Ubungo bus terminal dump ya uchafu, jiji wapi?

kama ni uchafu basi jiji la Dar limekithiri. Jamani watanzania tubadilike, hadi tuchapwe viboko jamani?

Mi nadhani kuongelea tu kwenye haya majukwaa tunakosea, inabidi kuanzisha kampeni nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu! vipeperushi vya kutosha! kuelimisha watu kuweka maeneo yetu safi. Lakini hii tabia ya msimu ya kutumia mamilion ya TZS kwa ajili ya wiki ya usafi wa majiji, ni kuibiana wenyewe. Inabidi kwenye vituo vya daladala, sokoni nk watu waelimishweharafu baada ya muda kamata kamata wanaozalisha taka taka. Mbona watakoma wenyewe!!
 
Nikitilia maani uwiano wa idadi ya watu wanaopita hapo kwa nikilinganisha na sehemu nyingine; mbona hapo pana uafadhali!!
Mara ya mwisho nimecheck kama wiki tatu hivi, vyoo vilikuwa na maji na viko katika kiwango cha kutumika kwa mtu aliyebanwa!!! Kumbuka kuna pahala penye mikusanyiko nimefika, yaani hata kama haja imekubana, unconsciously unajikuta umepata ahueni baada ya kuona mazingira yenye kinyaa chakupindukia pahala pa kujisaidia.

Wizi wa vitu pia umepungua, maana hawaruhusu tena wapokeaji kuingia ndani ya uzio kiurahisi kama ilivyokuwa mwanzo. Mabasi pia yanaondoka on time kuanza safari zake.

Uchafu kama unavyoonekana hapo kwenye picha ni matokeo ya hulka za wengi wetu. Ndivyo tulivyo; haswa Dar na 'umjini-umjini' kama sifa'!!! Inaudhi sana na ni kero kubwa.

Kaka naona unatetea kwa Nguvu zoote; pamoja na hulka za ajabu za Watanzania ambazo si suala la kubishia lakni si unaona pipa limejaa!!!.....unategemea watu wafanyeje?..na huo uchafu ulioko chini ni zaidi ya pipa mbili, hali inayoashiria kuwa hakuna umakini katika kufuatilia usafi wa mazingira stendi hapo, watu wakishafagia asubuhi wanaona kazi imeisha!
 
Kaka naona unatetea kwa Nguvu zoote; pamoja na hulka za ajabu za Watanzania ambazo si suala la kubishia lakni si unaona pipa limejaa!!!.....unategemea watu wafanyeje?..na huo uchafu ulioko chini ni zaidi ya pipa mbili, hali inayoashiria kuwa hakuna umakini katika kufuatilia usafi wa mazingira stendi hapo, watu wakishafagia asubuhi wanaona kazi imeisha!


Ukiona hivyo, watu walio katika payroll ya hiyo kazi wamewekwa kwa kujuana au wanajilipa wenyewe au hiyo kazi inawafanya wapate favour flani hivi. Kama wangekuwa serious, waajiri watu wawe wanareport asubuhi ofisini na kusambaa kwenye vituo vyao!! hata kama ni mida ya asubuhi saa 11 hadi saa 6 mchana, baadae tena saa 10 jioni hadi saa 3 usiku watu wanakuwa wanalipwa kwa masaa!!.

Tukifanya hivyo, huku tukiwaelimisha watu kuacha tabia ya kutupa taka hovyo, kukojoa hovyo na vitu kama hivyo! baada ya muda watu watalazimika kuweka taka ndani ya mikoba hadi watakapoona sehemu rasmi ya kutupa taka. Kingine, hizo taka zinawenyewe, kwa hiyo hao wanaozileta wawe responsible kuhakikisha hazitupwi hovyo ikiwa ni pamoja na kuwekwa maeneo maalumu ya kutupa taka taka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom