Uamsho Vs Serikali

Uamsho Vs Serikali

abdul 28

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2012
Posts
325
Reaction score
38
Tukumbuke kuwa katika uchaguzi wa 2001 jumuia ya Uamsho ilikuwa ni mawakala (observers) wa Marekani kusimamia uchaguzi na waliwakushanyia report na takuwimu za Uamsho na zawangalizi wengine wa kimataifa zililingana ZANZIBAR. Sasa kumwambia Marekani /western kuwa Uamsho ni tishio kwa dunia yani ni magaidi hili nikujidanganya wahafidhina, maana huwezi kuwafananicha Uamsho na makundi haramu ya ugaidi kama Buharamu au Al Qaida it is fareway.

Uamsho imesajiliwa kihalali na Serekali ya Mapinduzi ya watu wa Zanzibar ambayo ina %99 ya wananchi wake ni waislamu, na maadai ya Uamsho hayahusu mizozo ya kidini maana wananchi wake ni waislamu assilia hio. Kwa hio hakuna mivutano hapa kwetu Zanzibar ya Kidini tokea enzi hio, sera za uamsho ziko wazi na zinakubaliwa na wananchi wa Zanzibar katika kutetea na kudai haki na usawa wa nchi yetu na viongozi wetu wa smz chini ya Muungano ndio walengwa.

Laakini kwa zichukuwa Taka taka zao zenye kunuka kuzizika uani kwao basi wanataka kuzisukumiza kwengine, ndio hutafuta msada wa kufanya kama zanzibar nako kuna ugaidi ndio hukerwa na Ndevu, Majina ya Allah, viguo vifupi,etc. Ndio ukaona huwatuma vijana wao wa Uvccm Janjawi waliowapa Mafunzo ya Udundu na kuwalicha sumu za Ubaguzi wachome Makanisa ,waibe na wavunje Bar ili wapate mwanya wazanzibar ya leo kila mtu ana simu ya mchina haaaaaa habari mpaka za giningi zinapatikana seuze za uamshoo hehee mchina ukitaka habari za space utazipata njia pekee ya kuzuia uamsho ni kuzuiya kampuni za simu zisitoe GB za internent lakini hii ni bure sababu watu watapogiana simu.

CCM tizameni nini uamsho wanakidai ikilchobaki ccm magamba mubadilishe sera ili ziendane na matakwa ya watu sera za CCM za sasa ni sera za STALIN NA LENEN wa russia ya enzi hizo kukamata watu kuuwa watu kunyowa watu ngozi za kichwa kuchoma makanisa kuchoma bar huu ni upuuzi wa kimagamba sasa kitu cha msingi ccm fikirieni njia na sera nzuri za kudumisha muungano uwe wa kiuchumi kijamii na uweze kukabiliana na mawazo ya wakati wahafithina wako ulimwengu wa kaburini wenyewe wako haii wanatembeekuipaka matope Jumuki .


 
Nawaleteeni barua ya UAMSHO kwenda SMZ kulalamika kunyanyaswa. Naileta kama ilivyo mjisomee wenyewe.

JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU
(JUMIKI)
للجنة الدعوة الإسلامية
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
P. O. BOX: 1266 -Tel: +255-777-419473 / 434145-
FAX +255-024-2250022 E-Mail: jumiki@hotmail.com
MKUNAZINI ZANZIBAR

Ref. JMK/VOL/12/2012 01 Novemba, 2012

KWA;

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA
ZANZIBAR.

KWA;

KAMISHNA WA JESHI LA POLISI
ZANZIBAR

KWA;

KAMISHNA WA VYUO VYA MAFUNZO
ZANZIBAR

KUH: UVUNJWAJI WA SHERIA ZA NCHI UNAOFANYWA NA JESHI LA POLISI NA VIKOSI VYA SMZ.

Tafadhali husika na somo la hapo juu kama linavyo someka.

Kila sifa njema zinamstahikia Allah (S.W.T), rehma na amani zimuendee Mtume Muhammad (S.A.W), ahli zake, masahaba zake na waliowema katika Uislamu.

Jumuiya ya UAMSHO inaleta masikitiko yake juu ya uvunjwaji wa sheria za nchi unaofanywa na jeshi la Polisi wakishirikiana na baadhi ya viongozi wa SMZ kama kuteremsha na kuzichana bendera za jumuia ya UAMSHO, bendera ambazo zina jina tukufu la LAA ILAAHA ILLA LLAAH MUAHAMMADUN RASUULULLAAH, jumuia ambayo imesajiliwa na Serikali chini ya sheria ya taasisi zisizo za kiserikali ya mwaka 1995, ung’olewaji wa milingoti yenye kubeba bendera hizo, kuyang’oa mabango yenye nembo za UAMSHO ikiwemo ofisi ya kamati ya Mihadhara Mwanakwerekwe, kupigwa kwa wananchi kila siku katika maeneo tofauti ya Zanzibar wengine huumizwa vibaya na wengine kuuliwa, kuvunjiwa majumba yao na kuibiwa, kuvunjiwa vitu vyao ndani ya majumba yao. Jambo la kusikitisha hakuna taasisi yoyote inayolalamikia unyama huu na udhalilishwaji wanaofanyiwa raia madhlum wasionahatia. Jee huu ndio utawala bora wenye kuzingatia sheria na haki za wananchi?

Leo tunashuhudia uvunjwaji wa sheria za mahabusu (Washtumiwa) kwa kuzuiliwa kupelekewa chakula, nguo, na kuwanyoa ndevu hali ya kua bado wao ni watuhumiwa nao ni Amir wa Jumuia ya Maimamu Zanzibar Sh. Farid Hadi, Amir wa UAMSHO Sh. Msellem Ally, Sh. Azzan Khalid, Sh. Khamis Ali, Hassan Bakari, Ghalib na wengineo, jee hizi ndio taratibu za kimahkama kabla ya mtuhumiwa kupatikana na kosa la kujibu?!!!!

Baadhi ya viongozi wa Serikali ya SMZ wanaotumia madaraka yao vibaya wamepeleka taarifa ya kuzuia vyombo vya habari vyote hapa Zanzibar kutangaza habari za jumuia huu ni uvunjwaji wa haki ya kutoa na kupata habari vilivyomo ndani ya katiba ya Zanzibar.

Kumbuka katika kikao kilichofanyika ofisini kwako baina ya mkurugenzi wa mashtaka na jumuiya ya UAMSHO cha tarehe 10-10-2012 wewe ukiwa mwenyekiti tulihudhuria sisi na jeshi la Polisi mwisho wa kikao chetu tulikubaliana kwamba tubadilike kwa kufuata sheria ya nchi na kulinda amani ya nchi.

Tunatanabahisha kuhusu uadui unaooteshwa baina ya jeshi la polisi wakishirikiana na vikosi kwa upande mwengine ni madhluum rai wasio na hatia…

Jee huu ndio ulinzi wa Raia na mali zao unaofanywa na vikosi pamoja na jeshi la polisi…?
Ni muhimu kuzingatia kuwa ulikuwa hupo na leo upo na utaondoka muda ukifika INSHA-ALLAH kama waliopita walio kutangulia. Na ALLAH atakwenda kukuuliza kwa kila tendo ulilolitenda na ulilolizungumzan mbele ya hakimu wa mahakimu Muadilifu ambaye ni ALLAH(S.W).

Ni mategemeo yetu kupata mashirikianao mazuri kutoka kwako.

Shukran.

………………….
KATIBU MKUU.
JUMUIYA YA UAMSHO.

NAKLA;
MWANASHERIA MKUU- ZANZIBAR
MKURUGENZI WA MASHTAKA ZANZIBAR
VYOMBO VYA HABARI.
WAISLAMU.
 
1.uamsho hawafanani na al-qaeda au boko haram ILA BOKO HARAM LILIANZA KAMA UAMSHO

2.UAMSHO ni kundi la kidini ILA KUMBUKA KWA SASA LINAFANYA SIASA na kuiweka dini pembeni

3.uamso ichague kufanya siasa na kuomba usajili kama chama cha siasa-hii itawalazimu viongozi wake wabadilike na kusimikwa viongozi wenye ELIMU DUNIA na sii elimu ahera.

4.Uamsho kwa kukosa viongozi makini walitumia mbinu za KIGAIDI ili kuleta vurugu zenji.FARID eti alitekwa na hata kibao hakupigwa.huu ni uongo tunavyoijua nchii hii jamaa angerudi na maumivu tele.FARID aliibuka kutoka mafichoni kabla ya deadline ya masaa waliyotoa uamsho serikalini nia NI KUWAONESHA WAFUASI WAKE KUWA SERIKALI INAMWOGOPA IMEMWACHILIA. serikali sasa imeamua kuuonesha ulimwweng kuwa farid ni ndulele

5.NAIPONGEZA SERIKALI YA CCM KWA NAMNA ILIVYOAMUA KUPAMBANA NA UAMSHO NA PONDA ila inggekuwa rahisi sana LOWASSA angekuwa rais angetoa amri moja tu. nayo ni risasi mmoja maiti mmoja kisha dumbukiza maiti baharini
 
Tukumbuke kuwa katika uchaguzi wa 2001 jumuia ya Uamsho ilikuwa ni mawakala (observers) wa Marekani kusimamia uchaguzi na waliwakushanyia report na takuwimu za Uamsho na zawangalizi wengine wa kimataifa zililingana ZANZIBAR
Sasa kumwambia Marekani /western kuwa Uamsho ni tishio kwa dunia yani ni magaidi hili nikujidanganya wahafidhina, maana huwezi kuwafananicha Uamsho na makundi haramu ya ugaidi kama Buharamu au Al Qaida it is fareway.
Uamsho imesajiliwa kihalali na Serekali ya Mapinduzi ya watu wa Zanzibar ambayo ina %99 ya wananchi wake ni waislamu, na maadai ya Uamsho hayahusu mizozo ya kidini maana wananchi wake ni waislamu assilia hio.
Kwa hio hakuna mivutano hapa kwetu Zanzibar ya Kidini tokea enzi hio, sera za uamsho ziko wazi na zinakubaliwa na wananchi wa Zanzibar katika kutetea na kudai haki na usawa wa nchi yetu na viongozi wetu wa smz chini ya Muungano ndio walengwa.
Laakini kwa zichukuwa Taka taka zao zenye kunuka kuzizika uani kwao basi wanataka kuzisukumiza kwengine, ndio hutafuta msada wa kufanya kama zanzibar nako kuna ugaidi ndio hukerwa na Ndevu, Majina ya Allah, viguo vifupi,etc.
Ndio ukaona huwatuma vijana wao wa Uvccm Janjawi waliowapa Mafunzo ya Udundu na kuwalicha sumu za Ubaguzi wachome Makanisa ,waibe na wavunje Bar ili wapate mwanya wazanzibar ya leo kila mtu ana simu ya mchina haaaaaa habari mpaka za giningi zinapatikana seuze za uamshoo hehee mchina ukitaka habari za space utazipata
njia pekee ya kuzuia uamsho ni kuzuiya kampuni za simu zisitoe GB za internent lakini hii ni bure sababu watu watapogiana simu ccm tizameni nini uamsho wanakidai ikilchobaki ccm magamba mubadilishe sera ili ziendane na matakwa ya watu
sera za CCM za sasa ni sera za STALIN NA LENEN wa russia ya enzi hizo kukamata watu kuuwa watu kunyowa watu ngozi za kichwa kuchoma makanisa kuchoma bar huu ni upuuzi wa kimagamba
sasa kitu cha msingi ccm fikirieni njia na sera nzuri za kudumisha muungano uwe wa kiuchumi kijamii na uweze kukabiliana na mawazo ya wakati
wahafithina wako ulimwengu wa kaburini wenyewe wako haii wanatembeekuipaka matope Jumuki .



Kahawa drinkers' gossips
 
Hapa inatafutwa choko choko ya kuanzisha varangati upyaa huko zenji, ngoja tusubiri
 
Kwani Sheick Msellem Ali Msellem naye alikuwa na ndevu?
 
Ni kweli walisajiliwa kwa mjibu wa sheria, na kupewa masharti na kuelezea matakwa na maksudi ya chama, sasa kama wanakwenda kinyume lazima wabanwe tena kitendo cha kusema Allah atakuja kumuuliza mi inanichefua saana, kwa sababu huyo Allah anaangalia wanao wabana tu, ila wao wanapoua , wanapochoma makanisa na kuiba Allah anawabariki na hata wauliza, Uamsho waache Choko Choko wajue Allah pia atawauliza pia
 
JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU
(JUMIKI)
للجنة الدعوة الإسلامية
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
P. O. BOX: 1266 -Tel: +255-777-419473 / 434145-
FAX +255-024-2250022 E-Mail: jumiki@hotmail.com
MKUNAZINI ZANZIBAR
.

'MOBILISATION AND PROPAGATION????

Uamsho walijisajili kama jumuiya inayohusika na mambo ya dini za kiislam. Sasa ilikuwaje wakaingia kwenye siasa? Au ndio 'Mobilisation and Progation yenyewe?
 
wasipojibiwa itakuwaje!! kwa sababu wakija mabarabarani imepaswa watushawishi kuwa wanachokiingilia barabarani kina uzito wa kuwaalika watu majiani. ene wei kila la kheri kwenye kuikataa ccm.
 
'MOBILISATION AND PROPAGATION????

Uamsho walijisajili kama jumuiya inayohusika na mambo ya dini za kiislam. Sasa ilikuwaje wakaingia kwenye siasa? Au ndio 'Mobilisation and Progation yenyewe?

Wewe hufahamu na inaonesha wewe ni numb.naomba nikueleweshe chanzo cha migogoro hyo ni katiba mpya ambayo suala nyeti la muungano ndo source ya yote hayo.ccm kama kawaida wanataka serkali mbili kwenda moja na wanzanzibar wengi wao wanataka tatu,tatanganyika wamebakia walio wengi ni non-alliened.kwa hyo basi kama uamsho imesajiliwa kisheria ina haki pia kuongelea mambo yote ya kisiasa kwa sababu siasa ipo ndani ya jamii na ndo maana jaji warioba amesema makundi yote atayapitia ili kupata maoni yao juu yakatiba mpya yakiwemo wabunge,vikundi vya kidini,hata makundi ya rika tofauti.
 
Wewe hufahamu na inaonesha wewe ni numb.naomba nikueleweshe chanzo cha migogoro hyo ni katiba mpya ambayo suala nyeti la muungano ndo source ya yote hayo.ccm kama kawaida wanataka serkali mbili kwenda moja na wanzanzibar wengi wao wanataka tatu,tatanganyika wamebakia walio wengi ni non-alliened.kwa hyo basi kama uamsho imesajiliwa kisheria ina haki pia kuongelea mambo yote ya kisiasa kwa sababu siasa ipo ndani ya jamii na ndo maana jaji warioba amesema makundi yote atayapitia ili kupata maoni yao juu yakatiba mpya yakiwemo wabunge,vikundi vya kidini,hata makundi ya rika tofauti.


Hawa wamechoka Amani. Kwa nini sasa wana taka wanyolewe Ndefu wakati walikuwa wanaziona ni fahari?
Waache ujinga
 
mie napita tu hapa wangojeni wana uamsho waingie ndani....muelewane vizuri...
 
Vipi Pombe walizoiba na kunywa na pia mji wote wa Magharibi kwa chupa za bia, je Muhindi wa watu mtamlipa?
 
wanajamii wenzangu hapa ni ukumbi wa magreat thinkers, hebu kwa muda tutafakari mawili matatu juu ya kadhia hii ya Uamsho na yanayotokea zanzibar.

mm nnaamini kua UAMSHO walijisahau, walilewa ule umma unaohudhuria kwenye mikutano yao, wakashindwa kutumia busara na hekima za kudai haki zao. nimesikiliza sana CD zao nimeona wana madai ya msingi, madai yao ni madai ya wazanzibari walio wengi. hili halina ubishi.

uamsho walichokosea ni kulewa sifa, baada ya kutumia hekima na busara za kudai zanzibar huru, kwa kuwashirikisha watu wote bila kujali masuali ya dini zao, wakaonyesha wazi kabisa kuwa wao wanadai kwa misingi ya kidini na adui yao mkubwa ni makafiri (maana wakristo na kanisa) akiwemo nyerere. ubaguzi huu umewagharimu sana.

uamsho walifika pahali kuitisha serikali, walikuwa wakitoa matamko ya kutaka kuonyesha wanaweza kuiamuuru serikali kufanya wanavyotaka wao. huenda sheria zinaelekeza kupata haki wanazodai ili kufanya mikutano au mengineyo, lkn busara na kuelimisha ndio kazi ya mwanaharakati hadi afikie lengo lake.

ndugu zangu hawa ambao bila kutafuna maneno nnapenda harakati zao za kudai nchi yetu, ila sikubaliani na mwenendo waliokuwa wakienda nao, walijitengenezea maadui wengi kwa kujitakia. waliwajenga vijana kuwa na kiburi badala ya uimara wa hoja. walisahau kupima madhara ya baadhi ya kauli zao.

siku zote mwanaharakati mzuri ni yule ambae anapambana kudai haki zake, na kujitahidi kupunguza madhara kadri inavyowezekana. UAMSHO walishindwa kukemea kwa kauli moja na kuonyesha kuwa wao hawapendi vijana wao wajihusishe na uharibifu wa nchi yao

hata hivyo, nnalaani sana kwa serikali nao kukiuka katiba na kwenda kinyume na haki za binaadamu. UAMSHO ni raia wa nchi yetu, wanapaswa kuhukumiwa na kufanyiwa mambo yao kwa kufata sheria za nchi. kama watuhumiwa, wanapaswa wapewe haki zote kama zilivyoainishwa na sheria. na wafuasi wao waheshimiwe kama raia wengine. mwenye makosa ahukumiwe kwa mujibu wa kosa lake. utawala bora hauna maana kua mkosaji wa makosa fulani sheria zisifatwe.
UAMSHO WASIPENDELEWE ILA WASIONEWE
 
1.uamsho hawafanani na al-qaeda au boko haram ILA BOKO HARAM LILIANZA KAMA UAMSHO

2.UAMSHO ni kundi la kidini ILA KUMBUKA KWA SASA LINAFANYA SIASA na kuiweka dini pembeni

3.uamso ichague kufanya siasa na kuomba usajili kama chama cha siasa-hii itawalazimu viongozi wake wabadilike na kusimikwa viongozi wenye ELIMU DUNIA na sii elimu ahera.

4.Uamsho kwa kukosa viongozi makini walitumia mbinu za KIGAIDI ili kuleta vurugu zenji.FARID eti alitekwa na hata kibao hakupigwa.huu ni uongo tunavyoijua nchii hii jamaa angerudi na maumivu tele.FARID aliibuka kutoka mafichoni kabla ya deadline ya masaa waliyotoa uamsho serikalini nia NI KUWAONESHA WAFUASI WAKE KUWA SERIKALI INAMWOGOPA IMEMWACHILIA. serikali sasa imeamua kuuonesha ulimwweng kuwa farid ni ndulele

5.NAIPONGEZA SERIKALI YA CCM KWA NAMNA ILIVYOAMUA KUPAMBANA NA UAMSHO NA PONDA ila inggekuwa rahisi sana LOWASSA angekuwa rais angetoa amri moja tu. nayo ni risasi mmoja maiti mmoja kisha dumbukiza maiti baharini

umeweka points zako kutoka kinywani mwako bila ushahidi wowote.


Msikilize huyu padri anasema nini

Na Lilian Nyenza

Kanisa halitaacha kutoa mwongozo kwa watu wake hata kwa mambo ya kisiasa ukiwamo uchaguzi kwa kuwa, siasa bila dini ni sawa na uendawazimu.

Aidha, imedaiwa kuwa tabia ya kuwalaghai vijana kuwa ni taifa la kesho, ndiyo inayowadumaza kiakili na kuwafanya watumiwe na wanasiasa kufanya fujo, badala ya kujitokeza kuongoza kwa kufuata taratibu za nchi.

Mkurugenzi wa chama cha kifamilia cha Undugu Association Tanzania, Padri Baptiste Mapunda, alitoa kauli hiyo katika sherehe za kuuaga mwaka 2004 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2005, zilizofanyika katika ukumbi wa Parokia ya Mt. Yosefu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo wa UNDUGU ASSOCIATION TANZANIA alisema kuwa, Tanzania imeanza kuonesha dalili mbaya za machafuko kutokana na baadhi ya watu wakiwamo wanasiasa kuweka mbele ubinafsi.

“Tukikaa kimya huku mambo yanaharibika katika jamii; eti tuwaachie wanasiasa wafanye watakavyo, tutakuwa hatutendi wajibu wetu na hivyo, Kanisa halitaacha kusema ukweli kwa maslahi ya umma hata kama unamkera mtu.

Hii ni kwa kuwa tunajua wazi kuwa siasa bila dini, ni uendawazimu ambao mtu hajui akifanyacho kwa kuwa akili yake haijatimia kiroho.” alisema.
Aliitaka jamiii ya Kitanzania ijifunze thamani ya amani na siasa safi kutokana na hali ya amani na usalama katika nchi jirani za Rwanda na Burundi ambayo ni hatari na inasikitisha.

Alisema vita na mauaji yanayoendelea katika nchi hizo, yanasababishwa na uroho wa madaraka wa watu wachache ambao hawajali utu wa wengine.

Aliongeza kuwa, “Siku zote tunapaswa kukumbuka kuwa, amani na mapendo ambayo Mungu ametujalia, tunapaswa kuyaenzi sisi sote kwa kuwa siasa bila dini, ni sawa na uendawazimu.”

Padri Mapunda aliiasa jamii kuendelea kumuomba Mungu ili azidi kuwajalia amani,upendo na utulivu uliopo sasa, kuwa uwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu kupita.

Amewataka Waamini kuwaombea viongozi wanyanyasaji kama Herode, wabadilike na hivyo, kuongoza nchi kwa haki na akawasihi Watanzania kuyashinda maovu kwa kutenda yaliyo mema.

Hata hivyo, Padri Mapunda amewatahadharisha vijana kujiepusha kutumiwa na baadhi ya viongozi wa siasa, kwa nia ya kufanya fujo katika uchaguzi.

“Vijana mara nyingi wamekuwa wepesi wa kurubuniwa na vijizawadi vidogo vidogo, ili wafanye kile wanachokitaka wanasiasa wabinafsi. Sasa mimi nasema mkae chini na mlitafakari hilo kwa makini.

Mtakao angamia ni ninyi na si wao,” alitahadharisha.

Alisema vijana ni Taifa la leo na Taifa bila vijana limekufa, hivyo aliwasihi kuwaheshimu wazazi na walezi ili wapate kuishi maisha marefu na yenye heri duniani, kama walivyojaliwa kuuona mwaka huu mpya.

Naye Mwenyekiti wa Umoja huo, Bw. Benjamini Komba alisema, lengo la Shirika la Undugu, ni kuiunganisha jamii, ikiwa ni pamoja na kuimarisha Ukristo katika kupata hamasa katika kazi ya umisionari, ili ijengeke roho ya umisionari wa kweli nchini Tanzania.

Bw. Komba alisema kuwa, Shirika limekuwa na mchango mkubwa kwa jamii, kwa kuwa ni chombo cha kuelimisha jamii na kuendeleza mawasiliano na wamisionari wa Afrika ambao wapo ndani na nje ya nchi kwa lengo la kusukuma mbele kurudumu la Injili katika Taifa hili.

Umoja huo haujishughulishi na mambo ya siasa na hauna ubaguzi wa dini, rangi, imani wala itikadi.
Katika sherehe hizo, Wanaundugu na watu wengine walialikwa na kuhudhuria pamoja na familia zao.
 
umeweka points zako kutoka kinywani mwako bila ushahidi wowote.


Msikilize huyu padri anasema nini

Na Lilian Nyenza

Kanisa halitaacha kutoa mwongozo kwa watu wake hata kwa mambo ya kisiasa ukiwamo uchaguzi kwa kuwa, siasa bila dini ni sawa na uendawazimu.

Aidha, imedaiwa kuwa tabia ya kuwalaghai vijana kuwa ni taifa la kesho, ndiyo inayowadumaza kiakili na kuwafanya watumiwe na wanasiasa kufanya fujo, badala ya kujitokeza kuongoza kwa kufuata taratibu za nchi.

Mkurugenzi wa chama cha kifamilia cha Undugu Association Tanzania, Padri Baptiste Mapunda, alitoa kauli hiyo katika sherehe za kuuaga mwaka 2004 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2005, zilizofanyika katika ukumbi wa Parokia ya Mt. Yosefu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo wa UNDUGU ASSOCIATION TANZANIA alisema kuwa, Tanzania imeanza kuonesha dalili mbaya za machafuko kutokana na baadhi ya watu wakiwamo wanasiasa kuweka mbele ubinafsi.

"Tukikaa kimya huku mambo yanaharibika katika jamii; eti tuwaachie wanasiasa wafanye watakavyo, tutakuwa hatutendi wajibu wetu na hivyo, Kanisa halitaacha kusema ukweli kwa maslahi ya umma hata kama unamkera mtu.

Hii ni kwa kuwa tunajua wazi kuwa siasa bila dini, ni uendawazimu ambao mtu hajui akifanyacho kwa kuwa akili yake haijatimia kiroho." alisema.
Aliitaka jamiii ya Kitanzania ijifunze thamani ya amani na siasa safi kutokana na hali ya amani na usalama katika nchi jirani za Rwanda na Burundi ambayo ni hatari na inasikitisha.

Alisema vita na mauaji yanayoendelea katika nchi hizo, yanasababishwa na uroho wa madaraka wa watu wachache ambao hawajali utu wa wengine.

Aliongeza kuwa, "Siku zote tunapaswa kukumbuka kuwa, amani na mapendo ambayo Mungu ametujalia, tunapaswa kuyaenzi sisi sote kwa kuwa siasa bila dini, ni sawa na uendawazimu."

Padri Mapunda aliiasa jamii kuendelea kumuomba Mungu ili azidi kuwajalia amani,upendo na utulivu uliopo sasa, kuwa uwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu kupita.

Amewataka Waamini kuwaombea viongozi wanyanyasaji kama Herode, wabadilike na hivyo, kuongoza nchi kwa haki na akawasihi Watanzania kuyashinda maovu kwa kutenda yaliyo mema.

Hata hivyo, Padri Mapunda amewatahadharisha vijana kujiepusha kutumiwa na baadhi ya viongozi wa siasa, kwa nia ya kufanya fujo katika uchaguzi.

"Vijana mara nyingi wamekuwa wepesi wa kurubuniwa na vijizawadi vidogo vidogo, ili wafanye kile wanachokitaka wanasiasa wabinafsi. Sasa mimi nasema mkae chini na mlitafakari hilo kwa makini.

Mtakao angamia ni ninyi na si wao," alitahadharisha.

Alisema vijana ni Taifa la leo na Taifa bila vijana limekufa, hivyo aliwasihi kuwaheshimu wazazi na walezi ili wapate kuishi maisha marefu na yenye heri duniani, kama walivyojaliwa kuuona mwaka huu mpya.

Naye Mwenyekiti wa Umoja huo, Bw. Benjamini Komba alisema, lengo la Shirika la Undugu, ni kuiunganisha jamii, ikiwa ni pamoja na kuimarisha Ukristo katika kupata hamasa katika kazi ya umisionari, ili ijengeke roho ya umisionari wa kweli nchini Tanzania.

Bw. Komba alisema kuwa, Shirika limekuwa na mchango mkubwa kwa jamii, kwa kuwa ni chombo cha kuelimisha jamii na kuendeleza mawasiliano na wamisionari wa Afrika ambao wapo ndani na nje ya nchi kwa lengo la kusukuma mbele kurudumu la Injili katika Taifa hili.

Umoja huo haujishughulishi na mambo ya siasa na hauna ubaguzi wa dini, rangi, imani wala itikadi.
Katika sherehe hizo, Wanaundugu na watu wengine walialikwa na kuhudhuria pamoja na familia zao.

Huu ni msumari wa mwisho kwa wanaopinga UAMSHO KUJIHUSISHA NA SIASA hata kiongozi wa UAMSHO sheikh MSELLEM ALLY alisema huwezi tenganisha dini na siasa kwasababu dini ya kiislamu ni dini iliyokamilika katika masuala yoteya maisha ya mwanadamu kuanzia kwenye hukumu mpaka kwenye biashara
 
Back
Top Bottom