MUSSA ALLAN
JF-Expert Member
- Oct 13, 2013
- 18,925
- 13,279
Tundu Lissu ana kipaji cha uropokaji!
ninyi wanasheria wa Tz ni wehu sana. Njaa itaamaliza. Hata wewe kuna kamkate kako unatetea hapa. ZZK hajakanusha popote madai ya usaliti, that means tuhuma dhidi yake ni ukweli mtupu.
Kama hajaridhika akate rufaa kama ulivyomshauri
When arguing with someone in an attempt to get at an answer or an explanation, you may come across a person who makes logical fallacies. Such discussions may prove futile. You might try asking for evidence and independent confirmation or provide other hypotheses that give a better or simpler explanation. If this fails, try to pinpoint the problem of your arguer's position. You might spot the problem of logic that prevents further exploration and attempt to inform your arguer about his fallacy.
.............Confirmation biased people (similar to observational selection): This refers to a form of selective thinking that focuses on evidence that supports what believers already believe while ignoring evidence that refutes their beliefs. Confirmation bias plays a stronger role when people base their beliefs upon tradition and prejudice.
jidanganye nan asiejua kuna wachaga wana id zaid ya 4 humu
Nimejaribu walau kusoma post yako nimeona kuwa wewe bado mchanga sana kisheria.
1. Katiba za vyama zinasajiliwa na msajili baada ya kujiridhisha kuwa zinaendana na katiba ya nchi na ndiyo chama kinapata uhai.
2. Mwenye mamlaka ya kusema kuwa katiba imevunjwa ni mahakama na sio wewe kama ulivyojipa mamlaka hayo
3.Katika kesi ya Anisminic Ltd v Foreign Compensation Commission where House of Lord held that a statutory exclusion clause does not deprive the courts from their jurisdiction in judicial review unless it expressly states
4. Ouster clauses katika sheria za kawaida haviinyimi mahakama usingizi wake.
5. Nyongeza ni kuwa Interlocutory orders are not Appealable.
Mi sio mwanasheria lakini nimesoma post yako naona imejaa povu nyingi sana, kwanza nakataa kwamba wewe ni mwanasheria labda ndio upo semester ya kwanza mwaka wa kwanza unasomea sheria. Na wala hukumuelewa Tundu Lisu hoja yake. labda uludi tena ukasome vizuri nini hasa kimefanya zito afukzwe.
Sheria hii ndio kandamizi sababu mtu anaweza kuonewa na akaogopa kwenda mahakamani akihofia kushindwa kesi japo ana haki na kufutwa uanachama. Hamuoni kipengele hiki kinamnyima mtu haki yaki katiba?
Wanasheria tusaidieni.
Tundu Lissu ana kipaji cha uropokaji!
waulize wachaga kosa la zzk ni lip haswa,kwenda mahakaman au kutaka chama kikaguliwe au kuutaka uenyekit
Tuhuma amejibu labda ulikusudia kujibu mahala unapokusudia wewe. Baadhi ya majibu ya tuhuma hizo tembelea tovuti yake, www.zittokabwe.com
kuwa kwa msajili haina maana iko sahihi!!Nimesoma aya moja nimegundua ni ujinga tu... Kiufupi ni kwamba katiba ya CHADEMA inatambulika mpaka kwa msajili wa vyama then who are you?
Mimi sio mwanasheria na sina taaluma ya sheria ina ninataka kujua kutoka kwako mleta uzi huu. Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa daima imekuwa inaongozwa na Watanzania wenye taaluma ya sheria tena kwenye kiwango cha JAJI. Katiba zote za vyama vya siasa zinapelekwa kwa Msajili wa vyama vya siasa, anasoma na kuiridhia ndipo inapopewa baraka za kutumika. Je, vipengere kandamizi na vinavyokinzana na sheria mama ya nchi yaani Katiba ya JMT vilipataje baraka za Msajili na kuruhusu Katiba ya CDM itumike? Vinginevyo wanaotakiwa kurudi shule ni wengi tukianzia na Osisi ya Msajili wa vyama vya siasa.Katiba ya Chama chochote cha Siasa au kinginecho au sheria yoyote inayomzuia mtu yeyote kwenda Mahakamani kudai haki yake kwa kuona kama imekiukwa au inaelekea kukiukwa, katiba au Sheria hiyo ni batili tangu mwanzo wake (Null and void ab initio).
Ieleweke kuwa sheria yoyote inayotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au katiba ya Chama chochote kiwe cha Siasa au kijamii au kikundi chochote cha watu haipaswi kuwa juu ya/ au kukiuka matakwa yaKatiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ibara husika ya Katiba ya CHADEMA ni kandamizi na imekiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho ya mara kwa mara. Hata hivyo nawashangaa sana wananchi katika suala hili maana Mahakama haijatoa uamuzi juu ya uanachama wa Zitto Kabwe ndani ya CHADEMA bali imetupilia mbali kesi yake kwa kuunga mkono pingamizi la awali (P.O) la mawakili wa CHADEMA kwamba kulikuwa na makosa ya kisheria kufungua kesi hiyo kwenye Mahakama kuu ya Tanzania tena kwenye masjala kuu ya Mahakama kuu ya Tanzania (Main Registry of the High Court of Tanzania) badala ya Masjala ya Wilaya ya Mahakama hiyo (District Registry of the High Court of Tanzania)
Na kwamba kesi hiyo ingefunguliwa kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi.
Mimi sipendi kuzungumzia uamuzi wa Mahakama kwenye forum hii maana maadili ya kazi zangu na taaluma yangu hayaniruhusu ila ninachotaka kufanya ni kumkosoa kaka yangu, msomi mwenzangu Tundu Lissu kwamba si kweli kwamba tangu Zitto alipofungua kesi yake mahakamani dhidi ya CHADEMA basi alikuwa si mwanachama tena wa CHADEMA kutokana na ibara ya katiba ya CHADEMA inavyosema, maana kama ingekuwa hivyo basi Zitto asingehudhulia Bungeni tangu tarehe 2/1/2014 lakini mbona ameendelea kuwa Mbunge hadi leo na hata siku zijazo mpaka utaratibu wa kisheria utakapofuatwa?
yeye Tundu ni nani hadi kutamka kwamba Zitto si mbunge tena wa Kigoma Kaskazini kama alivyotamka jana mbele ya waandishi wa habari? why souldn't he leave this matter to the proper authorities?
Hata kama Zitto akikoma kuwa Mbunge ni kwa mujibu wa katiba na Sheria za nchi na si kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA hasa kwa Ibara hiyo inayozuia mwanachama wa CHADEMA kwenda Mahakamani maana Ibara hiyo ni batlli na kinyume cha Katiba ya nchi.
Zitto bado ana fursa kubwa ya kwenda mahakama ya Rufaa kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi huo wa mahakama kuu na ni haki yake kuendelea na ubunge wake wakati akisubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambacho ni chombo cha juu kabisa cha maamuzi juu ya haki za watu hapa Tanzania.
kwa msomi wa sheria na wakili mkongwe kama Tundu Lissu kukurupuka kwa hisia za kisiasa na kuropoka juu ya hatima ya Zitto ndani ya CHADEMA mimi naona kama ni tukano kwa taaluma hii ya kifalme (It is an abuse to this noble profession).
Taaluma hii sasa imeingiliwa na wanasiasa uchwara ambao wanaweza kusimama na kutamka lolote ili mradi tu wakidhi hoja zao za kisiasa badala ya kwenda kwenye uhalisia wa kisheria. Ndiyo maana hata Ngereja ambaye kitaaluma ni mwanasheria alipohojiwa na baraza la tume ya maadili ya viongozi katika kutoa utetezi wake anajitetea kuwa eti siyo yeye tu aliyepokea hela za escrow bali pia hata Zitto kabwe naye alipokea kutoka sehemu kadha wa kadha.
Uliona wapi mwanasheria wa kweli anatoa utetezi wa aina hiyo? Can somebody justfy wrongs because the same have been commited/done by somebody else? Unaua mtu kwa sababu fulani naye kaua? Hao ndo wanasheria dizaini ya Tundu Lissu, wanajua lakini wanajifanya hawajui ili kujustify position na kiu zao za kisiasa.
Mwisho Zitto nakupa nguvu uamue mambo haya kwa utashi wako mwenyewe. Ikiwa unaona unahitaji kupata tafsri sahihi juu ya uamuzi wa mahakama kuu kutoka katika mahakama ya rufaa tanzania sisi tupo tayari kukusaidia hata bure kabisa tukiungana na Wakili Msomi Alberto Msando ili tafsri hiyo isiwe kwa manufaa yako tu bali kwa kizazi chote cha Tanzania.
Ni katika Mahakama ya rufaa tunaweza kupata maelekezo juu ya katiba mbovu za vyama kama CHADEMA zinazofifisha haki za watu/ wanachama wake kukishitaki chama wakati hilo ni takwa na haki ya kikatiba. Kuwa mwanamapinduzi kunahitaji moyo na muda.
Usikate tamaa, kama ni chama chao waachie kidizaini lakini twende Mahakama ya Rufaa tupate tafsri sahihi, na je Mahakama kuu kuendelea na kesi yako bila kutoa notisi kwako au kwa wakili wako kama tarehe ya kusikiliza ilibadilishwa kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari ilikuwa sahihi(kama ni kweli)?
Hayo ndo mambo ya muhimu watanzania wangependa kujua na si longolongo za kisiasa kama za Tundu Lissu na wenzake wenye mtazamo kama huo.
Aluta Continua Comrade Zitto Zuberi Kabwe. Demokrasia ya kweli lazima izingatie sheria na Katiba za Nchi zilizo nzuri zisizokiuka haki za watu. Si sheria zote ni Sheria!