Kamati ya Maadili na usalama ya CCM imepokea na kujadili wana ccm 38 waliotia nia na kupeleka majina matano (5) Kamati kuu badala ya kupeleka majina yote na mapendekezo kama Katiba ya CCM inavyoagiza. Je huo ndio uadilifu wao? Pia kuna tetesi kuwa mchujo ulifanyika nje ya Kamati ya maadili na hivyo kukabidhiwa majina matano tu kufuata utaratibu. Je huo nao kama ni kweli ni uadilifu? Kama haya yalifanyika ni kweli kwa chama kongwe kama ccm je vyama vichanga viige nini kwake na ccm itabaki salama kwa dosari hizi katika karne hii ya siasa za vyama vingi? Nawasilisha kwa mjadala wanajamvi.