Uamsho Vs Serikali

Uamsho Vs Serikali

Kamwewe nimekukubali, kwa kweli kuna mkanganyiko mkubwa sana linapokuja swala la kutenganisha dini na siasa. DINI NA SIASA HAVITENGANI. Kama kuna mtu anawadanganya watu kuvitenganisha basi ana malengo yake. LABDA KAMA NI MBUMBUMBU asiyeijua dini yake. Siasa ni tawi la DINI.
 
'MOBILISATION AND PROPAGATION????

Uamsho walijisajili kama jumuiya inayohusika na mambo ya dini za kiislam. Sasa ilikuwaje wakaingia kwenye siasa? Au ndio 'Mobilisation and Progation yenyewe?

Uislamu ni mfumo kamili wa maisha ikiwa ni pamoja na matendo na maneno yanayofanyika (Ukifanya baya utalipwa Ubaya na ukitenda jema utalipwa wema). Je SIASA haimo katika maisha? Siasa ni moja kati ya parts za harakati ndani ya Uislamu lakini inategemea na jinsi utakavyoipreach. Ili kuhalalalisha maelezo yako kwanza ulitakiwa uje na suali, je UAMSHO wanafanya SIASA ya aina gani?
 
Ni kweli walisajiliwa kwa mjibu wa sheria, na kupewa masharti na kuelezea matakwa na maksudi ya chama, sasa kama wanakwenda kinyume lazima wabanwe tena kitendo cha kusema Allah atakuja kumuuliza mi inanichefua saana, kwa sababu huyo Allah anaangalia wanao wabana tu, ila wao wanapoua , wanapochoma makanisa na kuiba Allah anawabariki na hata wauliza, Uamsho waache Choko Choko wajue Allah pia atawauliza pia

Wewe unaweza kutupatia ushahidi kama UAMSHO wamechoma Makanisa coz Serikali ya Mapinduzi ilishindwa na hata ilipotakiwa iunde Tume kuchunguza walichokurupuka kukitoa walishindwa kufanya hivyo sababu walingundua kama Makanisa waliyachoma 'Wenyewe' kwa lengo lisilofahamika!
 
what were you trying to say?

Ni muhimu kuzingatia kuwa ulikuwa hupo na leo upo na utaondoka muda ukifika INSHA-ALLAH kama waliopita walio kutangulia. Na ALLAH atakwenda kukuuliza kwa kila tendo ulilolitenda na ulilolizungumzan mbele ya hakimu wa mahakimu Muadilifu ambaye ni ALLAH(S.W).
 
Haya yote ni moja ya kero za muungano wenu. Kwani wanaofanya haya wanapata amri toka upande wa pili wa muungano wenu na wanafanya hivyo ili kuleta fitna na chuki na mfomo usio sahihi kabisa kwa mila, desturi na sirka za waZnz na Znz kijumla.

kama waZnz waliweza kukaa kitako wenyewe na kuamua mustakabali wa amani ya nchi yao kuanzisha GNU na hili waachiwe wenyewe sio kukubali kuvamiwa na kuongozwa na mamluki kutoka Tanganyika.

Nasisitiza na kusema NI vizuri KUHISHIMIANA na SIO KUVUMILIANA.

Wa Znz liangalieni hilo kwani nia za wenzenu si njema kwenu na wanaingia kwa kisingizio cha Mvungano wenu.
 
Back
Top Bottom