivi: "Mti mwema huzaa matunda mema, na mti mbaya huzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mema."

Ndio maana siku zote ninasema kuwa taifa hili halitakuwa tena na waadilifu kama tutarithishana hulka hizi za kifisadi kuanzia kwa baba, mwana, mjukuu hadi kwa kitukuu. Na hayo ndio maangamizi tunayoyaandaa kwa jamii ya Watanzania.

Nihitimishe safu yangu kwa kusema hivi: Kwa mambo yanavyokwenda hivi sasa, kila mwezi utakuja na skandali zake kubwa za ufisadi lakini kombe litafunikwa na mwanaharamu atapita, na watu wataendelea kunywa bia zao bila wasiwasi; huku wakisubiri tena mwezi ujao……wakisubirii skandali nyingine tena iibuliwe ili nayo izimwe kwa staili ile ile ya kisanii ya kuunda tume nk!

Ndugu zangu, nyumba yetu (Tanzania) ni chafu, na inahitaji kufagiliwa. Sina hakika kama mchafuzi (CCM na serikali yake) ndiye huyo huyo anayeweza kuifagia na ikawa safi kweli kweli!
 
naomba ufafanuzi hapa '' LAKINI WALISHINDWA KUTOKANA NA KUONA AIBU.''

hiki ni kipande cha sentensi toka katika thread hiyo hapo juu
 
Sorry mkuu, natumia simu hivyo nimeshindwa kuweka alama. Umesema watakwenda jtatu tarehe 13 yaani kesho.

Kuna mahali ukasema walishindwa kutokana na aibu. Walishindwa kwenda au kupokea rushwa?
 
Mkuu, Which Right to privacy??? Kwa hiyo waliokuwa wanaandika habari za uchunguzi kama Mwanahalisi huwa wanakosea?
Mkuu Manyi, tasnia ya habari, nayo inayo miongozo na miiko yake iitwayo "media ethics". Miongoni mwa ethics ni hili la "the right to privacy".

Kukweli, kwenye ile story ya "Mwanahalisi" kuhusu kutekwa kwa Ulimboka, Mwanahalisi walikosea kwa kukiuka maadili ya " the right to privacy"!. Japo kwa upande mmoja, gazeti la Mwanahalisi, wanastahili pongezi kwa kuandika "investigative story", lakini wangeweza kuiandika investigative piece yao na wakafikisha ujumbe ule vizuri zaidi bila kukiuka "the right to privacy" kwa kuanika "private conversation" na "private numbers" kwenye public!.

Tanzania tunazo sheria nyingi za ajabu ambazo bado ziko kwenye vitabu vya sheria lakini hazitumiki, siku zikitumika ipasavyo, watu watapiga kelele, eti wanaonewa!.

Mimi naamini kabisa, sisi ambao angalau tunaamini katika "freedom of expression" ni wajibu wetu kuisaidia jf kumaitain uhuru wa kujieleza kwa members watu lakini hakuna uhuru usio na mipaka, uhuru wa mtu mmoja unaishia pale anapoingilia uhuru wa mtu mwingine!.
 
Hatuwezi kusita kufichua maovu kisa tunaingilia Privacy za watu. Kumbuka hata Zakia Meghji alivyokuwa anakataa kutoa taarifa za BoT kuhusu wizi wa EPA kwa kisingizio taarifa zinahusu Idara ya Usalama wa Taifa!

TUMBIRI (PhD, University of HULL - United Kingdom),

tumbiri@jamiiforums.com

Mkuu Tumbiri, unaweza kufichua maovu, bila kukiuka "the right to privacy".
 
Mkuu Gagnija, JF as a reputable social media outlet, has an obligation to respect "the right to privacy" za watu, mobile number is among the privacy za watu, hivyo kuijua mobile number ya mtu, haikupi right ya kuiexpose hiyo number in public bila ridhaa ya mwenye number, this is a violation of "the right to privacy".

Najua modes hawawezi kufuatilia kila kitu, ila sisi wanachama watiifu wa jf, pale tunapoona tunakwenda over and above, tunasaidiana kushtuana ili turejee kwenye mstari.
Tuache unafiki kwani katibu mkuu wa nishati na madini alipovunja sheria ya manunuzi ya umma alipongezwa kwa kigezo cha kusaidia taifa na huyu kama kafichua ufisadi kwa lengo la kusaidia taifa kwanini asiungwe mkono?
 
Mkuu Tumbiri, unaweza kufichua maovu, bila kukiuka "the right to privacy".

Mkuu
Pasco hivi nikitaja namba yako ya simu kwamba ni 0713XXXXXX na 0754YYYYYY hapa JF ntakuwa nimekudhuru nini in terms of Privacy? Hivi unajua kwamba kipindi kile tuna TTCL kama kampuni pekee ya simu nchini namba za watu zilikuwa zinachapishwa kwenye kile kitabu kikubwa maarufu kama 'Yellow page'? Na unakumbuka kile kitabu kilikuwa open kwa mtu yeyote? Kwa hiyo unataka kusema kwamba TTCL nayo ilikuwa inaingilia privacy za watu na mashirika mbalimbali?

Sasa mtoa taarifa kaandika namba za simu za huyo Waziri, Mkuu wa Wilaya na Afisa Usalama wa Wilaya kuna ubaya gani? Namba za simu siyo Privacy. Privacy ni Information ndani ya simu zinazohusu mapenzi yako na Mkeo, Hawala, Familia, Marafiki nk. Kama unatumia simu yako kuhujumu Taifa information hizo haziwezi kuwa Privacy. Kufanya hivyo ni kuhalalisha wizi usifichuliwe kwa sababu umehusisha simu ya mtu!

TUMBIRI (PhD, University of HULL - United Kingdom),

tumbiri@jamiiforums.com
 
hivii how development can to be brought brother when the people to whom we have entrasted power are corrupt? chukua hatuaaaa

Kukusaidia kidogo ungeandika hivi, HIVII HOW CAN DEVELOPMENT BE ACHIEVED BROTHER WHEN THE PEOPLE WHOM WE HAVE ENTRUSTED POWER ARE CORRRUPT?
 
Kama ni kweli basi hawa watu wa CCM ni wagonjwa hata hawawezi kusoma alama za majira? Ama kweli sikio la kufa halisikii dawa. Nawapongeza walioweza kunasa jambo hili. Ombi liletwe hadharani mapema kabla halijapoa. Wanaosema ni violation of privacy wana ufahamu kidogo kwa sababu hili ni jambo linalohusu uhujumu uchumi wa nchi siyo yeye na familia yake au marafiki.
 
Mkuu Pasco hivi nikitaja namba yako ya simu kwamba ni 0713XXXXXX na 0754YYYYYY hapa JF ntakuwa nimekudhuru nini in terms of Privacy? Hivi unajua kwamba kipindi kile tuna TTCL kama kampuni pekee ya simu nchini namba za watu zilikuwa zinachapishwa kwenye kile kitabu kikubwa maarufu kama 'Yellow page'? Na unakumbuka kile kitabu kilikuwa open kwa mtu yeyote? Kwa hiyo unataka kusema kwamba TTCL nayo ilikuwa inaingilia privacy za watu na mashirika mbalimbali?Sasa mtoa taarifa kaandika namba za simu za huyo Waziri, Mkuu wa Wilaya na Afisa Usalama wa Wilaya kuna ubaya gani? Namba za simu siyo Privacy. Privacy ni Information ndani ya simu zinazohusu mapenzi yako na Mkeo, Hawala, Familia, Marafiki nk. Kama unatumia simu yako kuhujumu Taifa information hizo haziwezi kuwa Privacy. Kufanya hivyo ni kuhalalisha wizi usifichuliwe kwa sababu umehusisha simu ya mtu! TUMBIRI (PhD, University of HULL - United Kingdom), tumbiri@jamiiforums.com
Mkuu Tumbiri, mwanzo nilipokuona unasomea Ph.D hapo Hull nikadhani kila Ph.D in kusomea udaktari wa falsafa, nikidhania kila falsafa inahusisha kutumia ubongo kufikiri, ndio maana kule nyuma niliwahi kukuuliza unasomea Ph.D ya nini?, uliponijibu nilielewa!.Vitu vingine vinahitaji just a comon sense reasoning, wala huhitaji hata kuwa msomi kuvibaini!. Fixed telephone lines, box office number, hse number, office number, street number, ni public domain information ambazo ziko access to public, mobile number ni personal, wengine wanaita "private number" hutolewa kwa idhini ya mwenye number!.Mfano mimi nazijua mobile za JK, Pinda, Othman, Mwamunyage, Mwema etc, by nature ya kazi yangu as a journalist. Hata ukiniuliza kuwa unaomba mobile ya JK, siwezi kukupa, sasa sana labda nimwambie fulani anashida naye na anaomba mobile number yake, only at his discretion, ndipo nitakupa!.Ukienda vituo vyote vya polisi pale mapokezi, utakuta official mobile number za wakuu wote, kuanzia IGP, RPC, OCD etc zimewekwa public, hizo ni public domain mobile, lakini wote hao wanazo private mobile number zao ambao hazipo pale ila watu wanazo, hizo ndizo hizo "right to privacy".Kwenye uandishi wa habari, kuna kitu kinaitwa "the confidentiality of the source", ukinipa taarifa nyeti za siri, mimi kama mwandishi ninawajibika kuhifadhi identity yako na hata ikibidi mimi kushikitakiwa kwa "possession of confidential information", nitakwenda jela bila kukutaja!. Baadhi ya waandishi wa gazeti la Mwanahalisi, wanaandikia masifa zaidi kuliko kufuata weledi, vivyo hivyo baadhi yetu hutumia masifa kuposti humu "private information za watu" kwa masifa tuu bila kufuata "the right the privacy", for jf survival a sustainibility for the future, this must stop sooner or later, vinginevyo jf tutageuka kijiwe cha kahawa kwa hoja za furahisha genge!.
 
Mkuu Gagnija, JF as a reputable social media outlet, has an obligation to respect "the right to privacy" za watu, mobile number is among the privacy za watu, hivyo kuijua mobile number ya mtu, haikupi right ya kuiexpose hiyo number in public bila ridhaa ya mwenye number, this is a violation of "the right to privacy".

Najua modes hawawezi kufuatilia kila kitu, ila sisi wanachama watiifu wa jf, pale tunapoona tunakwenda over and above, tunasaidiana kushtuana ili turejee kwenye mstari.
Impliedly, you applaud the govt's move to ban Mawanahalisi. Do you?
 
Back
Top Bottom