Shining Light
JF-Expert Member
- Jan 8, 2024
- 214
- 291
Naona tumefanya unyanyasaji wa mtandaoni uonekane kama kitu cha kawaida bila kujali kwa kufanya hivyo tunaweza kuharibu maisha ya watu wengi sana, kwasababu unyanyasaji au bullying kwa kimombo inaathiri sana afya za akili za watu.
Siku hizi mambo mengi yapo hadharani na yanaelezewa kwa upana na urefu, Matatizo ya Afya ya Akili iwemo. Ni dhahiri kuwa haya mambo yanaweza muumiza mtu katika fikra yake na kusababisha msongo wa mawazo ambapo unaweza kuharibu mfumo wa maisha ya mtu au mbaya zaidi ukaharibu maisha ya mtu kimoja kuanzia kazini, chuoni, shuleni na hata nyumbani.
Mitandaoni ni moja ya sehemu ambayo tunafanyiana unyanyasaji mkubwa sana, tunatukana na comments za kutisha.
Chukulia mfano Mange alivyopost connection ya Gigy, tukumbuke ni jambo la faragha, halituhusu, yeye kupost na sisi kuendelea kusambaza na kushadadia huku tukituna kwa maneno ya kashfa tayari ni kosa na sio uungwana.
Ni kwasababu hatujiweki katika viatu vyao ndio maana tunaona sawa tu kuendeleza jambo hili, lakini fikiria mtu wako wa karibu leo, mama yako, dada yako au wewe mwenyewe unapatwa na jambo hili utaweza kuhimili manyanyaso na masimango yanayokuja kwako? Sasa kwanini tunaendelea kuwa sehemu ya watu wanaendeleza ukatili huu dhidi ya waathirika hawa?
Tubadilike, jamii bora inaanza kujengwa na wewe.
Siku hizi mambo mengi yapo hadharani na yanaelezewa kwa upana na urefu, Matatizo ya Afya ya Akili iwemo. Ni dhahiri kuwa haya mambo yanaweza muumiza mtu katika fikra yake na kusababisha msongo wa mawazo ambapo unaweza kuharibu mfumo wa maisha ya mtu au mbaya zaidi ukaharibu maisha ya mtu kimoja kuanzia kazini, chuoni, shuleni na hata nyumbani.
Mitandaoni ni moja ya sehemu ambayo tunafanyiana unyanyasaji mkubwa sana, tunatukana na comments za kutisha.
Chukulia mfano Mange alivyopost connection ya Gigy, tukumbuke ni jambo la faragha, halituhusu, yeye kupost na sisi kuendelea kusambaza na kushadadia huku tukituna kwa maneno ya kashfa tayari ni kosa na sio uungwana.
Ni kwasababu hatujiweki katika viatu vyao ndio maana tunaona sawa tu kuendeleza jambo hili, lakini fikiria mtu wako wa karibu leo, mama yako, dada yako au wewe mwenyewe unapatwa na jambo hili utaweza kuhimili manyanyaso na masimango yanayokuja kwako? Sasa kwanini tunaendelea kuwa sehemu ya watu wanaendeleza ukatili huu dhidi ya waathirika hawa?
Tubadilike, jamii bora inaanza kujengwa na wewe.