Nawauliza manguli, wazoefu wa kulumba
Nimekiona kivuli, pichaye imenifumba
Inanikata kauli, mashairi kuyaimba
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Naanza na mlimani, vitivo vyenye kufana
Wamesoma wa zamani, elimu wameiona
Mbona nchi taabani, umasikini kwa sana
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Elimu ya uhandisi, wakufunzi wenye dhima
Wanabukua nahisi, matokeo mbona kimya
Au haina nafasi, kwa dunia hii jama?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Kwenye kitivo uchumi, maporofesa lukuki
Sioni faida mimi, digirii zenu feki
Mbona nchi haihami, kule chini haitoki?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nchi haifaidiki, hasa kwenye mikataba
Sheria yetu ya dhiki, isiyo jaa kibaba
Au kuna ushabiki, kila mtu anaiba?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Watu wenye mamlaka, kwa heshima nawaita
Wananchi tumechoka, kwa kauli zenu tata
Kwanini mnaridhika, wakati sisi twasota?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Siwaachi viongozi, mlioshika ofisi
Mbona mwatuchuna ngozi, mmegeuka mafisi
Sisi tumewapa kazi, kwanini mmetuasi?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nawe jemedari wetu, mkuu wa hii kaya
Kucha kutwa kwa wenzetu, kwako unaona haya?
Twataka ahadi zetu, chonde chonde we Jakaya
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nchi yenye utajiri, Tanzania yasifika
Mbona mambo siyo shwari, kwenye uchumi hakika
Tukae tutafakari, ninajua tutafika
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Kaditama wa tamati, nimemaliza kutunga
Mpira naweka kati, najua mmejipanga
Tukiweka mikakati, twaweza vuna mpunga
Napumzika jamvini, mlumbe mimi nafunga.
Nimekiona kivuli, pichaye imenifumba
Inanikata kauli, mashairi kuyaimba
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Naanza na mlimani, vitivo vyenye kufana
Wamesoma wa zamani, elimu wameiona
Mbona nchi taabani, umasikini kwa sana
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Elimu ya uhandisi, wakufunzi wenye dhima
Wanabukua nahisi, matokeo mbona kimya
Au haina nafasi, kwa dunia hii jama?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Kwenye kitivo uchumi, maporofesa lukuki
Sioni faida mimi, digirii zenu feki
Mbona nchi haihami, kule chini haitoki?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nchi haifaidiki, hasa kwenye mikataba
Sheria yetu ya dhiki, isiyo jaa kibaba
Au kuna ushabiki, kila mtu anaiba?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Watu wenye mamlaka, kwa heshima nawaita
Wananchi tumechoka, kwa kauli zenu tata
Kwanini mnaridhika, wakati sisi twasota?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Siwaachi viongozi, mlioshika ofisi
Mbona mwatuchuna ngozi, mmegeuka mafisi
Sisi tumewapa kazi, kwanini mmetuasi?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nawe jemedari wetu, mkuu wa hii kaya
Kucha kutwa kwa wenzetu, kwako unaona haya?
Twataka ahadi zetu, chonde chonde we Jakaya
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Nchi yenye utajiri, Tanzania yasifika
Mbona mambo siyo shwari, kwenye uchumi hakika
Tukae tutafakari, ninajua tutafika
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?
Kaditama wa tamati, nimemaliza kutunga
Mpira naweka kati, najua mmejipanga
Tukiweka mikakati, twaweza vuna mpunga
Napumzika jamvini, mlumbe mimi nafunga.