Hapana, labda nawe hujanielewa pia! Kufikiri tena kwa haraka pia ni akili, mi usingekometi kwangu, nilikuelewa kwamba, umeonesha uzembe kwa mamlaka husika, kwamba kibao kimeharibika wao hawajali, "kila siku napita hapo" kwahiyo kila siku unakiona, ukasimamisha gari na bado tu hujagundua kwamba kamsumali kameachia kweli?
Komenti yako sasa inanionesha kwamba, nawe kimakosa ungeweza kufanya kosa kama hilo, ndo maana umeona ni la kibinadamu. Hakuna anayeweza fanya hivyo, na ataikitokea lisingekaa masaa hapo. Hayapo kama urembo hapo, wapo hawazitumii alama ila wapo ambao wanazitumia sana.
Sori, inawezekana kweli ni mawazo ya kimasikini kweli, kwakuwa mimi ni masikini kweli, unadhani ningewazaje.. Ila kipi ni kipimo cha utajiri na umasikini? Mi nikiwa na furaha ndio utajiri wangu, sa Sijui wengine utajiri wao ukoje.