GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,890
- 109,608
Tokea nizaliwe sijawahi kuona kama siyo kusikia Mnyama Paka akikohoa na kupiga chafya ila kwa muda wa Siku kama Nne hivi nimebahatika kulala maeneo tofauti tofauti hapa Jijini Dar es Salaam kama vile Mbezi ya Kimara, Mbagala, Sinza na Tegeta Masaiti na kuona maajabu.
Zamani hapa Dar es Salaam ilikuwa Paka akikuona tu lazima atoke ' Nduki / Akimbie ' lakini kwa miaka ya hivi karibuni Paka ndiye amekuwa akitutoa ' Nduki / Akitukimbiza ' Sisi Wanadamu na kuna muda anaweza akawa anakukimbiza huku anakuita kabisa na jina lako.
Nina wasiwasi mkubwa sana kama Paka wa sasa hivi wa Dar es Salaam ni Wanyama kweli kweli.
Nawasilisha.
Zamani hapa Dar es Salaam ilikuwa Paka akikuona tu lazima atoke ' Nduki / Akimbie ' lakini kwa miaka ya hivi karibuni Paka ndiye amekuwa akitutoa ' Nduki / Akitukimbiza ' Sisi Wanadamu na kuna muda anaweza akawa anakukimbiza huku anakuita kabisa na jina lako.
Nina wasiwasi mkubwa sana kama Paka wa sasa hivi wa Dar es Salaam ni Wanyama kweli kweli.
Nawasilisha.