Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Rais anayesaini mikataba ya hovyo kuliko hata wa Chifu Mangungo; anayegawa bandari zetu zote na nia za usafirishaji kisirisiri kwa wageni; anayelazimisha Bunge kubariki uharamia huo, na anayenyang'anya watu wetu ardhi zao na kuwapa wageni, anastahili kukosolewa kwa staha gani?
Tundu Lissu
Julai 18, 2023
Barua ya wito wa Polisi
====
Mnamo jana, Julai 17 Mdau wa JF alidokeza kuwa Lissu na Mbowe walikuwa wanasakwa DOKEZO - Lissu na Mbowe wanatafutwa kukamatwa lakini Lissu aliifahamisha JF "Sijazisikia tetesi hizo. Kama ni za kweli, itakuwa ni mara ya kwanza kwa mimi au Mwenyekiti kukamatwa?"