El Roi
JF-Expert Member
- May 29, 2020
- 263
- 502
Nikiri kwamba mie kwa majukumu yangu ya kimaisha ni mtu ninayezunguka sana katika nchi hii na maeneo mengine ya Dunia ukipenda.
Arusha pamoja na kuwa na sifa za madhari nzuri, muingiliano wa watu wa mataifa mbalimbali, na taasisi mbalimbali za kimataifa, ukweli usemwe, Jiji hilo sio salama kabisa kwa maisha ya watu.
Arusha ndo mahali ambapo bangi inavutwa mahali popote, ni mahali ambapo watu wanatembea wakiwa wamechomekea visu kwenye nguo na vinaonekana, Arusha ndo watu wamejaa matusi ya nguoni na hakuna anayeshangaa.
Ukweli, Jiji hilo limejaa aina ya maovu ambayo mengi yake ukiyaona hakika yameruhusiwa na jamii yenyewe na vyombo vya Dola pia.
Kuna wakati najiuliza, hivi hii ni jamii Gani inayoogopa waovu kiwango hiki?
Ni kweli sitetei matumizi ya nguvu na kutofuata sheria, lakini ukweli ni kwamba, jamii ya Arusha, kwa sehemu kubwa ni jamii isiyozingatia maadili kabisa na ndo maana hata yanapofanyika matendo ya kijinai na uovu, bado utawaona watu wametulia tu na huoni kuteseka na kukereketwa kuzuia mambo ya kijinga ya viwango hivyo.
Kwa kuwa nimejitambulisha kama mtembezi, hapo ndo nawakumbuka watu kutoka kanda ya ziwa. " Jamii hailei mambo ya kijinga yaliyopitiliza kama yanayotendeka kwenye Jiji la Arusha.
Ni rahisi sana kushikwa na kutandikwa viboko hadharani na wananchi ukiwa baadhi ya maeneo kanda ya ziwa kwa sababu tu umetukana mama au mtu yeyote kinachoitwa matusi ya nguoni.
Kwa hiyo sitetei watu kuvunja sheria na kujichukulia sheria mikononi, lakini ukweli usemwe, " jamii haionekani hata kucahukia tu vitendo hivyo". Jamii ikianza kuonyesha hasira juu ya maovu na vitendo vyenye mwelekeo wa jinai, waovu na watu wanaojihusisha na mambo hayo wataogopa na kuacha au kuyafanya under cover na siyo waziwazi kama ilivyo.
Naiasa jamii ya Jiji la Arusha kubadili tabia na kuanza kuchukia aina ya matendo ya ovyo yanayoendelea jijini humo.
Kwa vyombo vya Dola, nashauri kuanza kufanya kazi zao nje ya mazoea.
Mazoea wanayofanya walinzi wetu wa amani, yatafanya jamii ianze kuishi bila kuogopa Sasa.
Uwepo wa majeshi huleta nidhamu katika jamii. Tatizo ninaloliona, uwepo wa majeshi ,Sasa unakuwa kama jambo la kawaida.
Hivi unawezaje ukiwa police, kupita mahali kwenye genge ambalo ukuta walioegemea au ukipenda kwenye kijiwe, kumechorwa picha za wavuta bangi na watu wanaovuta bangi na hata huulizi au kulazimisha magenge na vijiwe hivyo kutoweka?
Inawezekanaje ,kondakta wa gari anakutana na traffic police, wanamsikia kabisa ananuka bangi na bado hawawezi kumkamata na kumpeleka kituoni akajibu kwa Nini ananuka bangi?
Tukio lililotokea Jana la kuuawa wa kijana anayeitwa Ally Dangote, kwangu Mimi pamoja na kwamba kauawa lakini limekuja kwa kuchelewa. Kijana mwenye umri wa miaka 19 anawezaje kutamba kwenye jamii inayochukia uovu muda wote huo?
Inawezekana vipi mtu anasumbua na kuua watu hadharani Ili hali wananchi wanajua anakoishi, anachofanya na anapatikanaje? Police na vyombo vya Dola, vinawezaje kuacha mwovu anatamba karibu mwezi mzima akiua watu hadharani?
Nini maana ya uwepo wetu kama wananchi na vyombo vya Dola?
Wakati Fulani nilipatwa na taharuki nikiwa maeneo Fulani ya Jiji hilo.
Na ilikuwa hivi ," Kuna kijana mmoja aliyekuwa mwendesha pikipiki aliuawa kwa mazingira ya kugongwa na gari" sekeseke lilikuja siku ambayo kijana yule alikuwa anapelekwa mazikoni. Believe me, barabara ilichafuka. Pikipiki zilijaa barabara nzima kana kwamba mji umetekwa na boda boda, barabara ni zao na hakuna mwingine anayezitumia..
Ungewaona vijana wameshikilia chupa za pombe barabarani, wanakunywa pombe wakati wanaendesha pikipiki.
Ajabu ilifika mahali , wengine walikuwa wanabishana kwa maneno, hivyo wanachofanya ni kutelemka kwenye boda na wengine bajaji, wanapigana ngumi, huku magari ya abiria na watumiaji wengine wa magari wakiwa wanasubiri ugomvi uishe.
Pale nilipokuwa, nilishuhudia ugomvi unaisha wenyewe kwa wao kujiamua.
Sikuoni raia hata kulalamikia tu, waendesha magari wako kwenye magari wanasubiri nao bodaboda wamalize ugomvi wao.
Mbaya zaidi hakuna police waliokuja kuondoa hiyo bughudha, achilia ukweli kwamba kituo Cha police kilikuwa kama mita 200 tu kutoka eneo la tukio na magari yenyewe yalikuwa msururu mpaka eneo la kituo.
Hebu nambie katika mazingira hayo, huu uovu haujaruhusiwa?
Watu wa Arusha ni waoga hata kukemea tu ujinga. Wanajifanya wako busy kutafuta pesa. Wamejaa ulevi wa kutafuta Mali ambazo zinaibwa kijinga na watu wanaowalea kwa kuruhusu tambia mbaya kutamalaki.
Vyombo vya Dola na hasa police, woke up please.
Huu mji Sasa unataka aina nyingine ya ku curb criminality ambayo naiona inanyemelea mji huu.
Huu mji unataka psychology ya askari kubadilika Sasa. Huu mji unataka upolisi hasa na siyo kucheza na viashiria vya uhalifu.
Magenge yaliyotapakaa Kila mahali kama vijiwe yachunguzwe na yapigwe marufuku.
Unywaji wa mapombe usio na mipaka unazaa uharifu uliyopitiliza kwa kudhani Hawa ni walevi tu.
Yuko wapi RPC wa aina ya Kombe miaka ile? We need a serious police force , if at all, we want to defeat the rampant criminality hovers the city of Arusha.
Arusha pamoja na kuwa na sifa za madhari nzuri, muingiliano wa watu wa mataifa mbalimbali, na taasisi mbalimbali za kimataifa, ukweli usemwe, Jiji hilo sio salama kabisa kwa maisha ya watu.
Arusha ndo mahali ambapo bangi inavutwa mahali popote, ni mahali ambapo watu wanatembea wakiwa wamechomekea visu kwenye nguo na vinaonekana, Arusha ndo watu wamejaa matusi ya nguoni na hakuna anayeshangaa.
Ukweli, Jiji hilo limejaa aina ya maovu ambayo mengi yake ukiyaona hakika yameruhusiwa na jamii yenyewe na vyombo vya Dola pia.
Kuna wakati najiuliza, hivi hii ni jamii Gani inayoogopa waovu kiwango hiki?
Ni kweli sitetei matumizi ya nguvu na kutofuata sheria, lakini ukweli ni kwamba, jamii ya Arusha, kwa sehemu kubwa ni jamii isiyozingatia maadili kabisa na ndo maana hata yanapofanyika matendo ya kijinai na uovu, bado utawaona watu wametulia tu na huoni kuteseka na kukereketwa kuzuia mambo ya kijinga ya viwango hivyo.
Kwa kuwa nimejitambulisha kama mtembezi, hapo ndo nawakumbuka watu kutoka kanda ya ziwa. " Jamii hailei mambo ya kijinga yaliyopitiliza kama yanayotendeka kwenye Jiji la Arusha.
Ni rahisi sana kushikwa na kutandikwa viboko hadharani na wananchi ukiwa baadhi ya maeneo kanda ya ziwa kwa sababu tu umetukana mama au mtu yeyote kinachoitwa matusi ya nguoni.
Kwa hiyo sitetei watu kuvunja sheria na kujichukulia sheria mikononi, lakini ukweli usemwe, " jamii haionekani hata kucahukia tu vitendo hivyo". Jamii ikianza kuonyesha hasira juu ya maovu na vitendo vyenye mwelekeo wa jinai, waovu na watu wanaojihusisha na mambo hayo wataogopa na kuacha au kuyafanya under cover na siyo waziwazi kama ilivyo.
Naiasa jamii ya Jiji la Arusha kubadili tabia na kuanza kuchukia aina ya matendo ya ovyo yanayoendelea jijini humo.
Kwa vyombo vya Dola, nashauri kuanza kufanya kazi zao nje ya mazoea.
Mazoea wanayofanya walinzi wetu wa amani, yatafanya jamii ianze kuishi bila kuogopa Sasa.
Uwepo wa majeshi huleta nidhamu katika jamii. Tatizo ninaloliona, uwepo wa majeshi ,Sasa unakuwa kama jambo la kawaida.
Hivi unawezaje ukiwa police, kupita mahali kwenye genge ambalo ukuta walioegemea au ukipenda kwenye kijiwe, kumechorwa picha za wavuta bangi na watu wanaovuta bangi na hata huulizi au kulazimisha magenge na vijiwe hivyo kutoweka?
Inawezekanaje ,kondakta wa gari anakutana na traffic police, wanamsikia kabisa ananuka bangi na bado hawawezi kumkamata na kumpeleka kituoni akajibu kwa Nini ananuka bangi?
Tukio lililotokea Jana la kuuawa wa kijana anayeitwa Ally Dangote, kwangu Mimi pamoja na kwamba kauawa lakini limekuja kwa kuchelewa. Kijana mwenye umri wa miaka 19 anawezaje kutamba kwenye jamii inayochukia uovu muda wote huo?
Inawezekana vipi mtu anasumbua na kuua watu hadharani Ili hali wananchi wanajua anakoishi, anachofanya na anapatikanaje? Police na vyombo vya Dola, vinawezaje kuacha mwovu anatamba karibu mwezi mzima akiua watu hadharani?
Nini maana ya uwepo wetu kama wananchi na vyombo vya Dola?
Wakati Fulani nilipatwa na taharuki nikiwa maeneo Fulani ya Jiji hilo.
Na ilikuwa hivi ," Kuna kijana mmoja aliyekuwa mwendesha pikipiki aliuawa kwa mazingira ya kugongwa na gari" sekeseke lilikuja siku ambayo kijana yule alikuwa anapelekwa mazikoni. Believe me, barabara ilichafuka. Pikipiki zilijaa barabara nzima kana kwamba mji umetekwa na boda boda, barabara ni zao na hakuna mwingine anayezitumia..
Ungewaona vijana wameshikilia chupa za pombe barabarani, wanakunywa pombe wakati wanaendesha pikipiki.
Ajabu ilifika mahali , wengine walikuwa wanabishana kwa maneno, hivyo wanachofanya ni kutelemka kwenye boda na wengine bajaji, wanapigana ngumi, huku magari ya abiria na watumiaji wengine wa magari wakiwa wanasubiri ugomvi uishe.
Pale nilipokuwa, nilishuhudia ugomvi unaisha wenyewe kwa wao kujiamua.
Sikuoni raia hata kulalamikia tu, waendesha magari wako kwenye magari wanasubiri nao bodaboda wamalize ugomvi wao.
Mbaya zaidi hakuna police waliokuja kuondoa hiyo bughudha, achilia ukweli kwamba kituo Cha police kilikuwa kama mita 200 tu kutoka eneo la tukio na magari yenyewe yalikuwa msururu mpaka eneo la kituo.
Hebu nambie katika mazingira hayo, huu uovu haujaruhusiwa?
Watu wa Arusha ni waoga hata kukemea tu ujinga. Wanajifanya wako busy kutafuta pesa. Wamejaa ulevi wa kutafuta Mali ambazo zinaibwa kijinga na watu wanaowalea kwa kuruhusu tambia mbaya kutamalaki.
Vyombo vya Dola na hasa police, woke up please.
Huu mji Sasa unataka aina nyingine ya ku curb criminality ambayo naiona inanyemelea mji huu.
Huu mji unataka psychology ya askari kubadilika Sasa. Huu mji unataka upolisi hasa na siyo kucheza na viashiria vya uhalifu.
Magenge yaliyotapakaa Kila mahali kama vijiwe yachunguzwe na yapigwe marufuku.
Unywaji wa mapombe usio na mipaka unazaa uharifu uliyopitiliza kwa kudhani Hawa ni walevi tu.
Yuko wapi RPC wa aina ya Kombe miaka ile? We need a serious police force , if at all, we want to defeat the rampant criminality hovers the city of Arusha.