Acha Maneno
Member
- Oct 6, 2018
- 49
- 96
Hili swali nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila ya kupata majibu ðŸ˜
Nimehitimu Diploma ya Uhasibu kwa shida sana, maana nilikuwa natumia nguvu ya ziada kutafuta wanafunzi wenzangu wanisaidie walichofundisha Lecturers Darasani kwakuwa nilikuwa sisikii wakifundisha.
Baada ya kufaulu na kupata GPA iliyoniruhusu kuendelea na Degree nikakwama kwenye kulipia ada, ikabidi niingie mtaani kutafuta kazi.
Nimetafuta kazi sehemu tofauti lakini nimekosa, kuna baadhi ya watu niliowaomba kazi waliniweka wazi baada ya kuwaomba sana wakaniambia "Hawawezi kuajiri mtu mwenye shida ya usikivu".
Tatizo nililonalo
Nina shida ya masikio kuvuma kwahyo hili tatizo linanifanya nisielewe kinachozungumzwa japokuwa nasikia sauti. Napata changamoto hasa mtu anapoongea kwa haraka au anapoongea kwa kumung'unya maneno.
KUNA BAADHI YA WATU NINAWASILIANA NAO VIZURI KABISA KUTOKANA NA UONGEAJI WAO, NA KUNA MUDA MAZINGIRA YA UKIMYA YANANIPA AFUHENI KUBWA YA KUWASILIANA NA WATU.
SIJUI NI NANI ATANIAJIRI, INANIUMA SANA KUONA HAYA YAKINITOKEA NA UMRI WANGU UKIZIDI KUONGEZEKA BILA YA KUWA NA FUTURE YOYOTE.
Nimehitimu Diploma ya Uhasibu kwa shida sana, maana nilikuwa natumia nguvu ya ziada kutafuta wanafunzi wenzangu wanisaidie walichofundisha Lecturers Darasani kwakuwa nilikuwa sisikii wakifundisha.
Baada ya kufaulu na kupata GPA iliyoniruhusu kuendelea na Degree nikakwama kwenye kulipia ada, ikabidi niingie mtaani kutafuta kazi.
Nimetafuta kazi sehemu tofauti lakini nimekosa, kuna baadhi ya watu niliowaomba kazi waliniweka wazi baada ya kuwaomba sana wakaniambia "Hawawezi kuajiri mtu mwenye shida ya usikivu".
Tatizo nililonalo
Nina shida ya masikio kuvuma kwahyo hili tatizo linanifanya nisielewe kinachozungumzwa japokuwa nasikia sauti. Napata changamoto hasa mtu anapoongea kwa haraka au anapoongea kwa kumung'unya maneno.
KUNA BAADHI YA WATU NINAWASILIANA NAO VIZURI KABISA KUTOKANA NA UONGEAJI WAO, NA KUNA MUDA MAZINGIRA YA UKIMYA YANANIPA AFUHENI KUBWA YA KUWASILIANA NA WATU.
SIJUI NI NANI ATANIAJIRI, INANIUMA SANA KUONA HAYA YAKINITOKEA NA UMRI WANGU UKIZIDI KUONGEZEKA BILA YA KUWA NA FUTURE YOYOTE.