Uber yasitisha huduma zake Tanzania, yazitaja nauli elekezi Latra kama sababu. Itarejea kanuni zikibadilishwa

bro mimi ni dereva wa bolt hyo bei unayosema hapo ya bolt tujiulize wote 10000 hyo bolt wanakata 23.5%kama comision yao dereva anabaki na shilingi ngapi?? bolt wanaumiza sana madereva kwa kigezo cha kumjali mteja kitu ambacho sio sahihi, Latra wametoa bei elekezi na wamewaambia comision yao isizidi 15% nauli za mchana na usiku zitofautioane. na hapo hii bei elekezi LATRA walitoa kabla hata ya mafuta kupanda kama yalivyo sasa. wao wanataka waendelee na bei za zamani na commisiom za zamani dereva na mwenye chombo atapata faida gani??

Kwahiyo Mwisho wa Siku Manataka Kumuumiza Abiria.Abiria ndio alipe Mzigo wote
 
Kwahiyo Mwisho wa Siku Manataka Kumuumiza Abiria.Abiria ndio alipe Mzigo wote
Sasa serikali haitaki kubeba mzigo, mzigo huu unatwishwa mfanyabiashara, ambaye pekee yake hawezi! Serikali ilipaswa kugawana mzigo na wafanyabiashara hawa! Siyo kuwatwisha kichwani zigo la misumari ndani ya kiroba! Wajitafakari hapo hakuna mchawi wala katiba mbovu!
 
Wakuu,

Usiku huu Uber wametuma ujumbe unaosomeka hivi:
👇🏾

Huduma ambayo ilianza kama wazo tu — la kutumia simu yako kupata usafiri ndani ya dakika chache— Mfumo wa Uber umeenea duniani kote na zaidi ya safari milioni 15 hufanyika kila siku kupitia kwenye mfumo huu. Imekuwa ni heshima kubwa kupata nafasi ya kusaidia watu kupata usafiri duniani wanapofanya shughuli zao na kutangamana na watu wengine.

Lakini, maandalizi ni sehemu muhimu katika kufikia malengo ya siku za usoni.
Siku zote, lengo letu ni kuwa mshirika muhimu katika miji mbalimbali kwa kutoa usafiri wenye ufanisi, kutengeneza fursa za kiuchumi zinazowapa madereva uhuru wa kujiingizia kipato kwa muda wanaotaka wao na kuchangia katika mapato ya serikali. Na tumelisimamia lengo hili tangu tulipofungua milango yetu katika jiji la Dar es Salaam mwaka 2016.

Sera za usimamizi zinapaswa kuwa chachu wala sio kikwazo cha ubunifu

Tumefanya uamuzi mgumu wa kusitisha huduma zetu nchini Tanzania kuanzia Alhamisi ya Tarehe 14 Aprili 2022. Nauli elekezi iliyowekwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imesababisha changamoto kubwa kwa mifumo kama Uber kuendelea kutoa huduma kwa wateja wetu. Inakua ngumu kwetu kuendelea kutoa huduma. Hatuta weza kutoa huduma mpaka pale mazingira yatakapo kua rafiki kwa sisi kuendelea kutoa huduma.

Kipaumbele Chetu: kuwasaidia Madereva Watanzania
Uamuzi huu umekuja baada ya mamlaka kuweka kanuni ambazo ni changamoto kubwa kwa mifumo kama Uber kuendesha biashara yake. Tutafanya kazi kwa karibu na madereva kwenye mpito huu.

Tuweke Wazi: Tungependa sana kuendelea kutoa huduma zetu nchini Tanzania

Nchi ya Tanzania kupitia Dira ya Maendeleo ya 2025 imedhamiria kujenga uchumi imara, anuwai, himilivu na shindani ambao unaendana na mabadiliko ya masoko na kiteknolojia kikanda na kimataifa. Tulitegemea kwamba hii ingejumuisha kujenga mazingira wezeshi ili biashara ya ndani na kimataifa inawiri katika njia nzuri na yenye usawa, lakini kwa bahati mbaya, hali ni kinyume na matarajio.

Tutarudi kuzindua huduma zetu mara tu kutakapokuwa na kanuni mpya.

Ingawa tumefunga huduma za UberX, UberXL na UberX Saver nchini Tanzania, tuko tayari kushirikiana na mamlaka husika katika kuunda kanuni ambazo zitawezesha teknolojia kunawiri, ili tuanze tena kutoa huduma zetu zinazopendwa na watu wengu.

Asante, Tanzania!
Kuna App za wazawa kama TANTAXI ambazo ziko vizuri sana na zingeleta mabadiliko ila watu wamekariri uber na Bolt. Uwekezaji pia lazima utazame wawekezaji wa ndani ambao gharama zao za uendeshaji sio kubwa kivile kiasi haitowalazimu kuweka kamisheni kubwa kama ilivyo kwa Bolt na Uber: TanTaxi Passenger - Apps on Google Play. Hii TanTaxi haikati kamisheni kwa sasa na wamedhamiria kutovuka asilimia 10%. Abiria anafaidika na dereva anafaidika na kupata moyo wa kutoka huduma nzuri.
 
Back
Top Bottom