Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba

Mundu

JF-Expert Member
Sep 26, 2008
2,707
638
Nawauliza manguli, wazoefu wa kulumba
Nimekiona kivuli, pichaye imenifumba
Inanikata kauli, mashairi kuyaimba
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Naanza na mlimani, vitivo vyenye kufana
Wamesoma wa zamani, elimu wameiona
Mbona nchi taabani, umasikini kwa sana
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Elimu ya uhandisi, wakufunzi wenye dhima
Wanabukua nahisi, matokeo mbona kimya
Au haina nafasi, kwa dunia hii jama?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Kwenye kitivo uchumi, maporofesa lukuki
Sioni faida mimi, digirii zenu feki
Mbona nchi haihami, kule chini haitoki?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nchi haifaidiki, hasa kwenye mikataba
Sheria yetu ya dhiki, isiyo jaa kibaba
Au kuna ushabiki, kila mtu anaiba?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Watu wenye mamlaka, kwa heshima nawaita
Wananchi tumechoka, kwa kauli zenu tata
Kwanini mnaridhika, wakati sisi twasota?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Siwaachi viongozi, mlioshika ofisi
Mbona mwatuchuna ngozi, mmegeuka mafisi
Sisi tumewapa kazi, kwanini mmetuasi?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nawe jemedari wetu, mkuu wa hii kaya
Kucha kutwa kwa wenzetu, kwako unaona haya?
Twataka ahadi zetu, chonde chonde we Jakaya
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nchi yenye utajiri, Tanzania yasifika
Mbona mambo siyo shwari, kwenye uchumi hakika
Tukae tutafakari, ninajua tutafika
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Kaditama wa tamati, nimemaliza kutunga
Mpira naweka kati, najua mmejipanga
Tukiweka mikakati, twaweza vuna mpunga
Napumzika jamvini, mlumbe mimi nafunga.
 
Ukimya muoneshao
Nyinyi mlio upeo
Tusipoamka leo
Nchi haitagomboka

Nchi haitagomboka
Tukionyesha kuchoka
Wenzetu wameamka
Sisi bado tunaota

Sisi bado tunaota
Twaishi kwenye viota
watatupeleka puta
Hata majirani zetu

Hata majirani zetu
waibeza kasi yetu
Twatembea kama chatu
Tena tumejilegeza

Tena tumejilegeza
nchi haitapendeza
kaya zetu zina giza
Hata hilo latushinda?

Hata hilo latushinda
Wakati tuna matunda
malighafi zinavunda
Elimu yetu ya nini?

Elimu yetu ya nini?
Haifai maishani
Wananchi taabani
Taaluma ipo wapi?
 
Ninavyowaona mimi
Hawa wa kwetu wasomi
Sijui hawana ndimi?
Maovu kuyakemea

Inasikitisha sana
Na rohoni kusonona
Wanyonge tunapoona
Wasomi wanabung'aa

Tumetupa nguvu zetu
Kuwasomesha wenzetu
Wakomboe nchi yetu
Ona wanayotufanyia

Katu hawana mapenzi
Na nchi yetu azizi
Wanaona bora kazi
Ya kuibia raia

Wanakumbatia uovu
kwa mikataba mibovu
Hawajani maumivu
Sisi wanayotutia

Sina jibu la kutoa
Elimu gani inafaa
Kwani tulishakosea
Wezi tuliwaachia

Labda tupate kichaa
Nchi aje ibomoa
Tuanze upya sawia
Lakini, hilo si la kuombea
 
Ninavyowaona mimi
Hawa wa kwetu wasomi
Sijui hawana ndimi?
Maovu kuyakemea

Inasikitisha sana
Na rohoni kusonona
Wanyonge tunapoona
Wasomi wanabung'aa

Tumetupa nguvu zetu
Kuwasomesha wenzetu
Wakomboe nchi yetu
Ona wanayotufanyia

Katu hawana mapenzi
Na nchi yetu azizi
Wanaona bora kazi
Ya kuibia raia

Wanakumbatia uovu
kwa mikataba mibovu
Hawajani maumivu
Sisi wanayotutia

Sina jibu la kutoa
Elimu gani inafaa
Kwani tulishakosea
Wezi tuliwaachia

Labda tupate kichaa
Nchi aje ibomoa
Tuanze upya sawia
Lakini, hilo si la kuombea
Nimependa hiyo verse ya mwisho...
 
Nawauliza manguli, wazoefu wa kulumba
Nimekiona kivuli, pichaye imenifumba
Inanikata kauli, mashairi kuyaimba
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Naanza na mlimani, vitivo vyenye kufana
Wamesoma wa zamani, elimu wameiona
Mbona nchi taabani, umasikini kwa sana
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Elimu ya uhandisi, wakufunzi wenye dhima
Wanabukua nahisi, matokeo mbona kimya
Au haina nafasi, kwa dunia hii jama?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Kwenye kitivo uchumi, maporofesa lukuki
Sioni faida mimi, digirii zenu feki
Mbona nchi haihami, kule chini haitoki?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nchi haifaidiki, hasa kwenye mikataba
Sheria yetu ya dhiki, isiyo jaa kibaba
Au kuna ushabiki, kila mtu anaiba?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Watu wenye mamlaka, kwa heshima nawaita
Wananchi tumechoka, kwa kauli zenu tata
Kwanini mnaridhika, wakati sisi twasota?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Siwaachi viongozi, mlioshika ofisi
Mbona mwatuchuna ngozi, mmegeuka mafisi
Sisi tumewapa kazi, kwanini mmetuasi?
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nawe jemedari wetu, mkuu wa hii kaya
Kucha kutwa kwa wenzetu, kwako unaona haya?
Twataka ahadi zetu, chonde chonde we Jakaya
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Nchi yenye utajiri, Tanzania yasifika
Mbona mambo siyo shwari, kwenye uchumi hakika
Tukae tutafakari, ninajua tutafika
Tupate elimu gani, Tanzania iwe bomba?

Kaditama wa tamati, nimemaliza kutunga
Mpira naweka kati, najua mmejipanga
Tukiweka mikakati, twaweza vuna mpunga
Napumzika jamvini, mlumbe mimi nafunga.

Hodi naja jamvini, kutoa yangu majibu
Naomba pewa hisani, timiza wangu wajibu
Jamani sikilizeni, msijepata sababu
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tamaa tuweke pembeni, tujari utu zaidi
Tafakari akirini,athali za mafisadi
Makini sote tuweni, tusije kuwa hasidi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza

Maendeleo hakuna, bila kuwa na msingi,
Ikiwa moja hakuna, kumi haiwi shilingi,
Yatatufaa ya jana, kuujenga mpya msingi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza.

Elimu tumeshapata,tatizo ni matumizi
Mmmea afya utapata, tusipokata mizizi
Wala hakuna matata, tuuache usingizi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza.

Chai yake sukari, kuutengeneza utamu
Huwezi ramba shubiri, ukitamani utamu
Kuwa na nyingi habari, ni kukwepa majukumu
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tukubari rudi nyuma, kutaka maendeleo,
Tusiwe kama wanyama, waso jana wala leo,
Mazuri kuacha nyuma, kujifanya wa kileo,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tuachane na umimi, wa kujiwekea hazina,
Tukuze wetu uchumi, kutengeneza safina,
Tuondoe huu utemi, ili tuwe wa kufana,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Kulejea wetu msingi, hiyo ni Elimu tosha,
Tusiparamie vigingi, taa zetu kutowasha,
Asili yetu ni msingi, twendako kutuonesha,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.
 

Hodi naja jamvini, kutoa yangu majibu
Naomba pewa hisani, timiza wangu wajibu
Jamani sikilizeni, msijepata sababu
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tamaa tuweke pembeni, tujari utu zaidi
Tafakari akirini,athali za mafisadi
Makini sote tuweni, tusije kuwa hasidi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza

Maendeleo hakuna, bila kuwa na msingi,
Ikiwa moja hakuna, kumi haiwi shilingi,
Yatatufaa ya jana, kuujenga mpya msingi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza.

Elimu tumeshapata,tatizo ni matumizi
Mmmea afya utapata, tusipokata mizizi
Wala hakuna matata, tuuache usingizi
Turejee asili yetu taifa kuliendeleza.

Chai yake sukari, kuutengeneza utamu
Huwezi ramba shubiri, ukitamani utamu
Kuwa na nyingi habari, ni kukwepa majukumu
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tukubari rudi nyuma, kutaka maendeleo,
Tusiwe kama wanyama, waso jana wala leo,
Mazuri kuacha nyuma, kujifanya wa kileo,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Tuachane na umimi, wa kujiwekea hazina,
Tukuze wetu uchumi, kutengeneza safina,
Tuondoe huu utemi, ili tuwe wa kufana,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.

Kulejea wetu msingi, hiyo ni Elimu tosha,
Tusiparamie vigingi, taa zetu kutowasha,
Asili yetu ni msingi, twendako kutuonesha,
Turejee asili yetu, taifa kuliendeleza.
 
Asante kwa jibu lako
Umeonesha mwamko
Anyisile we kiboko
Kichaa ni suluhisho

Tukipata kiongozi
Kichwani mwenye uchizi
Tutaukata mzizi
Wa wetu umasikini?

Je nasi wananchi
Tunaoishi kijichi
Ili tuijenge nchi
Yatupasa tuwe vipi?
 
Asante kwa jibu lako
Umeonesha mwamko
Anyisile we kiboko
Kichaa ni suluhisho

Tukipata kiongozi
Kichwani mwenye uchizi
Tutaukata mzizi
Wa wetu umasikini?

Je nasi wananchi
Tunaoishi kijichi
Ili tuijenge nchi
Yatupasa tuwe vipi?
Mundu nimekupata,
Asante yako sijaifuta,
Yafaa kama mafuta,
Yatokanayo na ufuta.

Wametuongoza timamu,
Kutuimanisha mizimu,
Heri mwendawazimu,
Taifa kushika hatamu.

Kijichi siyo tatizo,
Atawaondolea mizozo
Atawapeni mwongozo
Imara kama nguzo.

Muwe wapole kijichi,
Kama juisi parachichi,
Mtaipenda nchi,
Wazimu akiishika.
 
Mundu nimekupata,
Asante yako sijaifuta,
Yafaa kama mafuta,
Yatokanayo na ufuta.

Wametuongoza timamu,
Kutuimanisha mizimu,
Heri mwendawazimu,
Taifa kushika hatamu.

Kijichi siyo tatizo,
Atawaondolea mizozo
Atawapeni mwongozo
Imara kama nguzo.

Muwe wapole kijichi,
Kama juisi parachichi,
Mtaipenda nchi,
Wazimu akiishika.
Obheli umesifia
kichaa anatujia
kutuonyeshea njia
neema tutaiona?

sisi tuwe watulivu
tena wenye usikivu
mbona wanivunja mbavu
pekee hawezi ndugu

nchi ni kombinesheni
ya sisi wavijiweni
nawale wenye mpini
ndipo itasonga mbele

swali bado lipo pale
lauliza vilevile
ni elimu gani ile
tusome tuende mbele?


 
Safi best ila mwenzenu hapa mchango sina manake kujibu kwa mashairi mwenzenu sijui. All in all michango yenu ni mizuri wanamalenga. I appreciate. Nawatakia usiku mwema. Mwogopeni na kumwomba Mungu daima dawama!
 
Remove CCM from power. Hawana nia ya kuinua elimu sababu wanafaidika na ujinga wa wananchi. Hawataki kutawala wasomi bali mbumbumbu ili waburuzwe. Wangekuwa wana usongo an elimu yetu wangewafukuza waziri na wasaidizi wake wote baada ya kuona wameshindwa kazi. Angalia matokeo, wameshtuka?
 
Obheli umesifia
kichaa anatujia
kutuonyeshea njia
neema tutaiona?

sisi tuwe watulivu
tena wenye usikivu
mbona wanivunja mbavu
pekee hawezi ndugu

nchi ni kombinesheni
ya sisi wavijiweni
nawale wenye mpini
ndipo itasonga mbele

swali bado lipo pale
lauliza vilevile
ni elimu gani ile
tusome tuende mbele?
Mundu nimejaribu,
Swali lako kulijibu,
Kukwepa sikujaribu,
Kuutimiza wajibu.

Tuliyonayo Elimu,
Kweli ni ya kudumu,
Tumeuleta ugumu,
Sa tusione vigumu.

Asili kuirejesha,
Hiyo ni Elimu tosha,
Mapito kuyanyoosha
Taifa kutoangusha.

Tumevamia uzungu,
Na tumekuwa mizungu,
Hatujawa na uchungu,
Tunazalisha majungu.

Tuachane na usasa,
Taifa lisiwe tasa,
Tukaziache anasa ,
Tusije huko kunasa
 
nakubali anyisile
wewe umeenda shule
usemayo ndiyo yale
yatakayo tunasua

tatizo nimebaini
nchi kuwa masikini
tumeacha umakini
wa kujali utaifa

kila mtu nimchoyo
hafanyi kazi kwa moyo
tufanyayo haya siyo
hayanemeshi taifa

hata tungesoma sana
kwa vidato vilofana
kama hatutashikana
bure tunajisumbua

lamgambo nalipiga
kwa tambo si kwa kuiga
nchi ni kama mafiga
ya kuivisha ubwabwa

Figa la kwanza ni watu
tena watu wenye utu
watu wenye roho kwatu
waloshikana pamoja

la pili niwatawala
wale wasopenda kula
waongoze bila hila
tutapata burudiko

Figa la tatu elimu
iliyo shika hatamu
Elimu jama muhimu
ya kutupatia TUNU

Ninamuomba rabuka
muumba wa kutukuka
atupe bila kuchoka
baraka na nema zake.
 
Back
Top Bottom