Tupende, tusipende: Tanzania inanyemelewa na udini!

Status
Not open for further replies.
Vipi kuhusu SHURA YA MAIMAMU NA WALAKA WAO? Kwa nin inapokuja dhana ya udini UKRISTO NDIO UNAPEWA KIPAUMBELE?
 
Kwa kawaida mtu anapofanya kosa kisha akakiri baada ya kuulizwa, kuna dalili ya kwamba ataacha. Ila ukikuta hataki kukiri na anakanusha na kusema uongo, basi kuna hatihati kuwa hataacha. Tangu kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi na hata baada ya uchaguzi matukio ni mengi mno ambayo hayahitaji maelezo maalum ndipo mtu aelewe kuwa kuna udini wa kutisha katika nchi hii. Actually kama mtu atapitia sawasawa vitabu na kuongea na watu waliokuwa serikalini tangu enzi hizo na wakawa wakweli, wala hakuna shaka kuwa udini ulitengenezwa na kupandikizwa na hata ukafikia hatua ya watu wanaopendelewa kuona ni haki yao kuwanyonya wengine na nchi ni yao peke yao. Mtu akizoea kula 90% ya chakula chote, basi siku akipewa hata 60% utamsikia analalamika eti kaonewa. Kama tungeamua sote kila mtu amuogope Mungu kwa kujizuia kusema uongo, basi wote maoni yetu yangekuwa ya aina moja hapa jamvini kwamba kuna UDINI MKUBWA MNO. Ni bahati mbaya kwamba inaonekana wengine uongo ni kama sehemu ya imani yao. Yeyote anayesema kuwa hakuna udini eti ameusikia kwa Kikwete tu na wengine Redio Iman, huyo ni muongo na anaweza kuongea lolote la kudanganya.
Asanteni
 
Ni bahati mbaya kwamba inaonekana wengine uongo ni kama sehemu ya imani yao. Yeyote anayesema kuwa hakuna udini eti ameusikia kwa Kikwete tu na wengine Redio Iman, huyo ni muongo na anaweza kuongea lolote la kudanganya.
Asanteni

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100% ila nadhani tatizo sio uongo bali ufuasi wa kibubusa wa viongozi wa siasa, watu wamepeleka bongo zao likizo na kusubiri waje waambiwe na 'mitume' watu wa vyama vyao. Ni ajabu kwa mtu mwenye akili zake asubiri mtu amuambie kama TZ kuna udini au la, la ajabu huyo huyo anayesema hakuna udini anatoa mfano wa redio imani kama inahubiri udini. Kwa ujumla nampongeza JK kusimama hadharani kulisemea hili na kumtaka Slaa na wenzake waje hadharani wawaambie wafuasi wao kuwa kuna udini na sote kama wa Tanzania tutafute suluhisho la kudumu badala kuendelea kuficha ficha eti ili tu kufikia malengo ya kisiasa.
 
Kikwete ndio huyo tushamsikia, je hao viongozi wengine wa vyama vya upinzani nao wana maoni gani?
 
Nadhani kuna ushindan wa kisiasa, kuanzia serikalin, chama tawala na hata upinzani. Swala la udini limekuwa agenda mhm kwa wanasiasa. TZ HATUJAFIKIA THAT KIWANGO! Kauli za Jk ndio cheche za moto wa udini tz, hii nikwa maoni yangu mimi!
 
Nadhani kuna ushindan wa kisiasa, kuanzia serikalin, chama tawala na hata upinzani. Swala la udini limekuwa agenda mhm kwa wanasiasa. TZ HATUJAFIKIA THAT KIWANGO! Kauli za Jk ndio cheche za moto wa udini tz, hii nikwa maoni yangu mimi!

Issue sio umefikia kiwango gani? issue ni kuwa upo au haupo ili tuweze kutibu, kama upo kwa kiwango kidogo huu si ndio wakati muafaka kuuuzungumzia ili kuutibu bado na mapema.
 
Mkuu Nduka nadhan sasa nakuleta kwenye hoja, unavyojenga hoja nami unanifungua, Jambo la kutambua hapo nikwamba UDINI BONGO HAUPO BT UNAJENGWA NA HAO WAOKUJA NA HOJA ZA UDINI PASIPO MASHIKO YOYOTE, kauli zao ndio Madhara kwa watanzia na chachu ya kujengeka kwa Udini bongo. Kuna swali halijajibika hapo, JE UDINI UNAJENGWA NA WAKRISTO TU? Kwa nin umekua ukizungumzwa kwenye matamasha ya kikristo sana?
 
Mkuu Nduka nadhan sasa nakuleta kwenye hoja, unavyojenga hoja nami unanifungua, Jambo la kutambua hapo nikwamba UDINI BONGO HAUPO BT UNAJENGWA NA HAO WAOKUJA NA HOJA ZA UDINI PASIPO MASHIKO YOYOTE, kauli zao ndio Madhara kwa watanzia na chachu ya kujengeka kwa Udini bongo. Kuna swali halijajibika hapo, JE UDINI UNAJENGWA NA WAKRISTO TU? Kwa nin umekua ukizungumzwa kwenye matamasha ya kikristo sana? NI NIN UPANDE WA WAISLAM KTK UDINI HUU ANAOHUBIRI MH?
 
Ndugu wanaJF wenzangu nadhani wengi wenu mtakubaliana nami kuwa ni muda sasa tangu hubiri za Jk juu ya wanasiasa watumiao dini zianze kusikika. Mwanzo wa haya ilikua kipindi kile cha kampeni wkt wa uchaguzi mkuu, pungeni akihutubia Bunge, ktk hotuba zake za mwho wa mwezi na hata apatapo nafasi popote pale.
Jana akiwa km mgeni rasmi ktk tamasha la Pasaka amepata kusikika akisisitizia juu ya udini..safari ameenda mbali zaidi akikesa/akiwataka watanzania tukumbuke kuwa UHURU WA WATANZANIA ULILETWA NA WAKRISTO NA WAISLAM WAKISHIRIKIANA KWA PAMOJA, Kifupi mimi simwelewi na sielewi haswa anachomaanisha. Siasa na dini zisichanganywe kivipi? Yeye ni Rais, mwanasiasa na mwenyekiti wa chama tawala, ktk tamasha la pasaka yeye km mwanasiasa kafata nin? Si wadhehebu hzo. Nani mdini? Nadhan Rais anapaswa kuwa direct ktk hili, atueleze kinagaubaga juu ya hili, zaidi ya hapo nikama vile mchezo wa kuvua dagaa kwa karabai. Wenzangu mnamuelewaje mheshimiwa wetu? Nawasilisha hoja!
Nafsi yake inamsuta. Mwanasiasa pekee aliyehubiri UDINI wakati wa kampeni alikuwa Jakaya Mrisho Kikwete. Alisaidiana na mtoto wake Miraji ambaye mama yake ni Mkristo. Mpambe mkuu wa Jakaya na Mwanae Miraji katika jitihada za kueneza udini alikuwa Shamte wa Six Mobile aliyeumbuliwa na Gazeti la Guardian. Mjinga mwingine aliyezungumzia UDINI alikuwa Zito Kabwe, aliyekuja kupata uenyekiti wa kamati ya bunge kwa msaada wa JK.
Kwa hali hiyo, mwenye kuweza kuelezea udini nchini mwetu ni ama Jakaya Kikwetu, ama Miraji Kikwete ama Shamte wa Six Mobile, ama Zito Kabwe
 
Anapandikiza notion mbaya kwa watanzania simply because of his defencing mechanism, KIATU SANA!
 
Mfamaji haachi kutapata. Rais wetu hajiamini na anachokitenda. Kama ni udini mbona siye watanzania tunaishi pamoja kwa amani. Yawezekana amechoka kuona tunaishi pamoja hivyo anatamani kuona tunajisudan au jinigeria. Viongozi wa dini msichoke endeleen kukemea maovu bila kuogopa. JK ukome kutaka kutenga watanzania kwa msingi wa dini.
 
mkuu kauli kama hizo si nzuri na hazitatufikisha pazuri. Katika dunia hii hapajatokea kuwa na wailam pekee au wakristo pekee. Kwa hiyo kila mmoja aone mwenzake bila yakujali dini yake kabila yake anahaki zote za msingi ikiwa ni pamoja na kuongoza/ lakini pale mmoja anapomuona mwengine hafai kuwa ikulu kwa sababu tu si waimani yake basi hilo ni tatizo na linapaswa kushughulikiwa. Frankly writting, mimi siipendi ccm sio leo tu tangu enzi hizo lakini kwa kauli kama hizo za akina mtikila haziniweki mahala pazuri kiimani.
We need changes. Lets make, na tuachane na mabo ya udini. Otherwise tunakoelekea si pazuri. Angalia michango ya wengi humu, imekaa kidini tu. Imefikia mpaka nikawa nafikiria hii jf ifutwansi kwa sababu ya hatari ya kisiasa bala ya kidini, wengi humu tuna ndugu wa damu wa dini tofauti, majirani, marafiki, mabosi na hata mademu/mameni. Ndo maana najaribu kuiangalia hatari hiyo kwa jicho la tatu. Ni hayo tu.

udini ni mradi wa watawala wa ccm kuwagawa watu ili watawale kiurahisi (divide and rule). Kwa bahati mbaya watu wanaaminishwa tofauti na hali halisi. Tanzania hakuna udini na familia zilizo nyingi bara utakuta ukoo mmoja kuna watu wa dini mbali mbali. Matukio ya kijamii watu wanashirikiana wote bila kujali kabila wala dini. Sasa hili la udini linatoka wapi??? Rais hapaswi kabisa kumwagia petrol hili la udini. "kwa watu kama mitikila wana falsafa za kidini-sawa na hili linatokana na rais kushindwa kukemea maovu yanayofanywa na upande fulani wa dini dhiidi ya mwingine. Mfano wanapona masheik wakihamasisha uvunjifu wa amani kwa mikusanyiko ya dini za kikristo, eg. Tukio la kushambuliwa na kuuwawa kwa wakristo mto wa umbu; mhadhara wa ki islamu kupongeza mauji hayo arusha, au mihadhara kiislamu ya chuki dhiidi ya ukristo ya manzese-inawafanya waamini kuwa kiongozi wa nchi ni mdini" kwa kuwa hachukua hatua kuzuia mambo yanayotia chachu mgawanyiko wa jamii.

Mzee ruksa (mwinyi) alikuwa na uwezo wa kukemea ukweli pale ambapo mtu aliingilia uhuru wa mtu wa kuabudu au kula au kufanya akipendacho ili mradi havunji sheria ya nchi. Aliweza kukemea hata pale dini yake mwenyewe ilipokengeuka (mfano, uchomaji mabucha ya nguruwe dsm). Kwa hili jk kashindwa! Nyerere aliyekuwa muasisi wa umoja wa watanzania aliweka misingi imara ya "serikali/mchi kutokuwa na dini" ni sera hii aliyoisimamia kwa nguvu zote na hivyo kufanikiwa kujenga jamii imara isiyo na udini tunayoendelea kufaidi sasa. Misingi hiyo inatakiwa kuenziwa kwa nguvu zote.

Pamoja na udhaifu wa kiutawala wa rais na rais, ukweli utabaki kuwa watanzanzania hawana udini damuni bali wanataka kuaminishwa wawe wadini. Ni hii ni hatari kubwa. Natoa wito kwa kila mwana jf kujivunia kwa kila hali "utanzania wake" na kuachana na fahari za "udini wake, ukabila wake, ukanda wake maana fahari hizo ni za kijinga na wala hazitatusaidia katika umoja na utengamano wetu.
 
jamani tuache kua negative sana na huyu president,he is not crazy,udini upo na nyie mnaojifanya kukataa haupo ndo wa kwanza kua na udini
 
hii radio ni uozo mwingine katika serikali ya KIKWETE wanajua kabisa kwamba hii radio inakera watu kwa kukashifu dini zao lakini sasa ina manufaa kwao wamekaa kimya, ina maana mpaka rais mristo aje kuifunga hii radio
Radio Imaan bado inaendelea kuwahimiza waislamu wasishirikiane na wakristo. Trh 21 jioni niliisikia Radio Imaan ikiwahimiza waislamu wawe tayari kwa lolote kama madai yao hayataingizwa kwenye katiba mpya.

Madai yenyewe:
1. Waislamu ndo walioleta uhuru hivyo madaraka serikalini lazima iwe 50/50.(eti wakristu waliopigania uhuru hawazidi 10 nchi nzima!)
2. Mahakama ya Kadhi lazima iwemo, na majaji wake lazima wahudumiwe na serikali kwa 100% kama majaji wa mahakama za taifa!
3. Na utumbo mwingi unao fanana na huo!

Nilishindwa kuelewa kama nchi hii imefika huko na vyombo vya dola havichukui hatua. Kama wameshindwa kuifungia Radio Imaan, basi wana-back up ya JK ili lengo lake litimie! Kwa taarifa yao "WATASHINDANA LAKINI HAWATASHINDA!"
 
Ni udini alioasisi jakaya mrisho kikwete ndio anaouenzi na kuutaja mara kwamara
 
Kuna watu wanataka kumpora kikwete kwamba ni Rais wa dini moja....huu ni upuuzi na haitakaa itokee katika taifa hili dini moja ikamnyakua Rais wa wote kuwa wa imani moja.
 
Rais Kikwete alifika katika tamasha la pasaka saa 10 jioni na kuondoka saa 1 usiku kwa maana kwamba alikaa masaa 3. Rais alishukuru sana kupata mwaliko huo na zaidi alishukuru sana kukuta Waislamu na wakristo wakiwa pamoja katika ukumbi huo na katika hili akajijumuisha yeye mwislamu na kaimu mkuu wa mkoa Meck Sadiq na wengine wengi. Rais akasema hiyo ndio Tanzania anaijua tangu akiwa mtoto ambapo watanzania wana umoja bila kujali dini zao. Kwamba hiyo ndio Tanzania tuliyoachiwa na Mwalimu Nyerere hivyo alisema ni faraja kwake kukuta Waisalmu na wakristo wakiwa pamoja ukumbini humo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom