Tuwapeleke watoto wakasome kiingereza

Tuwapeleke watoto wakasome kiingereza

Kazi inayopatikana Chuga ni za utalii peke yake? Hakuna shughuli zingine? Watu wote wa Chuga wanajua kiingereza? Huu ujauaji wa kifala ndo inafanya Arusha ionekane bangi tupu.
Kua na uelewa basii mada inasemaje?
Tuwapeleke watoto wakasome kiingereza.
Nimekupuuza
 
Nasisitiza kuwa kiingereza sio lugha ya kujivunia, hayo mambo ya kutoboa hakuna kitu hapo, wapo wengi duniani wsmetoboa na hawajui kuongea kiingereza.
Si habari ya kujivunia mkuu, ni suala la kurahisisha mawasiliano na dunia tu na kufikisha vigezo fulani muhimu katiaka maisha ya kisasa.

Yani hata kama unataka kusoma habari za The James Webb Telescope ni vigumu sana kuzikuta zimeandikwa katika Kiswahili.
 
Unamaanisha nn ?
Kiingereza ni lugha muhimu katika dunia ya leo.

Hata hapa JF unaweza kukipinga, lakini ili ukipinge katika post yako ya kukipinga utakuwa ushakitumia katika "Reply" na "Post Reply".
 
Raia wengi wa Tanzania hawana uwezo huo.
Habari.

Kumekuwa na changamoto ya watu kulalamika maisha magumu.

Ila yote juu ya haya kama mzazi unamtoto jitahidi sana uweke ubahili pembenj pelekeni watoto wenu English medium.

Leo hii kwenye interview tu kijana imekuwa ngumu kutumia hata dk 10 kujieleza kwa kiingereza.

Kwa muingiliano wa watu nchini na fursa mbalimbali katika soko la ajira inahitaji sana mtu mwenye kuweza kuongea na kuandika lugha ya kiingereza fasaha.

Rai yangu Tuwapeleke watoto wetu wakasome kiingereza.
 
Si habari ya kujivunia mkuu, ni suala la kurahisisha mawasiliano na dunia tu na kufikisha vigezo fulani muhimu katiaka maisha ya kisasa.
Unaweza kunipa sababu ya Google kuendelea kuzipa kipaumbele lugha za mataifa mbalimbali duniani?

Kwa nini hawajali lugha moja (English) pekee?

Ni kweli lugha ni mawasiliano Ila hiyo imani yenu Watz ya kuamini kuwa kila mzungu ni mwingereza itaendelea kuwaumbua kila siku dadeki
 
Habari.

Kumekuwa na changamoto ya watu kulalamika maisha magumu.

Ila yotw juu ya haya kama mzazi unamtoto jitahidi sana uweke ubahili pembenj pelekeni watoto wenu English medium.

Leo hii kwenye interview tu kijana imekuwa ngumu kutumia hata dk 10 kujieleza kwa kiingereza.

Kwa muingiliano wa watu nchini na fursa mbalimbali katika soko la ajira inahitaji sana mtu mwenye kuweza kuongea na kuandika lugha ya kiingereza fasaha.

Rai yangu Tuwapeleke watoto wetu wakasome kiingereza.
Mimi nakuunga mkono ndg. Hilo halina ubishi. Leo saa nne asubuh nimekutana na mzee mmoja mwaka jana mwishon tulikutana tena akaniomba nimuangalizie matokeo ya mwanae ya form two. Na ndio ilikuwa mara ya kwanza kuonana. Alipata Div IV=33

Sasa leo tumekutana tena tukakumbukana akaniambia aliongea na mwanae. Akaahidi atakazana. Tukiwa tunaendelea kuangalia possible solutions zaid akasema shule ya msingi tangu darasa la kwanza mpk la saba alikuwa anakuwa wa pili au wa 3. Nikamwambia mzee hapo mchawi ni kiingereza. Maana amepata D mbili zingine F.

Bas akanipa namb yake tukaachana.
Nilipofika nilipokuwa naenda nilianzisha mdahalo mkubwa san kuhs lugha ya kiingereza. Watu waliongea mpk bas.

So kiingereza ni maji ukisema huyaogi Urakunywa ukisema hunywi utapikia. Nk..
 
Unaweza kunipa sababu ya Google kuendelea kuzipa kipaumbele lugha za mataifa mbalimbali duniani?

Kwa nini hawajali lugha moja (English) pekee?

Ni kweli lugha ni mawasiliano Ila hiyo imani yenu Watz ya kuamini kuwa kila mzungu ni mwingereza itaendelea kuwaumbua kila siku dadeki
Mkuu,

Kwani nani kasema kila mzungu ni Muingereza? Mbona unachanganya madawa?

Sijasema Kiswahili hakina maana. Na sifikiri hoja hapa ni kwamba watoto waachane na Kiswahili wajifunze Kiingereza.

Katika Kiingereza kuna kitu kinaitwa "zero sum game", maana yake, ukipata hiki, unapoteza kile. Kujifunza lugha ya Kiingereza maana yake si kutojifunza Kiswahili. Wataalam wa lugha wanashauri watoto wajifunze lugha zaidi ya moja tangu wadogo, kwa sababu, kadiri mtu anavyozidi kukua, uwezo wa kujifunza lugha kirahisi unapungua.

Kiswahili ni lugha muhimu, ndiyo maana hata Google wanajitahidi.

Lakini, ukitaka kujua tofauti ya Kiswahili na Kiingereza, anagalia idadi ya vitabu vinavyochapishwa Kiswahili kwa mwaka, linganisha na Kiingereza. Angalia research papers, movies, websites etc.

Utaona Kiingereza kina nafasi kubwa sana, na hili halidogoshi nafasi ya Kiswahili.

We can chew gum and walk.
 
Habari.

Kumekuwa na changamoto ya watu kulalamika maisha magumu.

Ila yote juu ya haya kama mzazi unamtoto jitahidi sana uweke ubahili pembenj pelekeni watoto wenu English medium.

Leo hii kwenye interview tu kijana imekuwa ngumu kutumia hata dk 10 kujieleza kwa kiingereza.

Kwa muingiliano wa watu nchini na fursa mbalimbali katika soko la ajira inahitaji sana mtu mwenye kuweza kuongea na kuandika lugha ya kiingereza fasaha.

Rai yangu Tuwapeleke watoto wetu wakasome kiingereza.
Nilijua utasema serikali yako ibadili syllabus shule za kata zifundishwe kama shule za binafsi za English medium
 
Huo ni uongo mtupu
Hata hapo unapobisha shurti ubofye "Reply" na "Post Reply".

Unakibishia Kiingereza umuhimu wake, wakati huohuo, ili point zako za kubishia umuhimu wa Kiingereza zitufikie, inabidi ukitumie Kiingereza!

Hapo ndipo utajua Kiingereza ni muhimu au si muhimu.
 
Nilijua utasema serikali yako ibadili syllabus shule za kata zifundishwe kama shule za binafsi za English medium
Serikali ipi mkuu ya kuleta syllabus ya kiingereza wakati sekondari yenyewe wanataka physics ifundishwe kwa kiswahili.

Wanadai kiswahili ni lugha ya saba duniani.
 
Back
Top Bottom