Mnapenda Pesa anazotoa Rais katika makanisa yenu lakini mnachukia misimamo ya viongozi wa makanisa yenu huu ni upumbavu

Mto Songwe

JF-Expert Member
Jul 17, 2023
6,017
12,305
Moja ya kosa kubwa lililo fanyika Tanzania toka utawala wa awamu ya kwanza ni kushindwa kupambana na udini.

Kilichofanyika wakati wa Nyerere na sasa ni kupambana na udini kwa kutengeneza udini wa dini hizi mbili Ukristo na Uislam.

Sio kweli kuwa Tanzania hakuna udini kama katiba inavyosema. Tanzania kuna udini wa ukristo na uislam ulio sogezwa karibu zaidi na serikali.

Huwezi sema unapambana na udini kwa kutengeneza udini wa ukristo na uislam muda huo huo.

Ni wiki kadhaa zimepita nilihoji hapa kuhusu uhalali wa Rais kutoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa kanisa la KKKT Moshi majibu niliyopata humu yalinisikitisha sana.

Watu wanazipenda sana dini zao kuliko kupenda matumizi ya akili katika kuchanganua mambo.

Moja ya madhara ya dini katika utawala ni kutumika kulitawala vyema tabaka tawaliwa, hapa ndio sehemu rahisi zaidi kutawala watu wako vyema. matumizi ya akili katika dini kwa watu yapo chini sana kuliko sehemu yoyote ile.

Samia akitoa pesa katika ujenzi wa nyumba zenu za ibada mnaona sawa tu wala hamjiulizi ila viongozi wa dini wakisema wanakubaliana na serikali mnachukizwa. Ni kipi hasa kinacho wachukiza ?

Mnashindwa kuchukizwa na Rais kuvunja vipengele vya katiba kwa kushiriki kutangaza dini fulani kinyume na katiba inavyosema ila kwa ukosefu wenu wa akili mnasema Rais anadumisha upendo baina ya Watanzania.

Hivi Watanzania mnajua maana ya serikali isiyo na dini kweli ?
 
20231231_191715.jpg
 
Hapo kwenye kumchangisha SSH pesa za kanisa, Mbowe na KKKT walifeli sana ni aibu kupokea feza za mtu mbadhirifu kwa maana utakua mnafiki wakati wa kumkosoa utakapofika utaonekana mlamba asali tu.

Niliwambia CDM Mbowe kazingua KKKT wakanipopoa.
 
Balance hafa Magufuli alisaidia ujenzi kule Dodoma wa msikitini...Unachoshindwa kuelewa ni kwamba serikali inaangalia raia wake wale majority hata kuchaguliwa wanachaguliwa na majority ndio wanawapa power.

Serikali inalenga wahusika wananchi moja kwa moja ,wao wanatafuta njia ya kuwagusa wananchi ..Tz dini ipo na inagusa asilimia kubwa ya wananchi ndio maana wao wanatumia njia kuwagusa wananchi moja kwa moja kwa kuchangia dini.

Mbona hata mpira wanachangia ,wapo watu wanaona mpira ni ujinga hawana mda nao.
 
Moja ya kosa kubwa lililo fanyika Tanzania toka utawala wa awamu ya kwanza ni kushindwa kupambana na udini.

Kilichofanyika wakati wa Nyerere na sasa ni kupambana na udini kwa kutengeneza udini wa dini hizi mbili Ukristo na Uislam.

Sio kweli kuwa Tanzania hakuna udini kama katiba inavyosema. Tanzania kuna udini wa ukristo na uislam ulio sogezwa karibu zaidi na serikali.

Huwezi sema unapambana na udini kwa kutengeneza udini wa ukristo na uislam muda huo huo.

Ni wiki kadhaa zimepita nilihoji hapa kuhusu uhalali wa Rais kutoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa kanisa la KKKT Moshi majibu niliyopata humu yalinisikitisha sana.

Watu wanazipenda sana dini zao kuliko kupenda matumizi ya akili katika kuchanganua mambo.

Moja ya madhara ya dini katika utawala ni kutumika kulitawala vyema tabaka tawaliwa, hapa ndio sehemu rahisi zaidi kutawala watu wako vyema. matumizi ya akili katika dini kwa watu yapo chini sana kuliko sehemu yoyote ile.

Samia akitoa pesa katika ujenzi wa nyumba zenu za ibada mnaona sawa tu wala hamjiulizi ila viongozi wa dini wakisema wanakubaliana na serikali mnachukizwa. Ni kipi hasa kinacho wachukiza ?

Mnashindwa kuchukizwa na Rais kuvunja vipengele vya katiba kwa kushiriki kutangaza dini fulani kinyume na katiba inavyosema ila kwa ukosefu wenu wa akili mnasema Rais anadumisha upendo baina ya Watanzania.

Hivi Watanzania mnajua maana ya serikali isiyo na dini kweli ?
haiwezekani kuchukizwa kama wew watu wako huru kuwaza vema na kuamua watakavyo,

yaanini kung'ag'ana na chuki moyoni dhidi ya mwingine 🐒

kipengele gani cha Katiba kimevunjwa kikavinjika 🐒

atakuunga mkono nani kwa dharau na dhihaka kama hazi 🐒
eti "kwa ukosefu wenu wa akili "

haya mwenye akili kutwa kulialia, kulalamika na kulazimisha watu wafikiri, wawaze na kutenda utakavyo wewe 😜
 
Hapo kwenye kumchangisha SSH pesa za kanisa, Mbowe na KKKT walifeli sana ni aibu kupokea feza za mtu mbadhirifu kwa maana utakua mnafiki wakati wa kumkosoa utakapofika utaonekana mlamba asali tu.

Niliwambia CDM Mbowe kazingua KKKT wakanipopoa.
Watu sio waelewa
 
haiwezekani kuchukizwa kama wew watu wako huru kuwaza vema na kuamua watakavyo,

yaanini kung'ag'ana na chuki moyoni dhidi ya mwingine 🐒

kipengele gani cha Katiba kimevunjwa kikavinjika 🐒

atakuunga mkono nani kwa dharau na dhihaka kama hazi 🐒
eti "kwa ukosefu wenu wa akili "

haya mwenye akili kutwa kulialia, kulalamika na kulazimisha watu wafikiri, wawaze na kutenda utakavyo wewe 😜
Wewe ni mzima kweli ?
 
Balance hafa Magufuli alisaidia ujenzi kule Dodoma wa msikitini...Unachoshindwa kuelewa ni kwamba serikali inaangalia raia wake wale majority hata kuchaguliwa wanachaguliwa na majority ndio wanawapa power.

Serikali inalenga wahusika wananchi moja kwa moja ,wao wanatafuta njia ya kuwagusa wananchi ..Tz dini ipo na inagusa asilimia kubwa ya wananchi ndio maana wao wanatumia njia kuwagusa wananchi moja kwa moja kwa kuchangia dini.

Mbona hata mpira wanachangia ,wapo watu wanaona mpira ni ujinga hawana mda nao.
Kazi ya serikali ni kusaidia ujenzi wa makanisa na misikiti ?
 
Wewe ni mzima kweli ?
nina uzima wa milele,

hebu nawe check UTI tu tuone kama uko na health muzuri, achilia mbali malaria na sukari.

pressure ni juu sana hiyo mihemko inaeleza wazi hali ya uzima wako hamna haja kupima 🐒
 
Tanzania tuna udini na ukabila na unyumbani wa hali ya juu sana kuliko tunavyoona. Ila tu tumepoa, yaani sio issue kivile. Ikipigwa simba na yanga tunafurahi maisha yanaendelea
 
Back
Top Bottom