Ubaya wa kuwa na dhana mbaya kwa Binadamu wenzako

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,522
6,504
Dhana Mbaya ni Ile hali ya kuwafikiria wenzako vibaya juu ya Tabia zao au Matendo Yao Fulani pasina kuwa na ushahidi wowote ule.

Hii ni dhambi miongoni mwa madhambi ambayo Kwa Mwenyezi Mungu ni makubwa mno, kibinadamu tunaweza kuchukulia ni jambo dogo lakini Kwa Mola wetu ni kubwa mno.

Kuliweka hili Sawa nitahadithia kisa kilichowahi tokea enzi za Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) enzi hizo karibia miaka 1400 iliyopita.

Ilikuwa ni kipindi cha Vita ambapo nimesahau ilikuwa ni Vita gani dhidi ya makafiri, kulikuwa na upepo mkali Sana na hali ya hewa ilibadilika Sana, hivyo hivyo ikaamuliwa watu waondoke katika uwanja wa Vita.

Sasa bahati mbaya kipindi Hicho mama wa waumini bi Aisha (r.a) alikuwa ametoka nje ya gari la kuvutwa na farasi na kwenda washroom, huku nyuma wasaidizi wake walisahau kabisa kuwa Mama wa waumini alikuwa hajarejea bado katika hema na wala Mtume pamoja na Askari wengine hawakujua Hilo, basi wakaondoka na kurejea nyumbani huku wakimwacha bi Aisha nyuma pasina kufahamu.

Bi Aisha aliporejea akakuta msafara umeondoka, lakini bahati nzuri huku nyuma kulikuwa na Sahaba mmoja alibakia nyuma kuhakikisha hakuna kitu kilicho sahaulika ndo hamadi akamwona Mama wa waumini na kurejea nae.

Basi kama unavyojua wapuuzi huwa hawakosekani sehemu zote, basi wakazusha upuuzi kuwa bi Aisha alibaki nyuma na kufanya uchafu na Sahaba Yule, hakika ulizuka uzushi mkubwa mno na watu wengi wakiingia katika dhana mbaya juu ya bi Aisha, na walioeneza na kuushadadia ni Wale maadui wakubwa wa Uislamu kipindi kile.

Na Hali hii iliwatesa Sana waumini pamoja na Mtume na mpaka ikabidi Mtume akae mbali na bi Aisha Kwa tukio lile, lakini Alhamdulillah baadae Allah akashusha Aya kumtakasa bi Aisha na kusema hakika ule ulikuwa ni uwongo mkubwa, na hakika wamepata hasara wale wote ambao walizusha habari Ile. Na Allah akasema Hakika Jambo walilolizusha ni dhambi kubwa Sana mbele ya Allah na adhabu kubwa itawafikia wale wote walioshiriki isipokuwa Kwa ambaye atatubu.

Allah akahoji mambo yafuatayo kutokana na uzushi ule.

Je, habari Ile ilipowafikia waumini kwanini hawakuwa na dhana nzuri juu ya bi Aisha?

Kwanini hawakumdhania dhana nzuri bi Aisha na kuona ule ulikuwa ni upuuzi Tu?

Kwanini wasingeacha kueneza ule uzushi na ndimi zao Bila kuwa na uhakika na habari yenyewe?

Nadhani mpaka hapo msomaji wangu mpendwa umepata walau picha nazungumzia nini.

Haya mambo yamejaa Sana mitaani kwetu na majumba yetu, anatokea mpuuzi mmoja anasema Fulani anangoma na wote tunaenda na beat kuyazungumza tusiyokuwa na ushahidi nayo.

Fulani ni mzinzi, Fulani ni mchawi hao moja Kwa moja tunaamini hayo na kuyatangaza Kwa watu na mitaani pasina ushahidi wowote, hakika tunapata dhambi kubwa mbele za Mungu wetu na wallah tusipo tubia na kuacha hizi dhana mbaya Kwa watu hakika tutakuja kuangamia.

Kuna watu kutwa kucha Magufuli kamuua mwanaharakati Fulani, Je ukiitwa utoe ushahidi utaweza? Je siku ya mwisho utamwambia nini Mwenyezi Mungu? Nimetoa mfano wa Jiwe kwasababu tuna mfahamu na tunasema mengi juu yake lakini ole wetu Kwa kuyasema ambayo hatuna ushahidi nayo. Hakika tutakuja kuwajibika Kwa hayo na mengine mengi.

Msomaji wangu always penda kuwa na Dhana nzuri juu ya binadamu wenzako kwani Hilo ni jambo jema Kwa nafsi yako na Mungu wako pia.

Dini yangu inanifundisha kuwa hakika kukataza maovu na kuamrisha mema ni miongoni mwa Sadaka mbele ya Allah mjuzi wa yote.

# Aione pia baby zu

Ni hayo Tu!
 
Ma shaa allah, uzi mzuri sana huu hakika ktk vitu nahisi tunakosea sana kwenye maisha yetu ni kwenye swala la dhana, Allah atusamehe tu.

Naomba kujua.

1* dhana ambayo itabaki kwenye fikra tu bila kuisema popote nayo inaniingiza kwenye madhambi?

2* kwenye ibada ya dhikri je kupenda kuisfanya pasina kufungua mdomi ina juzu, yan kama upo mahala lkn unakua unamdhukuru Allah pasina kuchezesha midomo ni sahihi
 
Ma shaa allah, uzi mzuri sana huu hakika ktk vitu nahisi tunakosea sana kwenye maisha yetu ni kwenye swala la dhana, Allah atusamehe tu.

Naomba kujua.

1* dhana ambayo itabaki kwenye fikra tu bila kuisema popote nayo inaniingiza kwenye madhambi?

2* kwenye ibada ya dhikri je kupenda kuisfanya pasina kufungua mdomi ina juzu, yan kama upo mahala lkn unakua unamdhukuru Allah pasina kuchezesha midomo ni sahihi
Hii namba 1 ...na 2 ... Akhy tuletee dalili... Nitarudi badae hapa
 
Ma shaa allah, uzi mzuri sana huu hakika ktk vitu nahisi tunakosea sana kwenye maisha yetu ni kwenye swala la dhana, Allah atusamehe tu.

Naomba kujua.

1* dhana ambayo itabaki kwenye fikra tu bila kuisema popote nayo inaniingiza kwenye madhambi?

2* kwenye ibada ya dhikri je kupenda kuisfanya pasina kufungua mdomi ina juzu, yan kama upo mahala lkn unakua unamdhukuru Allah pasina kuchezesha midomo ni sahihi
Hakika katika kumtaja Allah pasina kutoa sauti inajuzu Sana na ni Jambo linalo pendeza zaidi.

Tuangalie dalili ifuatayo kutoka katika Qur'an

Allah (Subhanahu wataala) anasema kumwambia Mtume wake (swallallahu Alaih Wasallam) : "Na mtaje Mola wako Moyoni mwako Kwa unyenyekevu na khofu Bila kupiga makelele katika kauli ( na mtaje Mola wako) asubuhi na jioni!na wala usiwe miongoni mwa wenye kughafilika."
[Al Aaraf : 205]
 
Ma shaa allah, uzi mzuri sana huu hakika ktk vitu nahisi tunakosea sana kwenye maisha yetu ni kwenye swala la dhana, Allah atusamehe tu .
Naomba kujua .
1* dhana ambayo itabaki kwenye fikra tu bila kuisema popote nayo inaniingiza kwenye madhambi?
2* kwenye ibada ya dhikri je kupenda kuisfanya pasina kufungua mdomi ina juzu, yan kama upo mahala lkn unakua unamdhukuru Allah pasina kuchezesha midomo ni sahihj
Naam nashukuru kwa kuniita hapa, ama kuhusu dhana ni bora kujiepusha nayo kabisa kwasababu nyingi katika dhana ni wasiwasi kutoka kwa shetani na ni uchochezi wake, ila sisi umma wa mtume muhammad swala na salaam ziwe juu yake tumesamehewa muda wa kuwa hatujatamka ni kitu kimepita tu katika fikra.

Kuhusu adhkaar hili jambo pana muongozo kutoka kwa mola wetu mtukufu allah tabaaraka wa ta'alaa hivyo nitakunukulia hapa chini maneno yake na uyaingize katika utekelezaji kwa kujengea msingi swali lako.

Anasema allah tabaaraka wa ta'alaa
"Na mtaje mola wako katika nafsi yako kwa unyenyekevu na khofu, na bila ya kupiga kelele kwa kauli {mtaje} asubuhi na jioni, wala usiwe miongoni wa walioghafilika."
7:205

Hivyo utakachofanya ni kuchezesha midomo kwa unyenyekevu kwa sauti ya kunong'ona pasi na kuinyanyua au kuificha sana kwani allah si kiziwi wala hayuko mbali bali yuko karibu mno na ni msikivu mwenye kujua.

Hivyo wanawachuoni wakagawanya daraja za adhkaar kwa moyo, ulimi na moyo pamoja na ulimi basi hii ya mwisho ndio namna bora zaidi pale utakapomtaja mola wako kwa sauti ya chini kwa ulimi wako kisha ukahudhurisha moyo kwa tafakuri na mazingatio.

Wallahu a'alam.
 
Kuhusu namba moja kama alivyosema huyu ndugu yetu.

Ummati huu wa Muhammad tumesamehewa mambo ambayo yapo katika vichwa vyetu na mawazo yetu maadam Tu hatuja yatamka kinywani, hivyo kubwa jichunge kutotamka Kwa mdomo.

Na kuhusu dhikri kama ambavyo ametoa dalili na nilivyotoa Mimi, inajuzu pia kutamka katika moyo wako pasina kuchezesha midomo pia.
 
Hii namba 1 ...na 2 ... Akhy tuletee dalili... Nitarudi badae hapa
Jawabu
1.kuna hadithi inasema hatuandikiwi madhambi kwa yale ambayo hatujayatamka
Hadithi hii ipo katika kitabu kidogo ivi cha miatu hadithi
عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «إن الله تَجَاوَزَ عن أمتي ما حَدَّثَتْ به أَنْفُسَهَا، ما لم تَعْمَلْ أو تتكلم» قال قتادة: «إذا طَلَّقَ في نفسه فليس بشيء

Tafsiri
"Hakika ya Allah amesamehe umati wangu yale ambayo yanazungumza na nafsi zao,madam hajayafanya au kuyasema"


2.
( وَاذْكُر رَّبَّكَ فِي نَفْسِكَ تَضَرُّعًا وَخِيفَةً وَدُونَ الْجَهْرِ مِنَ الْقَوْلِ بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ الْغَافِلِينَ )

الأعراف (205) Al-A'raaf

Na mkumbuke Mola Mlezi wako nafsini kwako kwa unyenyekevu na khofu, na bila ya kupiga kelele kwa kauli, asubuhi na jioni. Wala usiwe miongoni wa walio ghafilika.


Aya hii inatufundisha kua kumdhukuru Allah sio lazima upige kelele kma wafanyavo Ahlul bidaa mfano hawa watu wa qadiriya
Bali yakupasa ww umdhukuru kwa sauti ya chini chini na mdomo utikisike kidogo
 
Si vibaya pia tukapata faida pia katika usomaji WA Qur'an pia.

Uqbah bin Amir (r.a) amesimulia kuwa amemsikia Mtume (s.a.w) akisema " Yule anayeisoma Qur'an Kwa sauti ni kama Yule anayetoa sadaka wazi wazi ,na Yule ambaye anaisoma kimya kimya ,ni kama Yule ambaye anatoa sadaka Kwa Siri"

Na siku zote tunajua hakika kutoa sadaka Kwa Siri ndio Bora zaidi.
 
Jawabu
1.kuna hadithi inasema hatuandikiwi madhambi kwa yale ambayo hatujayatamka
Hadithi hii ipo katika kitabu kidogo ivi cha miatu hadithi
عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «إن الله تَجَاوَزَ عن أمتي ما حَدَّثَتْ به أَنْفُسَهَا، ما لم تَعْمَلْ أو تتكلم» قال قتادة: «إذا طَلَّقَ في نفسه فليس بشيء

Tafsiri
"Hakika ya Allah amesamehe umati wangu yale ambayo yanazungumza na nafsi zao,madam hajayafanya au kuyasema"


2.
( وَاذْكُر رَّبَّكَ فِي نَفْسِكَ تَضَرُّعًا وَخِيفَةً وَدُونَ الْجَهْرِ مِنَ الْقَوْلِ بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ الْغَافِلِينَ )

الأعراف (205) Al-A'raaf

Na mkumbuke Mola Mlezi wako nafsini kwako kwa unyenyekevu na khofu, na bila ya kupiga kelele kwa kauli, asubuhi na jioni. Wala usiwe miongoni wa walio ghafilika.


Aya hii inatufundisha kua kumdhukuru Allah sio lazima upige kelele kma wafanyavo Ahlul bidaa mfano hawa watu wa qadiriya
Bali yakupasa ww umdhukuru kwa sauti ya chini chini na mdomo utikisike kidogo
Shukran ukhty baby zu njoo huku ahl Elim washafanya yao
 
Hakika katika kumtaka Allah pasina kutoa sauti inajuzu Sana na ni Jambo linalo pendeza zaidi.

Tuangalie dalili ifuatayo kutoka katika Qur'an

Allah (Subhanahu wataala) anasema kumwambia Mtume wake (swallallahu Alaih Wasallam) : "Na mtaje Mola wako Moyoni mwako Kwa unyenyekevu na khofu Bila kupiga makelele katika kauli ( na mtaje Mola wako) asubuhi na jioni!na wala usiwe miongoni mwa wenye kughafilika."
[Al Aaraf : 205]
Hiyo asbaabun nuzul ya bi Aisha ni mtego wa shia kumchafua bi Aisha,si wajua Wana ugomvi nae na wanavomuita!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom