Tungekuwa na viongozi wenye hekima, kusingekuwa na kukurupuka

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,066
Hivi karibuni waziri Bashe, ametoa kauli ya ajabu, kauli inayoashiria kukosa weledi na busara kama kiongozi.

Nasema amekosa weledi, kwa sababu mawazo yake yameishia pale alipokuwa amesimama bila ya kupima madhara yake kwasiku za mbeleni.

Kama Bashe angekuwa na hekima, kwanza angeomba taarifa kwa watoa msaada, ni virutubisho gani vimewekwa kwenye huo mchele, na ili vifanye nini kwa mlaji? Lakini pia, kama alikuwa bado na mashaka, angeweza kuchukua hata sampuli kadhaa na kuzipeleka kwenye maabara kadhaa kubwa za vyakula Duniani ili kujiridhisha.

Lakini maamuzi yake kuwa mchele huo utupwe, kudiplomasia, hiyo ni kupeleka ujumbe mzito kwa waliotoa, kuwa ni maadui zetu, wanaotaka kutuangamiza kupitia vyakula.

Nchi hii, chanjo zote za watoto tunapewa msaada. Madawa ya cancer ni msaada. Madawa ya kifua kikuu ni msaada. Madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ni msaada. Hospitali ya Mlangazila pamoja na vifaa tiba vyake, ni msaada.

Kwa kauli na maamuzi ya Waziri Bashe, ni kuwa hivi vyote tusivitumie kwa sababu hatujui vina nini ndani yake.

Sasa, kama hao walioutoa huo msaada, walifanya hivyo kwa dhamira njema, na sisi tumewachukulia ni maadui wa Taifa letu, na wenyewe wakaona kuwa kwa vile imeonekana wao hawana dhamira njema na Tanzania, wakasema basi kuanzia sasa hawatatoa msaada wowote kwa Tanzania unaohusiana na vyakula au madawa kwa sababu vitu hivyo vyote vinaingia miilini mwetu, yeye Bashe atagharamia chanjo zote za nchi hii, labda kwa kupitia ule mradi wake wa ng'ombe kule Nzega?

Nchi hii tunapewa misaada mpaka ya kujengewa vyoo!! Ni lini tuliwahi kukataa misaada ya vitu vidogo vidogo kwa maelezo kuwa tuna uwezo wa kujitegemea?

Nchi hii mpaka kutunza mbuga zetu za wanyama, tunafanya kusaidiwa. Umeme umesambazwa vijijini, kwa 80% uligharamiwa na pesa ya MCC. Tangu wasimamishe pesa ya MCC, hiyo 20% iliyobakia inatutoa jasho!

Hivi sisi ni nini tuliweza chini ya CCM hata tukasimama mbele ya uso wa Dunia, tukatamba kufanikiwa. Tunashindwa hata kuendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar. Kila siku ni hadithi. Umeme kila siku ni hadithi!!
 
Hivi karibuni waziri Bashe, ametoa kauli ya ajabu, kauli inayoashiria kukosa weledi na busara kama kiongozi.

Nasema amekosa weledi, kwa sababu mawazo yake yameishia pale alipokuwa amesimama bila ya kupima madhara yake kwasiku za mbeleni.

Kama Bashe angekuwa na hekima, kwanza angeomba taarifa kwa watoa msaada, ni virutubisho gani vimewekwa kwenye huo mchele, na ili vifanye nini kwa mlaji? Lakini pia, kama alikuwa bado na mashaka, angeweza kuchukua hata sampuli kadhaa na kuzipeleka kwenye maabara kadhaa kubwa za vyakula Duniani ili kujiridhisha.

Lakini maamuzi yake kuwa mchele huo utupwe, kudiplomasia, hiyo ni kupeleka ujumbe mzito kwa waliotoa, kuwa ni maadui zetu, wanaotaka kutuangamiza kupitia vyakula.

Nchi hii, chanjo zote za watoto tunapewa msaada. Madawa ya cancer ni msaada. Madawa ya kifua kikuu ni msaada. Madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ni msaada. Hospitali ya Mlangazila pamoja na vifaa tiba vyake, ni msaada.

Kwa kauli na maamuzi ya Waziri Bashe, ni kuwa hivi vyote tusivitumie kwa sababu hatujui vina nini ndani yake.

Sasa, kama hao walioutoa huo msaada, walifanya hivyo kwa dhamira njema, na sisi tumewachukulia ni maadui wa Taifa letu, na wenyewe wakaona kuwa kwa vile imeonekana wao hawana dhamira njema na Tanzania, wakasema basi kuanzia sasa hawatatoa msaada wowote kwa Tanzania unaohusiana na vyakula au madawa kwa sababu vitu hivyo vyote vinaingia miilini mwetu, yeye Bashe atagharamia chanjo zote za nchi hii, labda kwa kupitia ule mradi wake wa ng'ombe kule Nzega?

Nchi hii tunapewa misaada mpaka ya kujengewa vyoo!! Ni lini tuliwahi kukataa misaada ya vitu vidogo vidogo kwa maelezo kuwa tuna uwezo wa kujitegemea?

Nchi hii mpaka kutunza mbuga zetu za wanyama, tunafanya kusaidiwa. Umeme umesambazwa vijijini, kwa 80% uligharamiwa na pesa ya MCC. Tangu wasimamishe pesa ya MCC, hiyo 20% iliyobakia inatutoa jasho!

Hivi sisi ni nini tuliweza chini ya CCM hata tukasimama mbele ya uso wa Dunia, tukatamba kufanikiwa. Tunashindwa hata kuendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar. Kila siku ni hadithi. Umeme kila siku ni hadithi!!
Pamoja na njia ambayo si sawa lakini dhamira yake ni njema na waI kabisa kwamba nchi yetu lazima iwe na tahadhari na misaada kama hiyo
 
Bashe amekurupuka na kuropoka. Jambo lenyewe Wala halipo kwenye wizara yake.

Usalama wa chakula ni TBS (wizara ya viwanda na biashara)

Program ya lishe Iko wizara ya afya.

Shule ziko TAMISEMI na wizara ya elimu.

Yeye anakurupuka na kuongea uharo kwenye kitu ambacho kipo miaka nenda rudi.

Kama serikali inazo hela za kununua hicho chakula na kulisha watotot si wanunue kutoka kwa hao wakulima wa ndani!!

Unapewa msaada alafu unaanza kuleta maneno ya vijiweni na uswahili usio na maana.
 
Bashe amekurupuka na kuropoka. Jambo lenyewe Wala halipo kwenye wizara yake.

Usalama wa chakula ni TBS (wizara ya viwanda na biashara)

Program ya lishe Iko wizara ya afya.

Shule ziko TAMISEMI na wizara ya elimu.

Yeye anakurupuka na kuongea uharo kwenye kitu ambacho kipo miaka nenda rudi.

Kama serikali inazo hela za kununua hicho chakula na kulisha watotot si wanunue kutoka kwa hao wakulima wa ndani!!

Unapewa msaada alafu unaanza kuleta maneno ya vijiweni na uswahili usio na maana.

Huko vijijini wazazi wanachangishwa mahindi na maharage ili watoto wapate mlo wa mchana, wakati wazazi wenyewe, kuna maeneo, kupata chakula cha majumbani kwao, ni shida.

Ndugu zetu waislam, huwa wanasaidiwa mpaka nyama ya mbuzi toka Uarabuni, mbona hatujawahi kugomea, na kusema tuna mbuzi wa kutosha?
 
Bashe ali switch kwenye Al Shabaab mode alipokuwa akitamka hayo mbele ya hadhara ya Waislamu wenzake wala futari. Nimetambua yule jamaa ni mtu wa hisia na siyo some grounded rational thinking individual. His overall demeanor and the way he talks says it all.
 
Pamoja na njia ambayo si sawa lakini dhamira yake ni njema na waI kabisa kwamba nchi yetu lazima iwe na tahadhari na misaada kama hiyo

Tahadhari, siyo lazima uropoke!!

Kwanza hii Serikali yetu katika tahadhari za kiafya, ni duni kabisa. Huko kwenye maghala ya vyakula ya wafanyabiashara wetu wa ndani, wanatumia mpaka madawa yaliyopigwa marufuku kuwa siyo salama kwa afya za walaji, uliwahi kusikia Serikali imezuia mazao hayo kusambazwa kwa walaji? Mboga za majani na nyanya, watu wanafukiza madawa asubuhi, mteja akipatikana tu, mchana siku hiyo hiyo au masaa machache tu naadaye, mboga zinachumwa na kupelekwa sokoni. Ng'ombe wa maziwa wanakamuliwa maziwa, huku wanaumwa wakiwa wanaendelea na matibabu, uliwahi kuzisikia hizo mamlaka za Serikali zinachukua hatua zozote?

Bashe amekurupuka kutafuta sifa lakini hakuna chochote anachokijua kuhusiana na huo mchele. Kama anajua chochote, aseme amegundua una.madhara gani?
 
Hivi karibuni waziri Bashe, ametoa kauli ya ajabu, kauli inayoashiria kukosa weledi na busara kama kiongozi.

Nasema amekosa weledi, kwa sababu mawazo yake yameishia pale alipokuwa amesimama bila ya kupima madhara yake kwasiku za mbeleni.

Kama Bashe angekuwa na hekima, kwanza angeomba taarifa kwa watoa msaada, ni virutubisho gani vimewekwa kwenye huo mchele, na ili vifanye nini kwa mlaji? Lakini pia, kama alikuwa bado na mashaka, angeweza kuchukua hata sampuli kadhaa na kuzipeleka kwenye maabara kadhaa kubwa za vyakula Duniani ili kujiridhisha.

Lakini maamuzi yake kuwa mchele huo utupwe, kudiplomasia, hiyo ni kupeleka ujumbe mzito kwa waliotoa, kuwa ni maadui zetu, wanaotaka kutuangamiza kupitia vyakula.

Nchi hii, chanjo zote za watoto tunapewa msaada. Madawa ya cancer ni msaada. Madawa ya kifua kikuu ni msaada. Madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ni msaada. Hospitali ya Mlangazila pamoja na vifaa tiba vyake, ni msaada.

Kwa kauli na maamuzi ya Waziri Bashe, ni kuwa hivi vyote tusivitumie kwa sababu hatujui vina nini ndani yake.

Sasa, kama hao walioutoa huo msaada, walifanya hivyo kwa dhamira njema, na sisi tumewachukulia ni maadui wa Taifa letu, na wenyewe wakaona kuwa kwa vile imeonekana wao hawana dhamira njema na Tanzania, wakasema basi kuanzia sasa hawatatoa msaada wowote kwa Tanzania unaohusiana na vyakula au madawa kwa sababu vitu hivyo vyote vinaingia miilini mwetu, yeye Bashe atagharamia chanjo zote za nchi hii, labda kwa kupitia ule mradi wake wa ng'ombe kule Nzega?

Nchi hii tunapewa misaada mpaka ya kujengewa vyoo!! Ni lini tuliwahi kukataa misaada ya vitu vidogo vidogo kwa maelezo kuwa tuna uwezo wa kujitegemea?

Nchi hii mpaka kutunza mbuga zetu za wanyama, tunafanya kusaidiwa. Umeme umesambazwa vijijini, kwa 80% uligharamiwa na pesa ya MCC. Tangu wasimamishe pesa ya MCC, hiyo 20% iliyobakia inatutoa jasho!

Hivi sisi ni nini tuliweza chini ya CCM hata tukasimama mbele ya uso wa Dunia, tukatamba kufanikiwa. Tunashindwa hata kuendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar. Kila siku ni hadithi. Umeme kila siku ni hadithi!!
Na hao ndio viongozi tunaowategemea watuvushe !!!!

Huyu bwana sijawahi kuona busara na hekima kutoka kwake, hata siku moja.

Hata namna anavyoongea kwenye hadhara ni shida, ni kufoka na hasira juu,

Lakini tatizo sio hicho chakula, tatizo ni ili naye ajulikane yupo.

Hebu nizungumzie hili kwamba tuna chakula cha kutosha, hivi alishakuja na mpango wowote wa kuwalisha chakula Watoto mashuleni, au anajua namna watoto wanavyoteseka na njaa mashuleni,

Hivi hata anafahamu kuna miaka huko nyuma watoto walikuwa wanapewa uji mashuleni wakati wa mapumziko.

Hilo tuliache, je haoni kwamba huo ni mfano mzuri kwako kuja na wazo la umuhimu wa watoto angalau kunywa uji shuleni wenye lishe!

Kwa sababu kwa takwimu tunazopewa ni kwamba tuna tatizo kubwa sana la lishe duni hapa nchini , kiasi kwamba watoto wetu wengi wana udumavu wa akili.?!

Huvi serikali yetu haijawahi kuwaza hata siku moja kwamba wakitenga hata robo ya bajeti au chini ya hapo kwa ajili ya kununua mahindi na maharage kutoka kwa wakulima, itahamasisha hata vijana ambao hawana shughuli mjini kujikita kwenye suala la ukulima, na hapo serikali itakuwa imeua ndege wawili kwa jiwe moja.

Kwanza angalau kutakuwa na uwiano wa keki ya taifa kugawanywa kwa haki,
Ambapo kwa sasa ni wafanyakazi tu ndio wanafaidi,

Lakini pia ajira itapatikana kwa kwa sababu mazao hayo muhimu yatapata soko.

Aaa acha niishie hapa, sielewi hata hawa watu wana vivion gani!!!!
 
Hivi karibuni waziri Bashe, ametoa kauli ya ajabu, kauli inayoashiria kukosa weledi na busara kama kiongozi.

Nasema amekosa weledi, kwa sababu mawazo yake yameishia pale alipokuwa amesimama bila ya kupima madhara yake kwasiku za mbeleni.

Kama Bashe angekuwa na hekima, kwanza angeomba taarifa kwa watoa msaada, ni virutubisho gani vimewekwa kwenye huo mchele, na ili vifanye nini kwa mlaji? Lakini pia, kama alikuwa bado na mashaka, angeweza kuchukua hata sampuli kadhaa na kuzipeleka kwenye maabara kadhaa kubwa za vyakula Duniani ili kujiridhisha.

Lakini maamuzi yake kuwa mchele huo utupwe, kudiplomasia, hiyo ni kupeleka ujumbe mzito kwa waliotoa, kuwa ni maadui zetu, wanaotaka kutuangamiza kupitia vyakula.

Nchi hii, chanjo zote za watoto tunapewa msaada. Madawa ya cancer ni msaada. Madawa ya kifua kikuu ni msaada. Madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ni msaada. Hospitali ya Mlangazila pamoja na vifaa tiba vyake, ni msaada.

Kwa kauli na maamuzi ya Waziri Bashe, ni kuwa hivi vyote tusivitumie kwa sababu hatujui vina nini ndani yake.

Sasa, kama hao walioutoa huo msaada, walifanya hivyo kwa dhamira njema, na sisi tumewachukulia ni maadui wa Taifa letu, na wenyewe wakaona kuwa kwa vile imeonekana wao hawana dhamira njema na Tanzania, wakasema basi kuanzia sasa hawatatoa msaada wowote kwa Tanzania unaohusiana na vyakula au madawa kwa sababu vitu hivyo vyote vinaingia miilini mwetu, yeye Bashe atagharamia chanjo zote za nchi hii, labda kwa kupitia ule mradi wake wa ng'ombe kule Nzega?

Nchi hii tunapewa misaada mpaka ya kujengewa vyoo!! Ni lini tuliwahi kukataa misaada ya vitu vidogo vidogo kwa maelezo kuwa tuna uwezo wa kujitegemea?

Nchi hii mpaka kutunza mbuga zetu za wanyama, tunafanya kusaidiwa. Umeme umesambazwa vijijini, kwa 80% uligharamiwa na pesa ya MCC. Tangu wasimamishe pesa ya MCC, hiyo 20% iliyobakia inatutoa jasho!

Hivi sisi ni nini tuliweza chini ya CCM hata tukasimama mbele ya uso wa Dunia, tukatamba kufanikiwa. Tunashindwa hata kuendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar. Kila siku ni hadithi. Umeme kila siku ni hadithi!!
Bashe ametoa kauli kwa niaba ya Somalia tulieni.
 
Ha
Na hao ndio viongozi tunaowategemea watuvushe !!!!

Huyu bwana sijawahi kuona busara na hekima kutoka kwake, hata siku moja.

Hata namna anavyoongea kwenye hadhara ni shida, ni kufoka na hasira juu,

Lakini tatizo sio hicho chakula, tatizo ni ili naye ajulikane yupo.

Hebu nizungumzie hili kwamba tuna chakula cha kutosha, hivi alishakuja na mpango wowote wa kuwalisha chakula Watoto mashuleni, au anajua namna watoto wanavyoteseka na njaa mashuleni,

Hivi hata anafahamu kuna miaka huko nyuma watoto walikuwa wanapewa uji mashuleni wakati wa mapumziko.

Hilo tuliache, je haoni kwamba huo ni mfano mzuri kwako kuja na wazo la umuhimu wa watoto angalau kunywa uji shuleni wenye lishe!

Kwa sababu kwa takwimu tunazopewa ni kwamba tuna tatizo kubwa sana la lishe duni hapa nchini , kiasi kwamba watoto wetu wengi wana udumavu wa akili.?!

Huvi serikali yetu haijawahi kuwaza hata siku moja kwamba wakitenga hata robo ya bajeti au chini ya hapo kwa ajili ya kununua mahindi na maharage kutoka kwa wakulima, itahamasisha hata vijana ambao hawana shughuli mjini kujikita kwenye suala la ukulima, na hapo serikali itakuwa imeua ndege wawili kwa jiwe moja.

Kwanza angalau kutakuwa na uwiano wa keki ya taifa kugawanywa kwa haki,
Ambapo kwa sasa ni wafanyakazi tu ndio wanafaidi,

Lakini pia ajira itapatikana kwa kwa sababu mazao hayo muhimu yatapata soko.

Aaa acha niishie hapa, sielewi hata hawa watu wana vivion gani!!!!
Hatari sana
 
Back
Top Bottom