Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania

KUNA VITU KADHAA BADO VINANITATIZA

1. Kuhusu serikali kutomtembelea Lissu hapo awali.
Sasa tufanye nyumba ya jirani mtoto wao anaumwa sana. Wazazi wa mtoto wamepiga ramli na kuambiwa kuwa bibi kizee jirani yao ndie mchawi aliemroga mtoto.

Taarifa zimezagaa kijiji kizima na yule bibi amezisikia.

Hivi mnaweza kugeuka na kumlaumu yule bibi kizee eti kwa nini hajaenda kumjulia hali mgonjwa au hajampelekea hata uji tu?


2. Kuhusu polisi wa Tanzania kumhoji Lissu akiwa Kenya.
Lissu sio mshukiwa wa shambulio lake yeye mwenyewe. Kwanini awe mbishi kuhojiwa na polisi wa kitanzania popote pale duniani?

Fikiria:
Wezi wamevunja nyumba yako, wakakufunga kamba, wakaiba kilakitu wakati unawaangalia.

Wakati upo London kwa shughuli zako binafsi polisi wa Tanzania wakakuomba waje wakuhoji ili wapate maelezo yako kuhusu wezi wako pamoja na mali zako zilizoibwa.

Hivi utakataa kukutana nao na badala yake utataka uhojiwe na MI5 au Scotland Yard wa Uingereza?

Uhalifu ufanyike Tanzania, wewe ndio shahidi (eye witness) mkuu, lakini unataka uhojiwe na polisi wa nchi ya kigeni?

Makubwa haya.
 
IGP hajui taratibu za kumhoji mtu ambaye yupo nje ya Tanzania aibu kubwa sana.
Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu.
 
KUNA VITU KADHAA BADO VINANITATIZA

1. Kuhusu serikali kutomtembelea Lissu hapo awali.
Sasa tufanye nyumba ya jirani mtoto wao anaumwa sana. Wazazi wa mtoto wamepiga ramli na kuambiwa kuwa bibi kizee jirani yao ndie mchawi aliemroga mtoto.

Taarifa zimezagaa kijiji kizima na yule bibi amezisikia.

Hivi mnaweza kugeuka na kumlaumu yule bibi kizee eti kwa nini hajaenda kumjulia hali mgonjwa au hajampelekea hata uji tu?


2. Kuhusu polisi wa Tanzania kumhoji Lissu akiwa Kenya.
Lissu sio mshukiwa wa shambulio lake yeye mwenyewe. Kwanini awe mbishi kuhojiwa na polisi wa kitanzania popote pale duniani?

Fikiria:
Wezi wamevunja nyumba yako, wakakufunga kamba, wakaiba kilakitu wakati unawaangalia.

Wakati upo London kwa shughuli zako binafsi polisi wa Tanzania wakakuomba waje wakuhoji ili wapate maelezo yako kuhusu wezi wako pamoja na mali zako zilizoibwa.

Hivi utakataa kukutana nao na badala yake utataka uhojiwe na MI5 au Scotland Yard wa Uingereza?

Uhalifu ufanyike Tanzania, wewe ndio shahidi (eye witness) mkuu, lakini unataka uhojiwe na polisi wa nchi ya kigeni?

Makubwa haya.
hana imani kabisa na jeshi letu la polisi,ila wafanye kwasababu wanatimiza wajibu wao
 
Aache utukutu! Atulie na kulisaidia jeshi letu la polisi kuwatia nguvuni waliomshambulia. Hivi Ana uhakika gani kuwa taratibu hazijafuatwa? Kwani ofisi ya mwanasheria mkuu wa Kenya imo kwenye wodi anayotibiwa?. Hivi cheo cha rais wa TLS ndiyo amri ya kumtaka kila jambo linalofika ofisini mwake mwanasheria Mkuu wa Kenya lazima alilipoti kwa mgonjwa watu ambaye anapata nafuu Sasa?
kuna haja ya kupeleka watu shule kwa mara ya pili maana sio kwa umbumbumbu hu
 
Matamko ya viongozi wetu huku yanatia shaka mimi Jirani yangu ni hapa in police aliniuliza Hugo alietoa hilo tamko la kutuma makachero Kenya anajua maana ya kuundwa Interpol au hakuna analolijua...anawezaje kusema police wa Nchi moja aende akafanye kazi ya kipolice Nchi nyingine...
 
Tundu ndugu na rafiki yet tunakupenda sana. Hata tusiojua kusali tunasali kwa ajili yako. Mungu akupe nguvu na moyo wa kuvumilia yote na awalipe waliokudhuru stahiki zao.
Pole sna. Upone haraka
 
Mkuu Elias Maswe, dereva wa Lissu sio mtuhumiwa, wala Lissu sio mtuhumiwa, lakini kwa vile hao ndio mashuhda pekee wa tukio hilo wanaofahamika, hawa ndio mashahidi namba 1 na 2 wa tukio hili, hivyo polisi ina wajibu wa kuwahoji.

Sababu za hawa kuhojiwa ni ili tuu kuisaidia polisi kuwabaini wale wasiojulikana waliofanya tukio hili
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!.
Paskali
Pasco police wetu hawakuwa na haja na huyo kijana (dereva). Wamemtafuta siku tatu baada ya tukio tena kupitia vyombo vya habari !!
Ukumbuke huyu kijana alikuepo kwenye tukio, hospital na hata Airport kumsindikiza bosi wake!! Na kote huko police walikuepo wakihangaika na wafuasi wa CDM wasisogelee tukio!!
After all CCTV footage ziko wapi?! Upelelezi wa kitoto
 
MAKACHERO WALIO TUMWA KUMHOJI MH: LISU. Makachero waliotumwa kumhoji MH LISU katika sakata la kupigwa risasi miezi kadhaa iliyopita, wamekwama baada ya kutumwa uko kyenyeji kyenyeji bila kufata sheria na taratibu, wakijua watamhoji kama wanavyojua wao kana kwamba wanaenda kunywa chai na uji ndani ya nchi za wengine. Waambiwa walale kwanza vibarazani ili utaratibu ufuatwe na wakishindwa waondoke, kwa taarifa za kina wamerudi bila kumhoji, hasara za usafiri na gharama nyinginezo ni Kodi za watanzania.
ELIMU ELIMU ELIMU
Propaganga za kijinga
 
Ndugu zangu Watanzania. Salaam za upendo na shukrani kwenu wote.

Leo ni mwezi wa tatu tangu kufanyika kwa jaribio la kuniua la tarehe 7 September.

Tangu siku hiyo, nimetembelewa na mamia ya Watanzania na watu wengine kutoka nchi mbali mbali duniani.

Nimeombewa sala na mamilioni ya Watanzania na watu wengine wengi kutoka nchi nyingine walioguswa na tukio hili.

Nimetembelewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi na viongozi wengine wa serikali ya Kenya na taasisi zake; pamoja na wabunge wa Tanzania na wa Kenya, majaji na wanasheria wa nchi mbali mbali, n.k.

Hata hivyo, hadi sasa Jeshi la Polisi la Tanzania halijataja linamshuku nani kuhusika na kitendo hicho cha kigaidi.

Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu.

Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania.

Hadi sasa Bunge la Tanzania na uongozi wake haujachukua hatua yoyote ya kunitembelea hospitalini nilikolazwa wala kunihudumia kwa namna yoyote ile.

Sheria ya Uendeshaji wa Bunge inasema ni wajibu wa Bunge kumhudumia mbunge kwa matibabu na huduma nyingine anapokuwa hospitalini ndani au nje ya Tanzania.

Kwa kila namna, ninauguzwa na chama changu, Watanzania na watu wengine kutoka sehemu mbali mbali duniani kwa michango yao, sala zao na mapendo yao kwangu. Nawashukuruni sana na Mungu wetu awabariki sana.

Mambo yote haya yanatilia nguvu hoja yetu juu ya ulazima wa uchunguzi huru wa shambulio hili la kigaidi. Likiachiwa kwa serikali ya Tanzania peke yake ukweli hautakaa ujulikane.

Ninaendelea vizuri na matibabu na madaktari watakaposhauri nitaanza hatua nyingine ya matibabu yangu.

Mungu ni mwema, nitasimama na kutembea tena. Nitarudi nyumbani ili kuendelea na kazi ambayo imempendeza Mungu kuokoa maisha yangu ili niweze kuitenda.

Kumekuwa na matukio mengi ya kutisha kama hili na mengine mbaya zaidi. Nchi yetu inahitaji ukombozi ili maovu haya yakomeshwe kabisa. Hili ni jukumu letu sote tunaojiona kuwa wazalendo halisi wa Tanzania.

Nawashukuruni sana na Mungu wetu awabariki sana.

Tundu AM Lissu (MB)

The Nairobi Hospital, Kenya
cc: Lizaboni
Ruttashobolwa
Pascal Mayalla
stroke
 
Jeshi la polisi haliwez kukamilisha upelelezi kwa sababu Lissu ni first observation point...u cnt move on without his witness jamaa yupo hai na ushahidi wake unahtajika sasa...labda angekuwa amefariki...hvyo kama hataki bas shughuli zote za upelelezi zitasimama hadi pale atakaporudi tz...na pia mnaolalamika kuwa upelelezi unachelewa inabidi mkae kimya sasa
 
Kama huelewi kitu acha kuwa na maneno mengi. Tundu anajua afanyacho na hataki maisha yake yafanyiwe hadaa na mambo kama hayo ya mahojiano fake.
Anajua anataka kusema nini na mahojiano hayo ambayo yanaweza kutumika mahakamani kama ushahidi lazima yafanyike kisheria, na sheria hairuhusu kufanyika nje ya nchi bila kibali maalumu kutoka huko kama ilivyo kwetu kuwa huwezi fanya mahojiano usiku!
Sasa usichoelewa au kinachokufanya utunge nadharia mbovu ni nini?
Hujui kitu!! Mambo ya kipelelezi waachie wapelelezi wewe fanya yanayokuhusu!
 
Ndugu zangu Watanzania. Salaam za upendo na shukrani kwenu wote.

Leo ni mwezi wa tatu tangu kufanyika kwa jaribio la kuniua la tarehe 7 September.

Tangu siku hiyo, nimetembelewa na mamia ya Watanzania na watu wengine kutoka nchi mbali mbali duniani.

Nimeombewa sala na mamilioni ya Watanzania na watu wengine wengi kutoka nchi nyingine walioguswa na tukio hili.

Nimetembelewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi na viongozi wengine wa serikali ya Kenya na taasisi zake; pamoja na wabunge wa Tanzania na wa Kenya, majaji na wanasheria wa nchi mbali mbali, n.k.

Hata hivyo, hadi sasa Jeshi la Polisi la Tanzania halijataja linamshuku nani kuhusika na kitendo hicho cha kigaidi.

Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu.

Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania.

Hadi sasa Bunge la Tanzania na uongozi wake haujachukua hatua yoyote ya kunitembelea hospitalini nilikolazwa wala kunihudumia kwa namna yoyote ile.

Sheria ya Uendeshaji wa Bunge inasema ni wajibu wa Bunge kumhudumia mbunge kwa matibabu na huduma nyingine anapokuwa hospitalini ndani au nje ya Tanzania.

Kwa kila namna, ninauguzwa na chama changu, Watanzania na watu wengine kutoka sehemu mbali mbali duniani kwa michango yao, sala zao na mapendo yao kwangu. Nawashukuruni sana na Mungu wetu awabariki sana.

Mambo yote haya yanatilia nguvu hoja yetu juu ya ulazima wa uchunguzi huru wa shambulio hili la kigaidi. Likiachiwa kwa serikali ya Tanzania peke yake ukweli hautakaa ujulikane.

Ninaendelea vizuri na matibabu na madaktari watakaposhauri nitaanza hatua nyingine ya matibabu yangu.

Mungu ni mwema, nitasimama na kutembea tena. Nitarudi nyumbani ili kuendelea na kazi ambayo imempendeza Mungu kuokoa maisha yangu ili niweze kuitenda.

Kumekuwa na matukio mengi ya kutisha kama hili na mengine mbaya zaidi. Nchi yetu inahitaji ukombozi ili maovu haya yakomeshwe kabisa. Hili ni jukumu letu sote tunaojiona kuwa wazalendo halisi wa Tanzania.

Nawashukuruni sana na Mungu wetu awabariki sana.

Tundu AM Lissu (MB)

The Nairobi Hospital, Kenya
Mara hoo jeshi la polisi kwa nini halitaki kunihoji nikasema yote yaliyotokea. Sasa jeshi hilo limeamua kuja, unadai kuwa halina mamlaka ya kukuhoji ukiwa nje ya mipaka ya Tanzania! Sasa, mbona haueleweki? Si useme tu ukiwa hapo ili sisi watanzania tujue ukweli. Sasa kama siyo jeshi la polisi kukuhoji, unataka uhojiwe na nani?
 
Huo ndio utaratibu wa kisheria, kwani haiwezekani?? Umeweka wapi akili yako, japo ni ya QT.
Mkuu swala ni warudishwe Tanzania au Tanzania wawafuate hukohuko kuwahoji. Hakuna cha Kenya wamuhoji dereva wa lisu au lisu then watume ripot.
 
Mkuu, Shida ninayoiona Polis wetu wanataka kumuhoji Dereva wa lisu kama mtuhumiwa ukisikiliza maelezo ya kamanda Siro na agizo la mwanzo la kamanda wa polis mkoa dodoma kuna walakini kwa mwenye uelewa nini ajenda yao?

Waandishi wa habari msio egemea upande wa Serikali kuweni makini tunawapenda sana kwa michango yenu ya kutu Elimisha Inchi yetu si Rafiki wa ukweli na haki.

Uwe na siku njema
Mkuu Impongo, kwanza naungana na wewe kuwa utafutwaji wa dereva wa Lissu ni kama mtuhumiwa, ndio maana nikasema humu hao makachero waliotumwa Nairobi, sio kumhoji, bali kumsomba, mzobe mzobe.

Shida kuhusu tukio hili, haiko kwa polisi tuu, any reasonable man would wish to hear that side of the story especially the miraculous escape ya ki Jemsi Bond ya dereva huyo, risasi zaidi ya 40 zimepigwa, yeye akiwa dereva, akamvuta Lissu, akwambaza kiti cha dereva, akatoka nje kumiujiza, akaingia chini ya gari, huku risasi zinarindima. Yeye hakuna hata risasi moja iliyompata!. Kwa macho ya kawaida huyu ni zaidi ya Comandoo, kwa jicho la kipolisi huyu ni zaidi ya shuhuda muhimu, na jinsi viongozi wa Chadema wanavyompa protection, kumlisha, kumtunza ugenini, leaves much more to be desired, ndio
maana sisi ma open minded, don't rule out any options even an inside job of friendly fires.

Kanisome hapa

Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!.

Paskali
 
Mkuu swala ni warudishwe Tanzania au Tanzania wawafuate hukohuko kuwahoji. Hakuna cha Kenya wamuhoji dereva wa lisu au lisu then watume ripot.
'Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu.
Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania'.

By Tundu Lissu, Rais wa wanasheria Tanganyika, na mwanasheria msomi...pia ni mzalendo nambari one Tanzania.
 
Back
Top Bottom