rugumye
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 561
- 179
Mimi sikubahatika kuangalia kipindi hicho lakini hapa kazini kwangu kuna staff mwenzetu alikuwa amepangiwa kituo cha kazi Zanzibar kama driver yeye ni mtu wa bara. kutokana na kubaguliwa na wazanzibar imebidi aombe kuhamishwa kituo cha kazi ili arudi Bara. anasimulia kuwa ilifika wakati akanyimwa hata sehemu ya kupaki gari katika ofisi ya wizara moja ambayo sisi tunafanya nao kazi kawapa support. ilimbidi kuripoti kwa katibu mkuu wa wizara. kwa bahati nzuri katibu mkuu ni mwelewa akawasema sana wale drivers akawambia waache upemba. staff wetu aliendelea kuvumilia lakini hali ilizidi kuwa mbaya kwaani ubaguzi ulizidi na akaona maisha yake yako hatarini hivyo ameamua kurudi Bara tangu juzi. JAMANI HALI SIYO ZENJ. UBAGUZI WA ZENJ UNAKARIBIA ULE WA MAKABURU AFRIKA KUSINI. katika ofisi za bara kuna wazanzibar kibao wanafanya kazi na wamejenja na wala hakuna misukosuko wanayoipata:embarassed2: