Uamuzi wa NEC pigo kwa UKAWA

Uamuzi wa NEC pigo kwa UKAWA

....sasa ni hakika ccm imeshakufa hahahaaa ....
 
USHINDI wa Magufuli ni hakika.unaanzia Babati,Karatu na Monduli
 
Mimi mtu anaponambia magufuli atashinda naomba anipe sababu angalau nne za kunishawishi niamini ushindi wake
 
Rkebisha kichwa cha habari, UKAWA ndo wanamuuomba Malaika aendelee kukaa na Damian Lubuva kura zote zihesabiwe matokeo kubandikwa vituoni.
 
Ukisikia kuna habari toka kwa waliochanganyikiwa wakiwa "news room" kwenda kwa mixed audience ndo kama hii... Spin doctoring!!

Bila tume kubanwa vizuri kila angle maelezo hayo ya Lubuva tungeyajuaje..??.
Ni hivi tutajumlisha matokeo ya vituo vyote mapemaa kabla ya tume... Sasa waje wajumlishe tofauti waone moto wake..!!

Exactly mkuu hakika moto utawaka
 
Kama umewahi kuendesha kesi za uchaguzi usinge sema haya. Matokeo huwa yanabadilishwa wilayani na hata wakala apinge vipi lakini mtu wa IT pale wilayani huwa anapata agizo la mkurugenzi kuwa kura za kituo fulani kipo sawa scan tume NEC. Vile vile elewa kuwa matokeo ya urais hayapingwi mahakamani, yakishatangazwa hata kama kuna uongo wa wazi wazi ndio inakuwa imetoka hiyo. Dawa pekee ya kupinga matokeo ya urais ni riot tu. Zile carbonated copy wanazopewa mawakala vituoni huwa zinafutika baada ya muda si mrefu hivyo ukizileta mahakamani kama ushahidi huwa hazionekani vizuri hivyo Jaji kushindwa kuzitumia, inambidi atumie ile original ambayo hubadilishiwa wilayani. Watalamu wa kufoji saini wanakuwepo, ya msimamizi wa kituo inakuwa halali kwani huitwa usiku kuja kusaini mpya, wengi ni watumishi wa halmashauri na wapo chini ya mkurugenzi wa hiyo halmashauri


Sasa ni kwanini mnaingia kwenye uchaguzi kama mna uhakika wa 100% kwamba mtaibiwa kura? Ni kwanini msilianzishe sasa hivi tu badala ya kupoteza muda?

Kwangu mimi mnaonekana siyo watu intelligent kabisa kwa maana hata hamuelewi jinsi Dunia inavyo kwenda, ni hivi ili fisadi Lowasa aweze kuwashahwishi manyumbu kama wewe mpinge matokeo na kuandamana ni lazima kwanza aiweke International community upande wake sasa International Community yote iko hapa tayari kufanya tasmini ya uchaguzi na mwishowe watasema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki na kupeleka ripoti kwa wakubwa zao SADC, EAC, EU, UN n.k baada ya hapo mshindi ataapishwa sasa hayo maandamano yenu mtapigwa risasi na kuumizwa fisadi Lowasa atakimbia yeye na familia yake na kuwaacha manyumbu peke yenu bilaa mtetezi!
 
Mkuu umeyasema vizuri magamba, maana yalikuwa yanategemea sana hii mbereko ya kusafirisha masanduku kwenda wilayani!! Nafikri mnakumbuka habari ya Makongoro Mahanga!! Sasa hapa walioumbuka ni maccm!!
 
Kwani mleta mada kakosea nini? Nyinyi si ndio mlikuwa mnadai kwamba kura zenu zitahibiwa na kuwakosesha ushindi!! Jaji Lubuva kawatolea uvivu kwa kutangazia Dunia kwamba kila kitu kitaweka wazi kituoni - baada ya Jaji ku-pre empty njama zenu za kuchochea/hamasisha wafuasi wenu wafanye fujo vituoni siku ya upigaji kura sasa mnakuja madai mapya, akili zenu

Siku zote chadema ni kama genge la vichaa wenye unafuu wa kumbukumbu kidogo, kumbe ndo nimegundua kuwa hawajiamini kuongoza nchi ndo maana walitapatapa kumtafuta Mzee Warioba, walidhani na yy ni chizi kama wao, mzee akawashitilia mbali, mara wakakutana na fisadi na yy akawaonjesha pesa za richmond, waliposikia utamu wake wote wakabadilisha wimbo eti miaka nane hakuwa serikalini, mm nawauliza kuwa alikuwa wapi? na mbona miaka nane yote wamezunguka wakisema ubaya wake, na maandalizi ya kuendelea kumchafua yalipangwa endapo angepitishwa na chama chake kuwa mgombea urais, leo kuhama wanaleta ujinga eti miaka nane hakuwa serikalini, unajua ni wachache ambao wataamini upuuzi huo, na kwa kuwa walisha wajenga hivyo baadhi ya wanachama wao na wameamini hivo-du tuwapatie pole sana hawa wenzetu, lakini wengi wetu ni Makufuri for change(M4C)
 
Sasa hapo pigo la ukawa ni lipi???...nani ambaye amekuwa mnufaika na mfumo wa kubebelea masanduku kwenda wilayani??? Magazeti mengine hayafai hata kufungia vitumbua...!!!
 
Ni ajabu unamkuta mtu anayo kura moja ya kwake tu lkn ansema tutashinda
we hesabu kura yako tu.Mtu ana kura saba ndani ya nyumba yake lkn anayoiamini ni moja tu ya kwake maana kila mmoja ana maamuzi yake binafsi tuache kujidanganya.
 
Mi adhani njia bora ya kudeal na Upuuzi kama huu alioleta Ikungi ni Kuupuuza na kusonga mbele. Hawa watu wapo tu kwenye jamii !
 
ccm mnachekesha kweli! Dongo linalowahusu mnakimbilia kuanzisha thread na kulielekeza UKAWA.
NONSENSE AND SHAME ON YOU
 
ikungi

JK ni professor wa siasa, lowasa na ufisadi wake hamuwezi, Dr Magufuli ndiyo rais


Serikali yangu ndio imewafikisha hapa.... By Kikwete

Majizi na Majambazi ndio yametufikisha hapa.... by Magufuli



Hahahahahahah Raha tupu...


Ndio maraisi wenu hao
 
Last edited by a moderator:
Siku zote chadema ni kama genge la vichaa wenye unafuu wa kumbukumbu kidogo, kumbe ndo nimegundua kuwa hawajiamini kuongoza nchi ndo maana walitapatapa kumtafuta Mzee Warioba, walidhani na yy ni chizi kama wao, mzee akawashitilia mbali, mara wakakutana na fisadi na yy akawaonjesha pesa za richmond, waliposikia utamu wake wote wakabadilisha wimbo eti miaka nane hakuwa serikalini, mm nawauliza kuwa alikuwa wapi? na mbona miaka nane yote wamezunguka wakisema ubaya wake, na maandalizi ya kuendelea kumchafua yalipangwa endapo angepitishwa na chama chake kuwa mgombea urais, leo kuhama wanaleta ujinga eti miaka nane hakuwa serikalini, unajua ni wachache ambao wataamini upuuzi huo, na kwa kuwa walisha wajenga hivyo baadhi ya wanachama wao na wameamini hivo-du tuwapatie pole sana hawa wenzetu, lakini wengi wetu ni Makufuri for change(M4C)

Splendid indeed - jamaa hawa hawajambo kwenye nyanja za maigizo/usanii, actually ni suicidal/Kamikaze/Hara-Kiri kuwapa kura zetu ma flip floppers kama hawa, hawana kanuni kama gari moshi la kwenda Mpanda!! Viongozi wa design ya UKAWA Taifa aliwezi kujua likiwakabidhi Nchi, kesho watafanya maigizo gani hatarishi - ndio maana hivi sasa wapiga kura wengi mijini na vijijini hasa vijijini wamekwisha washtukia hivyo hawawezi kufanya makosa come October.

Kwa nini nasema hivyo - Mkuu kama unakumbuka vizuri Mh.Lowassa alipokuwa kwenye kinyanganyiro cha kuteuliwa na CCM kuwa mgombea wa Urais, wapinzani hasa hasa CHADEMA walikuwa overly vocal wakimpinga Mh.Lowassa - oh yes, walitayarisha dossier kubwa kuliko ya Encyclopedia Britannica yenye lengo la kumumaliza kisiasa Mh.Lowassa!! Lissu na Mbowe were spitting fire kwamba Lowassa akiteuliwa tu na CCM basi wao watahanika adhalani kila kitu, if my memories serves me right Mh.Mbowe aliongezea kwamba kwa jinsi wanavyo mfahamu Mh.Lowassa hawawezi kumkubalia mtu ambaye ni liability kisiasa ahamie kwenye chama chao just in case akitemwa na CCM - just imagine 4 a second!

Waandishi wa habari walipo mhoji zaidi Mh.Mbowe kama kweli yuko sincere na kauli yake ya kusema hawezi kumkubalia Mh.Lowassa ahamie CHADEMA, Mbowe alijibu +ve, si hilo tu Mh.Mbowe kuongezea kwamba labda Mh.Lowassa ahamie CHADEMA over his dead body - hii ilikuwa kauli nzito sana!!

Kinacho nishangaza mimi! Mh.Mbowe is unquestionably an Intelligent man sasa ni kitu gani kilicho mfanya agehuke/fanye a U-turn?? Mwanzo nilijiuliza maswali mengi kuhusu ukigehu gehu wa Viongozi hawa, lakini baada ya kuwasoma kisaikolojia wakina Mh.Mbowe na Mh.Mbatia kwa siku za hivi karibuni nikaja gunduwa kwamba architect/Engineer/the brains behid uhamiaji wa Mh.Lowassa kwenda UKAWA ulitokana na shinikizo/ushawishi wa Mh.Mbatia, ndio maana yuko mstari wa mbele sana kumkingia kifua hata ambapo hakuna ulazima wa kufanya hivyo atajitokeza tu kumtetea/kumsemea as if Mh.Lowassa hana uwezo wa kijieleza - why??

Sasa jaribu kumwangalia Mh.Mbowe kwa umakini unaona wazi wazi body language yake haiko in sync na kauli zake za kumtetea Mh.Lowassa, anajikaza hivyo hivyo kisabuni afanyeje - deep down anajua wajanja walimzidi kete akajikuta anafanya a blunder of a century ambayo itakisambaratisha CHADEMA au yeye mwenyewe kulazimishwa ku-resign unceremoniously baada ya uchaguzi kumalizika; however, tukija kwa Mh.Mbatia huyo is different- he knows chances za UKAWA kushinda kiti cha URAIS ni slim indeed ndio maana masaa yote anazungumzia kuhibiwa kura,kulinda kura vituoni unaweza kufikiri hawana wakala wao vituoni, kuitisha a makeshift press conferences kujaribu ku-counter vitu ambavyo havipo kabisa - one gets an impression kana kwamba kuna a latent contention na current Admin ambayo kiukweli ndio ilimpa Ubunge on a silver plate - ya nini bwana kuwazulia? Mara ooh sijui intelligensia yao imegunduwa njama fulani - mtu unaweza kufikiri labda Taifa letu lina a Govt within a Govt - hajui kwamba kauli zake zinaweza kuchochea uvunjifu wa AMANI, hayuko makini na kauli zake hata kidogo.

Ninacho washauri Watanzania wenzangu kwa nia njema tu, jamani tusishabikie Viongozi ambao hawatabiriki, mifano hai nimeitaja hapo juu - mabadiliko kweli yanaitajika Nchini lakini si kwa kupitia Viongozi wa design ya UKAWA - tunawezaje kuamini Viongozi ambao leo wasema hili kesho wasema lile, je Viongozi kama hao kweli wana nia ya kuleta mabadiliko ya kweli Nchini au wana ajenda zao na wajanja wenzao za kutuacha kwenye MATAA Watanzania tulio wengi - Mtanzania mwenzangu siku ya kura mpe kura yako ya ndio Dk.ISOTOPES TINGATINGA ndiye mwenye ufunguo wa kufungua MAKUFURI ya kuleta mabadiliko ya kweli Nchini, kwanza hana deni la mtu, hajachangiwa na mtu si wananchi wa kawaida au wafanya biashara wakubwa, hilo tu linamuweka huru kiutendaji wake kazi hakuna mtu yeyote mwenye uwezo kifedha anaweza kumuweka mfukoni au kumchezea, sasa Watanzania wenzangu Mungu atupe nini zaidi ya Dk. wa kweli. Najua baadhi ya members watanisema kweli kweli, lakini wakumbuke niliyo sema humu yametoka moyoni mwangu kwa kujali hatma ya Taifa letu, tusifanye majaribio jamani.
 
Back
Top Bottom