Ni hoja nzuri kuanza kuona na kuwapima wawakilishi wetu ili kuwatofautisha na wale waojiwakilisha wenyewe, vyama vyao au matakwa mengine tofauti na ya wapiga kura wao. Kwa kuwa Rasimu ya Katiba inapendekeza kila mkoa wa Tanzania bara uwe jimbo moja la uchaguzi, itakuwa vyema kuwalinganisha wabunge wanaotoka mkoa mmoja. Kwa mfano, kwa mkoa wa Mwanza, iwapo wabunge wote wa sasa wataingia katika kinyang'anyiro hicho na tunahitaji wawili tu kati yao, nani anatufaa kati yao? Kwa kundi la wanaume....Je ni Ngeleja, Dr. Limbu, Machemuli, Wenje, Kiwia, Ndasa, Kitwanga au Dr. Tizeba? Kwa wanawake...je ni Leticia Nyerere, Maria Hewa na wengine wa vitu maalum ambao siwakumbi? Vivyo hivyo tunaweza kuangalia mikoa mingine. Madhalani kwa mkoa wa Mbeya, je, ni Mbilinyi, Zambi, Pro. Mwandosya, dr. Mwakyembe au Prof. Mwandosya n.k.? Singida...je, ni Tundu Lissu, Mwigulu, Dewji, Chiligati etc? Kwa Dar... je, ni Mnyika, Makongoro Mahanga, Zungu, Ndugulile n.k? Karibuni tuendeleze hoja!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.