AMINATA 9
JF-Expert Member
- Aug 6, 2011
- 2,120
- 641
ma dear u made ma day nimecheka mpaka basi mana mm mbado kuona hayo mambo jamani wacha nikajionee na mm mwezi wa kwanza kwa macho yangu...........kama kweli ilo eneo ni ubungo ama lah! na mengineyo mengiiiiiiiii.................nitazururajeeeeeeeeeeeeWala hujakosea mkuu. Mwaka jana niilipokua Dar desemba nilishangaa hata nikawa najuta kuwasili Bongo mchana kweupeee!!
Mchizi nilikua niko juu ya daladala trying to get the home feeling na amini usiamini kulikua na jamaa kasimama barabarani akikojoa mtaroni laivu!!!...Mwenzio mbona nikamaka kwa mshangao na abiria aliyekua amekaa ubavu wa pili akaniuliza "hivi wewe ni mgeni hapa mjini?" namii nikamwambia ndivyo na ndo nimelandi kutoka Marekani. Jamaa akacheka kisha akanijibu "karibu nyumbani, utazoea tu". Nilishangaa na nikakataa kauli yake eti "nitazoea'....there is no way in hell nitaozea kumwona mtu mzima hoyvoo, dudu nje akimwaga jojo kadamnasi mitaa ya Sinza.
Kisha kuanzia mitaa ya Mikocheni hadi Kawe ndo hapafai kabisa maana ni arufu mtindo mmoja!!! Maji taka hayazolewi na hata wakifanya kuzoa ni upuzi mtupu. Jamaa wanatoa uchafu ndani ya mtaro na kuuweka right at the top. In simple common sense, when it rains wont all this trash go right back into the drains jamani!!!? Nilipohoji nikaambiwa jama wanafanya hivyo maksudi ndo waweza kuhifadhi kibarua for the next day...Gaaadem!...Yaani Bongo kivyakevyake aisee. Kisha maeneo yenyewe nd'o barabara inayopitiwa na matasha na nikahooji tena kwani hawaoni hali ilivyo hususan kukinyesha. Nikaambiwa ukilinganisha na swala la kwamba jamaa wanaendesha mashangingi fuli-kipupwe, kwani wanaipata hio harufu?...najua ushapata jibu hapo!
Kisha ukiingia mjini wakati mambo ya umeme yanaleta kasheshe utajuta!...Kelele ya majenereta ni kama kuzimu! Yaani waliohujumu wananchi wa Tanzania kwa skendo za ishu za umeme hawakuwatenedea wananchi haki...but then again, who cares.
Kisha hapo Ubungo nitawaachia wenyewe wajadli. Kama Nyani alivyosema hapo juu watu wanaosindikiza abiria wanatozwa hela lakini
hujui hela inaenda wapi au ni ya nini. There is no official communication for that matter. Kisha kila mtu ni mwizi/tapeli hususan kipindi cha krismasi na shamrashamra za New Year. Utauziwa tikiti na jamaa kisha mkishamalizana na umekaa kwenye nafasi yako, anatokea konda mwengine anakudai hela zaidi. Ukijaribu kumtafuta aliyekukapa tikiti humuoni. Mwenzenu niligoma kushuka basi la Tanga kwa upuzi huo. Jamaa ilibidi nimmwagie kimombo na kumsuta mbaya sana. Tatizo langu lilkua usumbufu tu wa hawa matapeli. At the end of the whole saga tukawa washkaji mpaka kubadili namba za simu na niikapata kupiga tripu zengine mbili na jamaa hadi Mombasa na kurudi Dar.
Bongo tambarare wakuu...akili mukichwa!