Ukisikia Bunge halina mvuto ni Bunge hili lililosheni wabunge wengi wa CCM, wabunge wa upinzani kiduchu Sana, wabunge hewa kama wanavyojulikana covid-19.
Mvuto umekosekana hata kama Bunge ni live Wananchi hawafuatilii mijadala Bunge kama ilivyokuwa enzi Samwel Sitta au Anna Makinda.
Wabunge wengi hawajui kujenga hoja na kusimamia, wabunge wengi hawajui kuuliza maswali, hii inapelekea Spika wa Bunge kutoa maelezo kwa wabunge namna ya kujenga hoja, na namna ya Kujadili hata namna ya kuuliza maswali.
Inatokea siku ambayo Waziri mkuu huulizwa maswali hakuna hata swali anaulizwa.
Wabunge wa upinzani licha ya uchache wao, wamemezwa na CCM, hawajielewi kwa kujenga hoja na kuzisimamia, licha ya changamoto kibao taifa linakabiliwa.
Nakumbuka enzi za akina Masumbuko Lamwai, licha ya uchache wao, walisikika na Wananchi waliwafuatilia.
Wabunge hewa a. k. a Covid-19, wapo vizuri na wanajielewa, lakini kwa sababu ni hewa wanaogopa kuleta mijadala mizito, maana watapigwa vijembe kuwa ni wabunge wa Chama gani.
Uchaguzi wa 2020 umeleta dhahama kwenye taifa hili, si kwa wabunge tu hata mawazir hawajui kujibu maswali.
Mimi nashauri wabunge wanatakiwa kutafuta maarifa kwa kusoma sana na kufuatilia mambo mbalimbali na kuweka kumbukumbu Sawa, wasipende kusikiliza tu na kuchukua posho.
Nchi hii ina changamoto nyingi mno ambazo haziibuliwi na kuwasilishwa Serikalini.
Mvuto umekosekana hata kama Bunge ni live Wananchi hawafuatilii mijadala Bunge kama ilivyokuwa enzi Samwel Sitta au Anna Makinda.
Wabunge wengi hawajui kujenga hoja na kusimamia, wabunge wengi hawajui kuuliza maswali, hii inapelekea Spika wa Bunge kutoa maelezo kwa wabunge namna ya kujenga hoja, na namna ya Kujadili hata namna ya kuuliza maswali.
Inatokea siku ambayo Waziri mkuu huulizwa maswali hakuna hata swali anaulizwa.
Wabunge wa upinzani licha ya uchache wao, wamemezwa na CCM, hawajielewi kwa kujenga hoja na kuzisimamia, licha ya changamoto kibao taifa linakabiliwa.
Nakumbuka enzi za akina Masumbuko Lamwai, licha ya uchache wao, walisikika na Wananchi waliwafuatilia.
Wabunge hewa a. k. a Covid-19, wapo vizuri na wanajielewa, lakini kwa sababu ni hewa wanaogopa kuleta mijadala mizito, maana watapigwa vijembe kuwa ni wabunge wa Chama gani.
Uchaguzi wa 2020 umeleta dhahama kwenye taifa hili, si kwa wabunge tu hata mawazir hawajui kujibu maswali.
Mimi nashauri wabunge wanatakiwa kutafuta maarifa kwa kusoma sana na kufuatilia mambo mbalimbali na kuweka kumbukumbu Sawa, wasipende kusikiliza tu na kuchukua posho.
Nchi hii ina changamoto nyingi mno ambazo haziibuliwi na kuwasilishwa Serikalini.