Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,426
- 18,228
Tujaribu ku-create story fupi,unaendeleza kutunga story fupi kwa kureply pale mwenzako alipoishia,na umwachie mwingine aendelee (kupokezana),unaweza kuandika mstari mmoja,miwili au hata tatu.
Usiweke hitimisho halafu wengine wakakosa pakuanzia.
Mfano mi naanza
.. Katavi alichoka na maisha magumu pale kijijini kwao,kila siku aliwaza na kuwazua jinsi ya kuanzisha maisha mapya
yenye matumaini na raha mustarehe,wazo pekee lililomjia akilini ni kutafuta nauli ili apande basi ya kuelekea jiji la Dar es salaam ili kuanzisha maisha mapya kwa kufanya vibarua.Jumapili asubuhi akiwa stendi ya mabasi wilayani mpanda aliamua kukata tiketi,akapangiwa siti ya dirishani,mda ulipofika abiria wote walipanda ndani ya basi,mara msichana mmoja mrembo aitwaye Preta
akaenda kusimama karibu na Katavi kisha akachukua kitambaa kwenye mkoba wake akaifuta kiti kisha akakaa na kumwonyeshea Katavi tabasamu,dereva akawasha gari na safari ya kuelekea dar ikaanza.............(endelea)
Usiweke hitimisho halafu wengine wakakosa pakuanzia.
Mfano mi naanza
.. Katavi alichoka na maisha magumu pale kijijini kwao,kila siku aliwaza na kuwazua jinsi ya kuanzisha maisha mapya
yenye matumaini na raha mustarehe,wazo pekee lililomjia akilini ni kutafuta nauli ili apande basi ya kuelekea jiji la Dar es salaam ili kuanzisha maisha mapya kwa kufanya vibarua.Jumapili asubuhi akiwa stendi ya mabasi wilayani mpanda aliamua kukata tiketi,akapangiwa siti ya dirishani,mda ulipofika abiria wote walipanda ndani ya basi,mara msichana mmoja mrembo aitwaye Preta
akaenda kusimama karibu na Katavi kisha akachukua kitambaa kwenye mkoba wake akaifuta kiti kisha akakaa na kumwonyeshea Katavi tabasamu,dereva akawasha gari na safari ya kuelekea dar ikaanza.............(endelea)
Last edited by a moderator: