Ualimu vs upolisi ngazi ya degree. Naomba ushauri.

NAJUA UNACHUKUA EDUCATION MUCCoBS,NENDA KAPOKEE TAKE HOME 385,000/-,MWENZIO AKACHUKUE 685,000/,ALAFU WEWE NDIYE KICHWA MAJI UNAEKUBALIANA NA KUPATA KAMSHAHARA KIDUCHU
Sisomi muccobs mr acha kujamba jamba
 
hamna mzembe wewe then ushahama kule mchamba wima
hesabu ipo hivi ukiingia na certoficate police/jwtz,unapewa ukoplo ,mshahara wa ukoplo police ni 300,000/-,take home ni 240,000/- +150,000/- =390,000/,tuje jeshi mshahara koplo ni kama 500,000/- take hom ni kama 400,000/- +300,000/-(posho)= 700,000/-,mwalimu degree 3
85,000/-
 
jamani jamani kazi ni kazi inategemea na wewe unaiboreshaje ili ikufae.
to me as mwl kwanza kabisa nimeridhika sana na kazi yangu ni nzuri na namshukuru sana alinipa baraka zake imenipa exposure nzuri sana, na hata leo nikidondosha salary slip yangu waweza kufikir nafanya kazi kama mtu tofauti si mwl kwani zero zake zimesonga sana tu.

tatizo kubwa la waalim wa kitanzania tunafikir ualim ni kufundisha darasan na tuition tu kumbe sio hivyo, unaweza kuuweka kama boya ambapo asbh unaamka unakwenda unapiga mzigo unatoka mchana unapiga kazi nyingine kama kilimo na biashara. maisha ya vijijin waalim wengi ndio wakulima wakubwa tena wenye vipato vizuri na kwa hapa mjini waalim wajanja ndo wano pata vikazi vya kufacilitate so hukai ofsn tena kama ni wa science wewe kila siku uko mikoan unafacilitate na kulamba per diem zao.

ushauri wangu fanya kazi ambayo moyo wako aunaipenda kama wapenda ualim basi fanya na kama wapenda upolis nenda usiwe mtu wa sitak nataka.
 
Kaka mi ni mwalimu mwaka wa 5 diploma hakuna cha kupanda madaraja wala nn?NIMEFUATILIA ISHU YA POLISI KAMA MARA 3 NAKOSA SASA NIMEKATA TAMAA,NAKUOMBA SANA KAKA NENDA UPOLISI UNALIPA KINOMA TOFAUT NA UALIMU MIZINGUO MIZINGUO NENDA POLISI......Ulipateje pateje hyo ishu maana miaka wanasema 25 mwisho?jaman kaka nakuombea kafanye interview mungu akusaidie upate
Nafasi zilitangazwa kwa graduates wa 2012 tu. Nashukuru kwa ushauri na usaili umeanza leo.



Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Samiti na samrich mtatoana macho. Najali sana hoja zenu kuliko madongo mnayotupiana. nazidi kushukuru kwa wote mnaochangia kwani naamini mnatusaidia wengi na ni kwa manufaa yetu sote.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Huyu samrich anasomea education sasaa anaona ukweli unazidi analeta lugha chafu uwezo mdogo wa kufikiri 1.5kb
 
Nashukuru sana mods kwa kumpiga ban huyu binti samrich haiwezekani uambiwe ukweli uchukiee
 
Nashukuru sana mods kwa kumpiga ban huyu binti samrich haiwezekani uambiwe ukweli uchukiee

Mtu kashachezea ban hapahapa duh! Kweli tunatofautiana.
Je upimaji afya wa police wanapima vitu gani?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Asante mkuu unajua linapokuja swala la kazi sio kukurupuka hivyo nilihitaji kujua na kutoka kwa watu wengine. Wacha nikapambane huko degree itanifaa baadae niwe optimist tu. Ntaamkia kwa mtendaji aniandikie hiyo barua maslahi huku afadhali. Ina maana hata kwa degree kuna uwezekano wa kupangiwa lindo bank na kupiga patrol mitaani?


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

umeambiwa na jamaa hapo juu maslahi safi kuliko mwalimu lakini kazi inakutaka uwe mvumilivu. Jeshi la polisi tofauti sana na jeshi la wananchi. kwanza promotion ni baada ya miaka 3 hadi minne, na sio lazima, itategemea na nidham na kujituma kwako.

Kwenye red ndo kazi haswa za askari polisi. Hivyo utalinda benk, utamlinda jaji, utafanya doria mtaani, utatoa elimu ya polisi jamii na ulinzi shirikishi, na baadaye wanaweza kukuweka kwenye kazi za kiutawala. Ukisha zijua kazi zile za ulinzi, ndipo utakapokuwa kiongozi mzuri hapo mbeleni.

Askari polisi ni mlinzi, hadi IJP ni mlinzi, na nadhani anafanya doria kubwa zaidi kuliko askari mdogo. Hana muda wa kulala, hana muda wa kupumzika hana raha na kazi yake, kwani kuwa askari itakuhitaji kuwa mvumilivu kwelikweli, ukiwa na moyo mwepesi, iache kazi hii haitakufaa. Lakini kama kweli unapenda kubadili utendaji ndani ya jeshi, vumilia yote ipo siku utakuwa sehem ya maamuzi mazito ya jeshi.
 
Wanapima urefu,hiv,usiwe na ulemavu,kama ni mwanaume jogoo wanaangalia kama anawika,
 
unafikiri huko kuhama hama kwenyewe utakuwa unapelekwa mjini tu? raha ya maisha ni kutulia labda kama utaoa/kuolewa na jobless mtakuwa mnahama wote lakini vinginevyo itakubidi umuache mke/mume somewhere c'se hakuna mwajiri anayeweza kukubali hizi karaha za kufuata familia. Pia utawaathiri watoto kielimu kwa kuwahamishahamisha

ukiondoa ishu ya kuhamishwahamishwa! polisi ina unafuu wowote kuzidi ualimu?
 
Kaka mi ni mwalimu mwaka wa 5 diploma hakuna cha kupanda madaraja wala nn?NIMEFUATILIA ISHU YA POLISI KAMA MARA 3 NAKOSA SASA NIMEKATA TAMAA,NAKUOMBA SANA KAKA NENDA UPOLISI UNALIPA KINOMA TOFAUT NA UALIMU MIZINGUO MIZINGUO NENDA POLISI......Ulipateje pateje hyo ishu maana miaka wanasema 25 mwisho?jaman kaka nakuombea kafanye interview mungu akusaidie upate
Kazi mbaya kama unayo.Hata ukienda huko polisi nakuhakikishia hautakaa uridhike. Kutokana na majukumu yanavobana na kukosa uhuru utautamani ualimu tena. Mie naona hiyo tofauti ya mshahara sio kubwa sana...Ni bora ufikirie mara mbili kutafuta kazi/biashara itakayokukomboa.
 
Liwalo na liwe kaa hon pinda. Kitaeleweka mbele ya safari mii najitosa tu.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
liwalo na liwe kaa hon pinda. Kitaeleweka mbele ya safari mii najitosa tu.

Sent from my blackberry 9800 using jamiiforums
sawawa assistant inspeca mtarajiwa lakini miguu **** ina uvunguu kama iko flat haina uvungu wanakutosaaa
 
komaa na fani ya ualimu, polisi ni hatari sana kwa maisha yako.. halafu utakuwa unahamishwa hamishwa kila mara na hivyo ni ngumu sana kujijenga kimaisha na kutulia na familia maana unaweza kupigwa transfer lindi baada ya miaka 2 unapigwa kibondo, mwaka unaofuata unapigwa loliondo, halafu ukiritimba wa huko ni balaa kama humjui mtu kwenye maswala ya kupanda cheo (nyota) na kuthaminiwa

Hayo ni mambo ya kupita tu! kwani kuna wangapi wanaofanya kazi onsite yaani wao leo uko bukoba kwa miezi 12 na wachina katika ujenzi wa barabara za Makufuri kesho kutwa anaenda Zanzibar kwenye mradi mwingine. Cha msingi tu wewe kuweka Base station yako ambapo utakuwa unapaendeleza kwa maisha ya baadaye. kingine kuhamahama si kama zamani coz serikali imeona cost kubwa kumhamisha mtu kwa muda mfupi tu kuna watu tangu nizaliwe yuko paleple mpka leo haohao police.
 
sawawa assistant inspeca mtarajiwa lakini miguu **** ina uvunguu kama iko flat haina uvungu wanakutosaaa

Uvungu upo mkuu bt I thot hiyo ni jwtz ndo wanakagua ama?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom