Tundu Lissu ni shujaa

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
17,919
Reaction score
24,754
Pamoja na yote yaliyomkuta, Tundu Lissu hakuogopa kurudi nyumbani na tena sio kurudu tu bali kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na aliporudi hakukaa kimya amezungumza ukweli wote wa mambo bila chembe ya uoga.

Hata baada ya hila za kila aina dhidi yake na wagombea wa CHADEMA, Lissu ameendelea kufanya kampeni zenye mvuto kuliko zote katika kila mkoa na wilaya za nchi yetu.

Tundu Lissu amewafungua watanzania macho, amewafanya wajisikie huru tena amewarudishia matumaini na kuwafanya wajiamini tena na kuthubutu kutumia uhuru wao.

Hatimaye Tundu Lissu amemaliza kampeni zake leo pamoja na kuzuiliwa na kuwekewa mizengwe kila mahali Lissu amemaliza mwendo kwa ufanisi mkubwa!

Hima hima mtanzania usifanye kosa kumchagua mtu ambaye hana maono wala huruma kwa watanzania, sote tumchague Tundu Antipas Lissu awe rais wetu 2020-2025.

Mungu mbariki Tundu Lissu, Mungu ibariki Tanzania. Nawatakia uchaguzi mwema!
 
Hebu kesho ipite zoezi liishe salama ili tujadili mambo mengine maanake wanajadiliwa watu wawili tu
 
Umechelewa watanzania wameshaamua ni mitano tena kwa MAGUFULI, karibu kwenye sherehe ya kuapiswa Rais uwanja wa Jamuhuri jijini Dodoma.
 

Yaan hapo ni kwamba ccm na serikali yake wanaforce kwenye uchaguzi huu kushinda kwa nguvu wakati ni jambo lisilowezekana. Hauwezi kumlazimisha punda kupanda kilima kikali kilichoshindikana kwa kumtamanishia majani kisa ana njaa, wakati huo umemkalia juu na kumbebesha mizigo mizito zaidi japo yeye ni mkokota mizigo.

Hapo kilichobaki ni punda kukataa utumwa wa kupanda kilima na kulala chini asubiri litalokuwa na liwe. CCM wanajidangana na msemo wa kijinga eti "ni bora afe lakini mzigo ufike", sasa ni bora mzigo uharibike lakini punda abaki maana yeye akibaki atasaidia kazi nyingine nyingi. Chadema na Lissu kwanza.
 
Nina maswali mengi
1.Wakiteka mawakala
2. Wakibadili matokeo ?
3. Kwanini wamezuia wakala asiingie na simu?
4. Kwanini inatumika nguvu kubwa wananchi wasilinde kura?
 
Shujaa wa nini aisee...Shujaa wa nchi hii ni Magufuli

Congratulations in advance President Magufuli

JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Pamoja na yote yaliyomkuta, Tundu Lissu hakuogopa kurudi nyumbani na tena sio kurudu tu bali kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na aliporudi hakukaa kimya amezungumza ukweli wote wa mambo bila chembe ya uoga...
Kesho ndio mwisho wa hizi ngonjera..
 
Mh Lissu kamtikisa kweli kweli Bw Yule hadi kachanganyikiwa. Akiwa kwenye kampeni badala ya kunadi sera za chama chake amejikuta akizindua miradi iliyokwisha zinduliwa tena na yeye mwenyewe. Mfano bomba la mafuta toka Uganda kwenda Tanga.
 
Hebu soma hizi uelewe. Usikurupuke tu kwa ushabiki WA kishamba.View attachment 1614055
 
Pamoja na yote yaliyomkuta, Tundu Lissu hakuogopa kurudi nyumbani na tena sio kurudu tu bali kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na aliporudi hakukaa kimya amezungumza ukweli wote wa mambo bila chembe ya uoga...
Tundu Lissu ni shujaa na nusu!
 
Reactions: BAK
Umenena vema madam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…