UBAKWAJI WA TELEZA: Mtoto aathirika kisaikolojia kwa kushuhudia unyama wa Teleza dhidi ya dada zake

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138
Teleza ni jina linalomaanisha aina ya ubakaji unaotokea ndani ya kata ya Mwanga Kusini katika Halmashauri ya Kigoma Ujiji Mkoani Kigoma.

Jina hili lilitokana na kwamba, wakati wa usiku kuna wanaume wamekuwa wakiingia kwenye nyumba wanazoishi wanawake na kuwabaka. Watu hawa kabla ya kufika kwa mwanamke mlengwa huvua nguo zote na kubaki kama alivozaliwa, kisha wanajipaka grease ama mafuta ya kula mwili mzima. Baada ya hapo hubeba silaha aina ya kisu kikali ama mapanga, huvunja, ama hubomoa na kuingia kwenye nyumba anamoishi mwanamke kwa nia ya kubaka, kujeruhi, kuharibu mali na kuiba.

Simulizi kutoka kwa binti wa kidato cha tatu aliyeshuhudia unyama huu wa TELEZA.

Tukio hili lilitokea mwaka jana nikiwa form two. Tunaishi kwenye nyumba ya kupanga na tunapanga chumba na sebule. Tunaishi na mama yetu pekee, tukiwa watoto watano wa kike. Siku ya tukio, ndugu zangu wawili walikuwa wamekwenda kijijini. Na hapo tulikuwa na mgeni ambaye alikuja kututembelea akiwa na katoto ka kiume miaka kumi. Mtoto wa mama mkubwa. Mtoto wa kiume huyu mwenye miaka kumi alilala kwenye kochi sebuleni. Sisi wasichana tulilala chumbani na mama yetu siku hiyo alienda kulala kwenye msiba hapo jirani.

Tukiwa tumelala usiku wa manane, hatukusikia kitu chochote, japo mdogo wetu wa kiume aliyekuwa sebuleni alisikia huyu kijana jinsi alivyovunja kioo cha kwenye dirisha na kufungua mlango. Alijifanya amelala kwa woga.

Yule TELEZA alipingia ndani alienda moja kwa moja kwa yule mtoto kwenye kochi akamvua nguo na kumchunguza. Alipogundua kwamba ni wa kiume akamuacha ndo akaja chumbani kwetu.

Mimi binafsi sikumsikia akiingia chumbani bali nilimsikia akimlazimisha dada yetu (Mgeni) avue chupi na wakati huo huo akimtishia kwa panga. Ndipo na mimi nilistuka, na wadogo zangu wengine walistuka na kuanza kupiga kelele. Alitupiga kwa mapanga na mara nyingine alitukata kwa hilo panga lake. Tulizidi kulia kwa hofu maana tiyari tulishaumizwa sana.

Alipoona hatunyamazi akachukua mwiko mkubwa na kuanza kututandika nao. Wote tulikuwa tunajificha nyuma ya dada yetu ambaye aliumizwa Zaidi. Baba mwenye nyumba alisikia lakini walishindwa kutoka kwasababu walifungiwa nje pamoja na majirani wengine.

Walianza kupiga simu kwa mama, na mpaka watu wanafika tiyari tulishaumizwa vibaya sana. Dada yetu alizimia. Tulikimbizwa police na hatimaye kukimbizwa hospitali na kushonwa nyuzi tano tano kila mmoja wetu.

Tukio liliniogopesha sana. Lakini baada ya hapo jamii na shuleni ndio kuliniogopesha Zaidi. Nilitamani kuhama shule na nikamwambia mama yangu, lakini kwa kuwa hana uwezo na tiyari alishaingia gharama za kutufanyia matibabu ambayo ilibidi auze godoro moja ilibidi nivumilie tu.

Shuleni wanafunzi walinitania saana kwa kuniita majina na kwamba mimi ni mke TELEZA. Lakini nilijikaza mpaka sasa wanaonekana wamesahau, labda mara moja moja mtu aamue tu kunichokoza kwa kuniita mke wa TELEZA.

Kwasasa siwezi kubeba kitu chochote kichwani kwani nilikatwa mapanga ya kichwani. Na dada yangu alimaliza mwezi mzima akivuja damu puani. Alivyopona aliondoka.

Mama wa binti

Mimi biashara zangu ni kuuza dagaaa sokoni. Siku tukio limetokea sikuwa na pesa hata kidogo. Lakini ilibidi nikope kwa watu ili niweze kukodi tax itupeleke police ajili ya kupata PF3 kwa watoto 2 ilikuwa elfu 10,000. Kisha taxi hiyo ikatupeleka hospitali ambako walishonwa kwa elfu 30,000 kwa kila mtoto na kununua madawa kwa ajili ya matibabu.

Hizi pesa hazikuwa kwenye mpango wangu na ilibidi niuze godoro la watoto ili niweze kulipa madeni ya matibabu.

Jamii bado walisema kwamba huyu TELEZA alikuwa ni bwana wangu kwa kuwa mimi sina mume alishafariki. Na wengine waliongeza kuwa nimekula pesa za hao vijana ndio maana wamewaingilia watoto wangu. Hii sentensi ilikuwa inanihuzunisha sana kwani nilihofia kama watoto wangu wataamini wataniona mimi ni mbaya. Nashukuru Mungu walielewa tu.

NA mtoto wangu wangu wa mwisho naona tangu siku hiyo amekuwa mgonjwa kabisa. Hayuko vizuri kiakili. Maana alishuhudia tukio zima. Sasa amebaki na woga wa hali ya juu sana. Ikiingia jioni anaanza kujikunyata na kusikia baridi sana. Hayuko sawa kabisa.
 
Write your reply...Awamu hii tutaona na kusikia mengi sana.Sasa ni mwendo wa kuteleza tu.Nanyi Waha ubishi wote ule mnashindwa kutongoza hadi mbake!?Mmeniaibisha kwakweli dada zenu wenyewe wanahuruma na wanaelewa haraka acheni kubaka tongozeni ee bhana!Aaah ni mwendo wa kuteleza tu cc:Numbisa
 
Dah poleni sana huko Kigoma. Ila it does not change kwamba Tanzania kuna amani huu ni uhalifu mdogo mdogo ambao serikali itabidi ichukue hatua kali kupambana nao.
Fact: Tanzania ni inchi ya amani yenye raia wasio na furaha.
 
Watu wanaumia wanapigwa na kujeruhiwa anakimbilia police anaambiwa leta hela, really?
Hao wa kulipa ni hao wahalifu watafutwe wakamatwe na walipe fidia za majeruhi na jela waende
Vingine ni uonezi tu
Sheria zingine mpaka unajiuliza nani anatunga?
 
Hiyo PF3 ndio mtihani kwa maskini, kwanini watoze?
Tozo kila mahali halafu utendaji zero
Watu wanaumia wanapigwa na kujeruhiwa anakimbilia police anaambiwa leta hela, really?
Hao wa kulipa ni hao wahalifu watafutwe wakamatwe na walipe fidia za majeruhi na jela waende
Vingine ni uonezi tu
Sheria zingine mpaka unajiuliza nani anatunga?
Hakuna mahala mama amesema alitozwa pesa kwa ajili ya pf3,acha chuki kwa jeshi la polisi.Ulinzi unaanzia ndani ya jamii husika sasa wewe unafikiri polisi mmoja anatakiwa kulinda wananchi wangapi?

Wanadamu wanaweza kufanya uhalifu wowote ule na sio kwamba jeshi letu la polisi halifuatilii,kule zanzibar kulikuwa na ishu ya mazombi,wamebanwa huko sasa wamehamia kigoma wamebadili jina lao na kujiita teleza.

Nashauri hao wajane kwa namna yoyote ile wana majirani na kaka zao,shemeji zao wanatakiwa kushirikiana kwanza kuweka ulinzi wa familia na hapo polisi wataanzia hapo.
 
HAKUNA MAHALA MAMA AMESEMA ALITOZWA PESA KWA AJILI YA PF3,ACHA CHUKI KWA JESHI LA POLISI.ULINZI UNAANZIA NDANI YA JAMII HUSIKA SASA WEWE UNAFIKIRI POLISI MMOJA ANATAKIWA KULINDA WANANCHI WANGAPI?
WANADAMU WANAWEZA KUFANYA UHALIFU WOWOTE ULE NA SIO KWAMBA JESHI LETU LA POLISI HALIFUATILII,KULE ZANZIBAR KULIKUWA NA ISHU YA MAZOMBI,WAMEBANWA HUKO SASA WAMEHAMIA KIGOMA WAMEBADILI JINA LAO NA KUJIITA TELEZA.
NASHAURI HAO WAJANE KWA NAMNA YOYOTE ILE WANA MAJIRANI NA KAKA ZAO,SHEMEJI ZAO WANATAKIWA KUSHIRIKIANA KWANZA KUWEKA ULINZI WA FAMILIA NA HAPO POLISI WATAANZIA HAPO.
Umekurupuka bila kusoma yote
Umejibu kwa mihemko sana
Soma tena kisa cha mama na binti utaona kalipa 10000
Unajitoa ufahamu kutetea ujinga
Police wapo kwa ajili ya kutulinda sisi na mali zetu.
Haki yetu hiyo na huwezi kuibadili
Jibu hoja bila jazba
 
Umekurupuka bila kusoma yote
Umejibu kwa mihemko sana
Soma tena kisa cha mama na binti utaona kalipa 10000
Unajitoa ufahamu kutetea ujinga
Police wapo kwa ajili ya kutulinda sisi na mali zetu.
Haki yetu hiyo na huwezi kuibadili
Jibu hoja bila jazba

Unayejibu kwa jaziba ni wewe?unabeza watunga sheria lakini lakini husemi kwa uwazi kuwa ni sheria ipi imeruhusu watu kuvunja amani au kufanya uhalifu.

ukisoma maelezo ya uyo mama na wahanga wengine wanadai ya kuwa hata vikao vya wazee kijijini hapo vilipo kaa wazee hawakufikia muafaka baada ya baadhi yao kusema kuwa inawezekana wanakula pesa za wanaume(hapo ndo niliposema kuwa jamii husika ianze kubadilika maana nina uhakika vijana hao wanawajua na wanaishi kijijini hapo),kama ulivyo unyanyasikaji mwingine tu ndani ya familia zetu hivyo ndo maana nilishauri jamii husika kwa kupitia vikao vyake iwabaini hao watu na polisi wataanzia hapo.

Kulitegemea jeshi la polisi hata kukulindia mkeo na watoto ili warudi nyumbani mapema sio wajibu wao bali huu ni wajibu wa muhimu sana kwako.Nina jua unayohaki kisheria ya kulindwa na jeshi la polisi lakini kujiwekea tahadhali na kupunguza vihatarishi hilo ni jukumu lako la karibu.

Kuhusu kutoa pesa ya Pf3 hatuwezi kulisemea sana maana tunaona ameainisha gharama zote zikiwemo za matibabu lakini hajatuonesha akitaja kiasi alichomlipa dreva tax.
 
Unayejibu kwa jaziba ni wewe?unabeza watunga sheria lakini lakini husemi kwa uwazi kuwa ni sheria ipi imeruhusu watu kuvunja amani au kufanya uhalifu.
ukisoma maelezo ya uyo mama na wahanga wengine wanadai ya kuwa hata vikao vya wazee kijijini hapo vilipo kaa wazee hawakufikia muafaka baada ya baadhi yao kusema kuwa inawezekana wanakula pesa za wanaume(hapo ndo niliposema kuwa jamii husika ianze kubadilika maana nina uhakika vijana hao wanawajua na wanaishi kijijini hapo),kama ulivyo unyanyasikaji mwingine tu ndani ya familia zetu hivyo ndo maana nilishauri jamii husika kwa kupitia vikao vyake iwabaini hao watu na polisi wataanzia hapo.
Kulitegemea jeshi la polisi hata kukulindia mkeo na watoto ili warudi nyumbani mapema sio wajibu wao bali huu ni wajibu wa muhimu sana kwako.Nina jua unayohaki kisheria ya kulindwa na jeshi la polisi lakini kujiwekea tahadhali na kupunguza vihatarishi hilo ni jukumu lako la karibu.
Kuhusu kutoa pesa ya Pf3 hatuwezi kulisemea sana maana tunaona ameainisha gharama zote zikiwemo za matibabu lakini hajatuonesha akitaja kiasi alichomlipa dreva tax.
Noted
 
Majimbo yote yanayoongozwa na Chadema umejaa ujinga ,ushirikina na uchawi.
 
Write your reply...Awamu hii tutaona na kusikia mengi sana.Sasa ni mwendo wa kuteleza tu.Nanyi Waha ubishi wote ule mnashindwa kutongoza hadi mbake!?Mmeniaibisha kwakweli dada zenu wenyewe wanahuruma na wanaelewa haraka acheni kubaka tongozeni ee bhana!Aaah ni mwendo wa kuteleza tu cc:Numbisa
Wamanyema hao mkuu.
 
Back
Top Bottom