UBORA WA UDSM.
Pamekuwa na msuguano mkali kuhusu ni nini hasa kinapelekea Udsm kuwa chuo bora hapa nchini na Afrika kwa ujumla.
Aidha wapo mahasimu wanaokibeza kwa kejeli na vijembe visivyo na kichwa wala miguu. Kutokana na haki ya kutoa maono basi ni wazi hawakosei kwani hutekeleza haki yao ya kutoa maoni ambayo ipo kikatiba.
Mimi ni Mhitimu wa chuo hicho bora. Ninajivunia kusomea chuo hiko. Nimeshiba kile nilichokusudia kukipata. Ninaouwezo wa pambano lolote kulingana na taaluma yangu.
Yafuatayo ni moja ya mambo yanayofanya Udsm kiwe chip Bora nchini kama si Afrika;
1. Mchakato wa udahili na wadahiliwa.
Udsm ndio chuo pekee kinachodahili wanafunzi wenye ufaulu mkubwa ukilinganisha na vyuo vingine.
60%= wanadivisheni one.
25%= divisheni two.
15%= divisheni three.
Utaona ni kwanamna gani Udsm ilivyobora kwa upande wa Input( wadahiliwa).
2. Uwepo wa Maprofesa na madokta wakutosha.
Udsm kina Ghala la maprofesa na madokta wakutosha. Ndio chuo pekee Tanzania chenye maprofesa wakutosha ukilinganisha na Vyuo vingine. Hata barani Afrika ni miongoni mwa vyuo vyenye maprofesa wengi wakutosha.
3. Miundombinu
Miundombinu kama Maktaba kubwa, Usafiri kwa wanafunzi, Hostel kwa sasa changamoto imepungua kama si kuisha, Viwanja vya michezo na burudani, vimbweta vya kusomea, miundombinu ya wa maji, Kafteria n.k.
Miundombinu hii hukifanya Chuo hiki kiendelee kuwa bora japokuwa kinakumbwa na uchakavu wa baadhi ya miundombinu kama choo na baadhi ya hostel kama hall 4&5.
4. Uwepo wa miradi Miradi.
Udsm kina miradi kadhaa ambayo imekuwa na manufaa kwa chuo na jamii kwa ujumla.
Baadhi ya Miradi ni pamoja na Uwepo Wa Shuttle zinazosafirisha wanafunzi kutoka Main Campus mpaka mabibo.
Uwepo wa Mlimani Tv ambayo inatoa huduma ya habari, Matangazo ya biashara na huduma zingine. Ndio chuo pekee chenye Channel ya TV.
Pia mradi wa Mlimani City Mall inayoendeshwa na kamapuni ya Nakumati. Mlimani city imeufanya Jiji la Dar es salaam kuwa bora na maarufu.
Bila shaka mtu ambaye hajafika Mlimani City atakuwa bado hajaonja utamu wa Dar es salaam.
5. Hali ya Hewa na Mazingira yake
Hali ya hewa ya Udsm ni yakuridhisha. Udsm imezungukwa na miti kila pahala, hivyo vivuli kila mahali jambo linalofanya wanafunzi wafurahie mazingira. Pia kuna Viumbe kama tumbili ambao wanaongeza upekee wa chuo hiki.
6. Uwepo wa Wahitimu Mahiri.
Mbali na Ukongwe wa Chuo hiki na umahiri wake wa Maprofesa na Wahitimu mahiri kama Tundu Antipus Lisu, Zito zuberi Kabwe, Jakaya Mrisho Kikwete, John pombe Magufuli, Halima Mdee n.k.
Kwa kifupi Udsm bado kipo makini na ubora wa kutosha japokuwa kina changamoto zake.