Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Leo nchi yetu tumepata mkopo wa 1.3 trilioni kutoka IMF (International Monetary Fund) tumefurahia sana watanzania na kupongeza sana kwa hatua hii
Lakini ukifuatilia sana mikopo hii, ambayo mabeberu wanasema eti ni mikopo ya masharti nafuu (concession loan) kutoka kwenye hizo taasisi za kifedha za kibeberu (Bretton woods institutions) haina historia nzuri sana kwa nchi zetu zinazoendelea (Developing countries)
Watatatukopesha sana kuwekeza kwenye miradi ya kuhdumia jamii, kama mashule, hospital, lakini baadaye mikopo hiyo huwa mikubwa sana na mzigo mkubwa kwa nchi zetu zinazoendelea
Mikopo ikiwa mikubwa sana na mzigo kwa nchi zetu, watatuambia tukae chini na kuandaa mipango ya kutupunguzia mzigo wa madeni (Debt relief)
Mpango huo wa kutupunguzia madeni, kwa kawaida huwa inaambatana na masharti magumu, ambayo kumsingi sio rafiki sana kwa maendeleo ya kiuchumi kwa nchi zetu, bali masharti hayo yatakuwa rafiki zaidi wa maendeleo ya kiuchumi ya nchi zao (mabeberu)
Kwa mfano kwenye miaka ya 1990, hizo taasisi za kibeberu (Bretton woods institutions) kama IMF, WORLD BANK, IDA nk, walikuja na mpango wa Structure Adjustments programs (SAP) ambapo moja ya masharti, walitutaka tuachie uchumi wetu (soko huria) ulioambatana na ubinafsishaji kwa mashirika na viwanda vyetu muhimu vya Kimkakati (Strategic companies& industries) ikiwa eti ni kupunguzia mzigo wa gharama za uendeshaji kwa serikali
Mabeberu walituambia eti hatuwezi kutumia fedha za walipa kodi wetu, kuyapa ruzuku (subsides) baadhi ya mashirika/ viwanda vyetu muhimu vya Kimkakati kwa uchumi na maendeleo ya nchi yetu
Nini kilitokea?
Baada ya masharti yao hayo, hatimaye mashirika/ viwanda vyetu vilishindwa kujiendesha kutokana na ushindani
na hatimaye viwanda/mashirika vyetu kufa
Nini kilitokea?
Baada ya mashirika/ viwanda hivyo kushindwa kujiendesha kwa kibiashara, walitokea wawekezaji wenye lengo la kunujua viwanda/ mashirika hayo kwa lengo la kuviendeleza
Lakini kwa bahati mbaya au kwa makusudi, viwanda na mashirika hayo muhimu kwa uchumi wa yetu yalikufa na ndio ukawa mwanzo wa nchi yetu kuwa soko la bidhaa zao kutoka kwenye viwanda vya nchi zao na washirika wao kitu ambacho kwa kiwango kikubwa sana kimechangia kuua ajira kwa nchi yetu
Lakiii very unfortunately, kwenye miaka ya 2000, uchumi wa nchi za kibeberu ulipata mtikisiko mkubwa (Economic recession)
Mfano mashirika na makampuni makubwa ya nchi ya Marekani tena makampuni binafsi (Public liabilities company) kama JP Morgan, Ford, Lehman Brothers, Godman and Sachs nk yalipata mtikisiko mkubwa wa kiuchumi
Lakini cha ajabu, serikali ya Marekani kwa kutumia fedha za wzlipa kodi, walitoa ruzuku kwa mashirika hayo binafsi ili kuyanusuru yasife, wakasema eti ts too big to fall
Kitu walichotukataza sisi kudanya, ndio exactly wao wanafanya kunusuru mashirika yao binafsi na uchumi wa nchi zao kwa ujumla, kwa sababu mashirika hayo yalikuwa ni msingi mkubwa wa ajira ndani ya nchi yao
Sasa leo tutakuwa ni watu wa ajabu sana na kushangaza, eti tukiamini kuwa taasisi hizo za kibeberu wanaweza kutupa msaada wa kuokoa uchumi wa nchi zetu, ambao umeathirika vibaya kutokana na janga hili la COVID-19
Mimi naamini, kama kweli walikuwa na lengo la kunusuru uchumi wa nchi zetu za Kiafrika, basi walipaswa kutusamee madeni yetu ya nyuma na si kutukopesha, kwa sababu nchi zetu hizi za kiafrika tunatumia peaa nyingi sana kila mwezi kuservice madeni yetu (Debt expenses) ambayo kimsingi kwa kiasi kikubwa madeni yetu hayo ni kutoka kwenye hizo Multilateral institutions
Waafrika tunapaswa kuwa pamoja, kushirikiana pamoja na kutafuta suluhisho la matatizo yetu bila kuwashirikisha mabeberu
Mungu ibariki Afrika
Lakini ukifuatilia sana mikopo hii, ambayo mabeberu wanasema eti ni mikopo ya masharti nafuu (concession loan) kutoka kwenye hizo taasisi za kifedha za kibeberu (Bretton woods institutions) haina historia nzuri sana kwa nchi zetu zinazoendelea (Developing countries)
Watatatukopesha sana kuwekeza kwenye miradi ya kuhdumia jamii, kama mashule, hospital, lakini baadaye mikopo hiyo huwa mikubwa sana na mzigo mkubwa kwa nchi zetu zinazoendelea
Mikopo ikiwa mikubwa sana na mzigo kwa nchi zetu, watatuambia tukae chini na kuandaa mipango ya kutupunguzia mzigo wa madeni (Debt relief)
Mpango huo wa kutupunguzia madeni, kwa kawaida huwa inaambatana na masharti magumu, ambayo kumsingi sio rafiki sana kwa maendeleo ya kiuchumi kwa nchi zetu, bali masharti hayo yatakuwa rafiki zaidi wa maendeleo ya kiuchumi ya nchi zao (mabeberu)
Kwa mfano kwenye miaka ya 1990, hizo taasisi za kibeberu (Bretton woods institutions) kama IMF, WORLD BANK, IDA nk, walikuja na mpango wa Structure Adjustments programs (SAP) ambapo moja ya masharti, walitutaka tuachie uchumi wetu (soko huria) ulioambatana na ubinafsishaji kwa mashirika na viwanda vyetu muhimu vya Kimkakati (Strategic companies& industries) ikiwa eti ni kupunguzia mzigo wa gharama za uendeshaji kwa serikali
Mabeberu walituambia eti hatuwezi kutumia fedha za walipa kodi wetu, kuyapa ruzuku (subsides) baadhi ya mashirika/ viwanda vyetu muhimu vya Kimkakati kwa uchumi na maendeleo ya nchi yetu
Nini kilitokea?
Baada ya masharti yao hayo, hatimaye mashirika/ viwanda vyetu vilishindwa kujiendesha kutokana na ushindani
na hatimaye viwanda/mashirika vyetu kufa
Nini kilitokea?
Baada ya mashirika/ viwanda hivyo kushindwa kujiendesha kwa kibiashara, walitokea wawekezaji wenye lengo la kunujua viwanda/ mashirika hayo kwa lengo la kuviendeleza
Lakini kwa bahati mbaya au kwa makusudi, viwanda na mashirika hayo muhimu kwa uchumi wa yetu yalikufa na ndio ukawa mwanzo wa nchi yetu kuwa soko la bidhaa zao kutoka kwenye viwanda vya nchi zao na washirika wao kitu ambacho kwa kiwango kikubwa sana kimechangia kuua ajira kwa nchi yetu
Lakiii very unfortunately, kwenye miaka ya 2000, uchumi wa nchi za kibeberu ulipata mtikisiko mkubwa (Economic recession)
Mfano mashirika na makampuni makubwa ya nchi ya Marekani tena makampuni binafsi (Public liabilities company) kama JP Morgan, Ford, Lehman Brothers, Godman and Sachs nk yalipata mtikisiko mkubwa wa kiuchumi
Lakini cha ajabu, serikali ya Marekani kwa kutumia fedha za wzlipa kodi, walitoa ruzuku kwa mashirika hayo binafsi ili kuyanusuru yasife, wakasema eti ts too big to fall
Kitu walichotukataza sisi kudanya, ndio exactly wao wanafanya kunusuru mashirika yao binafsi na uchumi wa nchi zao kwa ujumla, kwa sababu mashirika hayo yalikuwa ni msingi mkubwa wa ajira ndani ya nchi yao
Sasa leo tutakuwa ni watu wa ajabu sana na kushangaza, eti tukiamini kuwa taasisi hizo za kibeberu wanaweza kutupa msaada wa kuokoa uchumi wa nchi zetu, ambao umeathirika vibaya kutokana na janga hili la COVID-19
Mimi naamini, kama kweli walikuwa na lengo la kunusuru uchumi wa nchi zetu za Kiafrika, basi walipaswa kutusamee madeni yetu ya nyuma na si kutukopesha, kwa sababu nchi zetu hizi za kiafrika tunatumia peaa nyingi sana kila mwezi kuservice madeni yetu (Debt expenses) ambayo kimsingi kwa kiasi kikubwa madeni yetu hayo ni kutoka kwenye hizo Multilateral institutions
Waafrika tunapaswa kuwa pamoja, kushirikiana pamoja na kutafuta suluhisho la matatizo yetu bila kuwashirikisha mabeberu
Mungu ibariki Afrika