sikupenda kuchangia mada hii kwa kuwa inaonekana na ya kihiyo wa sheria au kama ulivosema mwanafunzi wa sheria wa semister ya kwanza ya law certificate.
Mwanasheria eti hajui kuwa sheria ya vyama vya siasa chini ya msajili imekubali kusajiliwa katiba ya chadema ambayo mwenye mada anaisema ni void ab initio. Sasa kama sheria ya vyama vya siasa imeruhusu huo mwanya wa katiba kutungwa, kwa iyo Sheria ya vyama vya siasa ya1992 ni void? Je nani anaamuru kuwa sheria iyo ni void? Ni subject of it or the court of Law? na kama ni court - inasubiri nini?
mwanasheria hajui kuwa zipo sheria za vikundi au hata nchi zinazokataa kwenda mahakamani, ipo sheria ya magazeti, sheria za TFF, cdm, nk nk.( Ouster of jurisdiction) japo bound by (courts inherent powers) Hizi hazimnyimi mtu haki yake bali zinamtaka kwanza kufuata utaratibu waliojiwekea kabla ya kuiona chombo cha haki/mahakama,au hata kuheshimu maamuzi ayo ya vyombo au taasisi husika....PIA: Ningemshauri tu akifika semester ya kwanza ya digrii ya sheria asikimbie Law of Contract, kwa kuwa aya yaliyotokea yana contractual features/yaani kujiunga kwa kwenye chama ni kukubaliana na msharti ya chama, Sheria ya mikataba inatoa mwanya wa watu kukubaliana kutokwenda mahakamani endapo mkataba umekwama, ukisaini umekubali, ukikataa kwa hiari umekataa!
Mwanasheria anadai Lissu arudi darasani sijui kusoma tafsiri ya mahakama kumkatalia ombi lake, hajui kuwa ukienda mahakamani kuomba zuio/injuction , zuio likikataliwa ina maana makubaliano yenu ya awali kabla ya zuio yanaedelea as if no injuction was sought. Kwa maana hiyo, kama chama walishaazimia kumfukuza mwanachama, wanamfukuza then yeye akikimbia kuomba zuio likafeli, then maamuzi ya chama yanabaki pale pale, zuio likikubaliwa basi maamuzi ya chama hupoteza nguvu!! Zuio limefeli maamuzi ya chama yamekubaliwa....actually failure of injuction should cement that the court reaffirms the already taken steps/awards.
Mleta mada hapa unalaumu mwakilishi wa chama kwa kukumbushi maamuzi ya kamati kuu kabla ya zuio la mfukuzwa, au unalaumu mahakama kwa kukataa kutoa amri ya zuio la ayo maamuzi? Sipendi unipe jibu.
Mwanasheria anahoji mamlaka ya mwakilishi wa chama, anataka yatolewe na superior authority? ...Ukifika hatua ya mbele utafundishwa Administrative Law, ....iyo itakufundisha vitu kama Delegation authority, ...huwezi kuwapangia chama nani atoe tamko, wao na kwa wakati wao na kwa utaratibu wao uliokubaliwa na vikao vyao halali na kupitishwa na wengi wanajua nani akisemee chama. Pia atafundishwa kuwa ukishakuwa mwanasheria mkuu wa taasisi au jumuiya flani unapewa mamlaka za kisheria kutokana na kazi yako, aidha expressly au impliedly...pia ikumbukwe kuwa Mkurugenzi wa idara ya sheria katika taasisi ndiye anayeelekeza maamuzi yoooote ya kisheria ndani ya iyo taasisi, hawezi kumwachia mwenyekiti au mtunza hazina kutoa maelekezo ya kisheria katika suala husika, endapo utaratibu uliowekwa hauruhusu mkurugenzi kuja directly basi utakuwa umeeelekeza mkurugenzi uyo aripoti na kushauri kwa nani, je utaratibu na organization chart ya chadema ikoje??...pia sio lazima maelezo ya mkurugenzi au wakili kwenye tafsiri za kisheria yasubiri aliyemtuma/ anaweza kusema ila atakutana na mwajiri wake kwenye 'kwa nini unisemee'? nayo sio kwenye ishu za kisheria ....mfano wakili akitoka kwenye maamuzi na vyombo vya habari vikataka kumuhoji mambo ya kisheria, ni kihiyo pekee anaweza kusema ngoja nikamwombe mteja ruhusa- kwa mambo ambayo ni tafsiri za kisheria wala si siri za mteja [ni kwa asiyejielewa pekee]
Anamshauri aliyekataliwa zuio kwenda kuappeal kuomba tafsiri ya kisheria ...ni mwanafunzi wa sheria wa mwaka wa kwanza anaweza kushauri ivo. Eti mtu aombe injuction/ mahakama ikatae,...kwa kukataa mahakama inakuwa imebariki maamuzi ya awali, sasa aliyenyimwa zuio akaappeal kuomba tafsiri ya sheria. Mbele ya mahakama lililetwa ombi la zuio, zuio limefeli then ubebe content nje ya document ya ombi then ukaappeal???
Je unaappeal kukataa kukataliwa zuio au unaappeal kuhusu mahamuzi ya chama na apo kumbuka hakuna maamuzi ya chama yaliyoshtakiwa bali alienda mahakamani kukataa kutolewa maamuzi na chama, je akaappeal kukataa zuio au maamuzi ya chama? Kama ni agaist maamuzi ya chama then anapasw kuappeal kwenye ngazi ya juu kwenye chama,...kama anaappeal against kukataliwa zuio basi atakuwa anaappeal kukataa kukosa zuio. Itakuwa ni Court V. Mlalamikaji , Content iwe : KUHUSU KUNYIMWA ZUIO
Je hicho kitu kipo kwenye sheria ??
Mtetezi anakataza doing an evil to justify other evil ila bado analeta kesi ya Ngeleja kwenye content ya zuio la mlalamikaji akihusisha lisu, the the emphasis of a wrong reverts to right?? Kama unalalamika kuhusu Lissu inakuwaje ulalamikie lissu compared to Ngeleja, treat different cases differently!!
kama haya yanajulikana kwa sisi watu wa kawaida, je mleta mada, mwanasheria nguli huyajui aya???Ni fedhea wala siwezi kubishana na mleta mada.[/QUOTE
Hapo umemsomesha huyo mwanafunzi wa sheria. Mkumbushe pia kuwa sheria ya uchaguzi inazuia mgombea wa urais aliyeshindwa kwenda mahakamani kuhoji matokeo. Hii haivunji katiba?