Ground Zero
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 342
- 95
Mniwie radhi kwa kuweka picha ambazo hazipendezi hapa. Hawa ni vijana watatu waliopatwa na mauti kwa kuchomwa moto ( kama wanavyoonekana kwenye gari) na mwingine akiwa amepigwa mawe pale chini ( alikuwa hai bado wakati picha zinachukuliwa leo asubuhi). Tukio hilo lilitokea leo asubuhi eneo la makuburi ambapo watu wenye hasira wamewachoma hawa vijana kwa tuhuma za ujambazi.
kutokana na uzoefu wangu, tabia ya kujichukulia sheria mikononi imegharimu maisha ya watu wengi wasio na hatia na kuwasababishia vilema vya maisha kwa dhana tu. Siku hizi hata mwendawazimu akipiga kelele za mwizi ukiwa unapita hata kama unafanya mazoezi ya kwenda kwenye michezo ya olympic watu bila kujiuliza wanaweza kukuvamia na maisha yakakutoka. Tabia hii isipodhibitiwa kwa adhabu kaliiiiii, nchi hi haitakuwa salama kwa yeyote!