Tusitishane: Hakuna maisha baada ya kifo!

Tusitishane: Hakuna maisha baada ya kifo!

Hakuna mwenye ukweli, fanya unachoweza wakati wa uhai wako. Roho ikitoka inaenda kuanzisha maisha mahali pengine kwa umbo lingine. Wewe unafutika katika uso wa dunia.
 
Huu ni mtazamo wangu na ndio maana hakuna reference toka kwenye kitabu chochote!.

Kama unafikiri swala la kufikiri uliwaachia waliopita tu na wewe hufai kufikiri kuhusu hayo basi jua wewe ni Kama bendera fuata upepo!. Kama unutafuta ukweli juu ya maisha yako usifikiri ukweli huo upo mbali! Maana hata wewe ni sehemu ya uhai ambao ni maisha!.

Kauli tamu na fikirishi ni it's your choice!..
Kufikiri nimekuachia wewe mwenye ubongo mpana.

Basi sawa, hebu fikiria mwanaadamu huwa anakuwa wapi/nini kabla hajazaliwa, halafu unipe majibu.

Halafu linganisha na hii hoja yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha yapo baada ya haya tunayoishi. Tenda mema na utubu sana utaenda ukaishi PEPONI au tenda maovu maisha yako baada ya haya itakuwa MOTONI.
 
Mi najiulizaga ni kwanini? mtu anapozaliwa ajui kama kuna mungu mpaka aambiwe.kwaiyo mungu anashindwa kuumba binadamu automatic tukimjua yeye bila kuambiwa habari zake uku tukiambiwa akuna analo shindwa.
 
Mkuu unajifunga sana kwa kutumia akili tu umesema kufa ni kama vile bado hujazaliwa yaani hujui chochote dunia lakini uko tumboni kwa nchi za wenzetu wanakuwa wshatambua kuwa ni mtoto wa kike au kiume then ukazaliwa ukaishi ndo uhai sasa ukafa tena duniani kwa nn usiwe tena mzima na kuishi maisha mengine kama continuation of trend

Yaani tulianza kuwa wafu tukiwa tumboni tukaishi tukafa duniani kwa hyo tunaweza kuwa hai katika maisha mengine full stop epuka kula viporo asubuhi unaleta mawazo mgando hapo nimekujibu kwa fikra kama wewe sio vitabu
Kitendo cha mimba kuingia tumboni ushaingia dunian anataka kujua kabla ya mimba kutungwa kwenye alikuwa ndiko kwenye ataenda
 
Mkuu vitu vingi kwenye hizo nukuu zako ni mifano tu
Biblia inasema wafu hawajui chochote, then wafu wawe wanaongea, nini maana ya kufa sasa.
Ikiwa wanaongea maana yake wote wapo hai
Kifo kinafananishwa na usingizi
Mtu anasehemu tatu yaani mwili, roho na nafsi. Lazima ujue mtu akifa kila sehemu itaenda wapi
 
Jibu fupi na rahisi ni kuwa huwezi kupata ushahidi wa kitu ambacho hakipo! Ukiona umepata ushahidi wa ambacho hakipo basi jua kipo otherwise wanaosema Kuna maisha baada ya kifo waje watupe ushahidi maana wao wanaamini yapo.
S
Jibu fupi na rahisi ni kuwa huwezi kupata ushahidi wa kitu ambacho hakipo! Ukiona umepata ushahidi wa ambacho hakipo basi jua kipo otherwise wanaosema Kuna maisha baada ya kifo waje watupe ushahidi maana wao wanaamini yapo.
Sasa sijui hujaelewa wapi ? Nimekwambia hivi, tupe ushahidi wa kile unachodai, unaleta utoto kwamba kitu ambacho hakipo. Sasa tunakuuliza hivi umejuaje kama hakuna maisha baada ya kifo ? Swali ndilo hilo la wewe kutupa ushahidi juu ya kutokuwepo maisha baada ya kifo.

Sasa usikimbie swali ambalo, wewe kwanza unatakiwa kutoa ushahidi kisha wanao sema kuna maisha baada ya kifo walete ushahidi. Kwahiyo tupe ushahidi usi ruke ruke kama bisi.8
 
Mkuu ni vizuri kabla hujaandika hii mada ungejiridhisha kwanza kwa kufanya utafiti juu ya Near Death Experiences watu waliokaribia kufa kabisa na madaktari wakathibitisha mtu huyu kafa lakini baada ya kupelekwa mochwari anazinduka. Huenda ukajifunza jambo,,,
 
ukipita jangwani ukaona nyumba na imepandwa maua na bustani kwa utaritibu utasema hii nyumba imejenga yenyewe na bila mtu yeyote kubuni kutulia na kudesign sivyo?
Ha ha! Naelewa dhana ya Uungu ila sijui ni Mungu yupi ndio kaumba ulimwengu! Kwa maana Miungu wanaotwajwa na walioandikwa kuwa wao ndio chanzo cha ulimwengu kwangu naona bado hawajajitosheleza! Au wanapewa sifa zilizozidi uhalisia.. so ili unielewe hapo usiweke Umungu bali Uungu!.. Uungu kinaweza kuwa chochote aidha ni nguvu yenye intelligence this is what i think! Ndio maana unaona jibu Kama tata.
 
S

Sasa sijui hujaelewa wapi ? Nimekwambia hivi, tupe ushahidi wa kile unachodai, unaleta utoto kwamba kitu ambacho hakipo. Sasa tunakuuliza hivi umejuaje kama hakuna maisha baada ya kifo ? Swali ndilo hilo la wewe kutupa ushahidi juu ya kutokuwepo maisha baada ya kifo.

Sasa usikimbie swali ambalo, wewe kwanza unatakiwa kutoa ushahidi kisha wanao sema kuna maisha baada ya kifo walete ushahidi. Kwahiyo tupe ushahidi usi ruke ruke kama bisi.8
Kwanza nyinyi mnaosema kuwa kunamaisha baada ya kifo hamjaleta ushahidi isipokuwa mnaamini tu kuwa kuna hilo Jambo!.. hakuna mfu yoyote alieweza kutoka ktk huo ufu na akaleta majibu ya uhakika juu ya maisha baada ya kifo!.. (na najua hilo haliwezekani maana kilichokufa ni kimekufa na hakuna kipya hapo!)
Mmekuwa mkihusisha zaidi hayo maisha na maswala ya kiroho na hata hiyo roho hamjawahi thibitisha uwepo wake!.
Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wenye wenye uhalisia wenye kuonyesha kuwa kilichokufa kinaenda kuwa hai ktk ulimwengu mwengine! Hakuna uthibitisho wa hilo!. Uhai unamazingira yake kwa haya unayoyaona,kuyahisi na kuyasikia.
Unapata ugumu wa kuelewa kwa maana bado haujafahamu maana nzima ya kifo! Kilichokufa hakina uhai na kilicho hai ni kile chenye sifa za uhai.. hizi ni kama zone na uhai ni sifa fulani zikipotea hiyo hali ndio kifo nothing utafanya you go no where!.
Kiumbe kikifika tunakizika then unaambiwa kimeenda mbinguni kwenye maisha mapya!.. huu upofu wa aina yake!.

Uhai ni uhai na kifo ni kifo labda Kama baadhi yenu hamuelewi maana ya kifo.
 
Mkuu ni vizuri kabla hujaandika hii mada ungejiridhisha kwanza kwa kufanya utafiti juu ya Near Death Experiences watu waliokaribia kufa kabisa na madaktari wakathibitisha mtu huyu kafa lakini baada ya kupelekwa mochwari anazinduka. Huenda ukajifunza jambo,,,
Huko kunathibitisha vipi kuwa kunamaisha baada ya kifo..?

Unauhakika upi kuwa hao madaktari walipima kwa asilimia zote kuwa mtu huyu process zake zote za mwili zilikufa..?

Mi sioni Kama mnaelewa maana ya kifo for sure..😅 kifo hakina near kikifika kimefika nitafatiliaje waliokaribia kufika kifoni na wakati hawakufikia kifo!! Waliofika kifoni ni waliokufa hawana Tena sifa za uhai.. hawasemi,hawatendi,hawapumui na hawali n.k
Kama alizinduka basi jua alikuwa hai huyo na walikosea kupima! Kilichokufa kimekufa sasa Kama alizinduka huyo atawekwa ktk kundi la waliokuwa wamepoteza fahamu tu. Mkuu uhai unamazingira yake ulishawahi ona kiumbe kilichoharibika kimezinduka..?

Sasa hao unaowaona wamezinduka jua bado mazingira ya uhai wao hayajaharibika!. Ni Kama mbegu ikiwa nje ya mazingira ya yenyewe kuweza kuota basi haitaota ila ikiwekwa ktk mazingira yake ya kuota itaota haswa ikiwa haijaharibiwa!

Siku nitajua Kuna miujiza nikiona kilichoharibika (kukosa sifa ya uhai) kikiwa hai namaanisha hata ubongo uwe umeharibika kabisa halafu hicho kitu kiwe tena hai.

Nafikiri ipo haja ya watu kufundishwa sifa za uhai na kifo!.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom