Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 742
- 479
Balozi wa Tanzania Nchini Ufaransa Mhe. Ali Jabir Mwadini amekutana na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Kimataifa la Nishati (International Energy Agency - IEA) Bw. Faith Birol, tarehe 10 Januari, 2024
Viongozi hao wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na shirika hilo (IEA) katika nyanja mbalimbali za sekta ya nishati hususan uendelezaji wa nishati salama na endelevu.
Mhe. Mwadini na Bw. Birol wamekubaliana kuendeleza jitihada za kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia (clean cooking energy) suala ambalo bado ni changamoto kwa nchi nyingi za Afrika.
Viongozi hao wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na shirika hilo (IEA) katika nyanja mbalimbali za sekta ya nishati hususan uendelezaji wa nishati salama na endelevu.
Mhe. Mwadini na Bw. Birol wamekubaliana kuendeleza jitihada za kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia (clean cooking energy) suala ambalo bado ni changamoto kwa nchi nyingi za Afrika.