Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 3,522
- 6,504
Dhana Mbaya ni Ile hali ya kuwafikiria wenzako vibaya juu ya Tabia zao au Matendo Yao Fulani pasina kuwa na ushahidi wowote ule.
Hii ni dhambi miongoni mwa madhambi ambayo Kwa Mwenyezi Mungu ni makubwa mno, kibinadamu tunaweza kuchukulia ni jambo dogo lakini Kwa Mola wetu ni kubwa mno.
Kuliweka hili Sawa nitahadithia kisa kilichowahi tokea enzi za Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) enzi hizo karibia miaka 1400 iliyopita.
Ilikuwa ni kipindi cha Vita ambapo nimesahau ilikuwa ni Vita gani dhidi ya makafiri, kulikuwa na upepo mkali Sana na hali ya hewa ilibadilika Sana, hivyo hivyo ikaamuliwa watu waondoke katika uwanja wa Vita.
Sasa bahati mbaya kipindi Hicho mama wa waumini bi Aisha (r.a) alikuwa ametoka nje ya gari la kuvutwa na farasi na kwenda washroom, huku nyuma wasaidizi wake walisahau kabisa kuwa Mama wa waumini alikuwa hajarejea bado katika hema na wala Mtume pamoja na Askari wengine hawakujua Hilo, basi wakaondoka na kurejea nyumbani huku wakimwacha bi Aisha nyuma pasina kufahamu.
Bi Aisha aliporejea akakuta msafara umeondoka, lakini bahati nzuri huku nyuma kulikuwa na Sahaba mmoja alibakia nyuma kuhakikisha hakuna kitu kilicho sahaulika ndo hamadi akamwona Mama wa waumini na kurejea nae.
Basi kama unavyojua wapuuzi huwa hawakosekani sehemu zote, basi wakazusha upuuzi kuwa bi Aisha alibaki nyuma na kufanya uchafu na Sahaba Yule, hakika ulizuka uzushi mkubwa mno na watu wengi wakiingia katika dhana mbaya juu ya bi Aisha, na walioeneza na kuushadadia ni Wale maadui wakubwa wa Uislamu kipindi kile.
Na Hali hii iliwatesa Sana waumini pamoja na Mtume na mpaka ikabidi Mtume akae mbali na bi Aisha Kwa tukio lile, lakini Alhamdulillah baadae Allah akashusha Aya kumtakasa bi Aisha na kusema hakika ule ulikuwa ni uwongo mkubwa, na hakika wamepata hasara wale wote ambao walizusha habari Ile. Na Allah akasema Hakika Jambo walilolizusha ni dhambi kubwa Sana mbele ya Allah na adhabu kubwa itawafikia wale wote walioshiriki isipokuwa Kwa ambaye atatubu.
Allah akahoji mambo yafuatayo kutokana na uzushi ule.
Je, habari Ile ilipowafikia waumini kwanini hawakuwa na dhana nzuri juu ya bi Aisha?
Kwanini hawakumdhania dhana nzuri bi Aisha na kuona ule ulikuwa ni upuuzi Tu?
Kwanini wasingeacha kueneza ule uzushi na ndimi zao Bila kuwa na uhakika na habari yenyewe?
Nadhani mpaka hapo msomaji wangu mpendwa umepata walau picha nazungumzia nini.
Haya mambo yamejaa Sana mitaani kwetu na majumba yetu, anatokea mpuuzi mmoja anasema Fulani anangoma na wote tunaenda na beat kuyazungumza tusiyokuwa na ushahidi nayo.
Fulani ni mzinzi, Fulani ni mchawi hao moja Kwa moja tunaamini hayo na kuyatangaza Kwa watu na mitaani pasina ushahidi wowote, hakika tunapata dhambi kubwa mbele za Mungu wetu na wallah tusipo tubia na kuacha hizi dhana mbaya Kwa watu hakika tutakuja kuangamia.
Kuna watu kutwa kucha Magufuli kamuua mwanaharakati Fulani, Je ukiitwa utoe ushahidi utaweza? Je siku ya mwisho utamwambia nini Mwenyezi Mungu? Nimetoa mfano wa Jiwe kwasababu tuna mfahamu na tunasema mengi juu yake lakini ole wetu Kwa kuyasema ambayo hatuna ushahidi nayo. Hakika tutakuja kuwajibika Kwa hayo na mengine mengi.
Msomaji wangu always penda kuwa na Dhana nzuri juu ya binadamu wenzako kwani Hilo ni jambo jema Kwa nafsi yako na Mungu wako pia.
Dini yangu inanifundisha kuwa hakika kukataza maovu na kuamrisha mema ni miongoni mwa Sadaka mbele ya Allah mjuzi wa yote.
# Aione pia baby zu
Ni hayo Tu!
Hii ni dhambi miongoni mwa madhambi ambayo Kwa Mwenyezi Mungu ni makubwa mno, kibinadamu tunaweza kuchukulia ni jambo dogo lakini Kwa Mola wetu ni kubwa mno.
Kuliweka hili Sawa nitahadithia kisa kilichowahi tokea enzi za Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) enzi hizo karibia miaka 1400 iliyopita.
Ilikuwa ni kipindi cha Vita ambapo nimesahau ilikuwa ni Vita gani dhidi ya makafiri, kulikuwa na upepo mkali Sana na hali ya hewa ilibadilika Sana, hivyo hivyo ikaamuliwa watu waondoke katika uwanja wa Vita.
Sasa bahati mbaya kipindi Hicho mama wa waumini bi Aisha (r.a) alikuwa ametoka nje ya gari la kuvutwa na farasi na kwenda washroom, huku nyuma wasaidizi wake walisahau kabisa kuwa Mama wa waumini alikuwa hajarejea bado katika hema na wala Mtume pamoja na Askari wengine hawakujua Hilo, basi wakaondoka na kurejea nyumbani huku wakimwacha bi Aisha nyuma pasina kufahamu.
Bi Aisha aliporejea akakuta msafara umeondoka, lakini bahati nzuri huku nyuma kulikuwa na Sahaba mmoja alibakia nyuma kuhakikisha hakuna kitu kilicho sahaulika ndo hamadi akamwona Mama wa waumini na kurejea nae.
Basi kama unavyojua wapuuzi huwa hawakosekani sehemu zote, basi wakazusha upuuzi kuwa bi Aisha alibaki nyuma na kufanya uchafu na Sahaba Yule, hakika ulizuka uzushi mkubwa mno na watu wengi wakiingia katika dhana mbaya juu ya bi Aisha, na walioeneza na kuushadadia ni Wale maadui wakubwa wa Uislamu kipindi kile.
Na Hali hii iliwatesa Sana waumini pamoja na Mtume na mpaka ikabidi Mtume akae mbali na bi Aisha Kwa tukio lile, lakini Alhamdulillah baadae Allah akashusha Aya kumtakasa bi Aisha na kusema hakika ule ulikuwa ni uwongo mkubwa, na hakika wamepata hasara wale wote ambao walizusha habari Ile. Na Allah akasema Hakika Jambo walilolizusha ni dhambi kubwa Sana mbele ya Allah na adhabu kubwa itawafikia wale wote walioshiriki isipokuwa Kwa ambaye atatubu.
Allah akahoji mambo yafuatayo kutokana na uzushi ule.
Je, habari Ile ilipowafikia waumini kwanini hawakuwa na dhana nzuri juu ya bi Aisha?
Kwanini hawakumdhania dhana nzuri bi Aisha na kuona ule ulikuwa ni upuuzi Tu?
Kwanini wasingeacha kueneza ule uzushi na ndimi zao Bila kuwa na uhakika na habari yenyewe?
Nadhani mpaka hapo msomaji wangu mpendwa umepata walau picha nazungumzia nini.
Haya mambo yamejaa Sana mitaani kwetu na majumba yetu, anatokea mpuuzi mmoja anasema Fulani anangoma na wote tunaenda na beat kuyazungumza tusiyokuwa na ushahidi nayo.
Fulani ni mzinzi, Fulani ni mchawi hao moja Kwa moja tunaamini hayo na kuyatangaza Kwa watu na mitaani pasina ushahidi wowote, hakika tunapata dhambi kubwa mbele za Mungu wetu na wallah tusipo tubia na kuacha hizi dhana mbaya Kwa watu hakika tutakuja kuangamia.
Kuna watu kutwa kucha Magufuli kamuua mwanaharakati Fulani, Je ukiitwa utoe ushahidi utaweza? Je siku ya mwisho utamwambia nini Mwenyezi Mungu? Nimetoa mfano wa Jiwe kwasababu tuna mfahamu na tunasema mengi juu yake lakini ole wetu Kwa kuyasema ambayo hatuna ushahidi nayo. Hakika tutakuja kuwajibika Kwa hayo na mengine mengi.
Msomaji wangu always penda kuwa na Dhana nzuri juu ya binadamu wenzako kwani Hilo ni jambo jema Kwa nafsi yako na Mungu wako pia.
Dini yangu inanifundisha kuwa hakika kukataza maovu na kuamrisha mema ni miongoni mwa Sadaka mbele ya Allah mjuzi wa yote.
# Aione pia baby zu
Ni hayo Tu!