Gedeli
JF-Expert Member
- Mar 16, 2012
- 497
- 222
Unaweza kurejea kwenye mjadala wa jana hapa chini juu ya kifo cha Kassim Hanga
Yamemkuta Lissu: Kushtakiwa na mtoto wa Hanga kwa udanganyifu!
WanaJF,
Mtoto wa aliyekuwa mwasisi wa mapinduzi ya Zanzibar, bwana Juma Abdallah Hanga, ameamua kuchukua maamuzi magumu ya kumpeleka Tundu Lissu mahakamani kufuatia kauli za mwanasheria huyo wa CHADEMA kuwa za uongo, uchochezi na udanganyifu.
Mtoto huyo wa kwanza wa hayati Hanga, ambae pia ni mwanachama wa CCM, amesema baba yake alifariki kifo cha kawaida na kuzikwa kwa kufuata taratibu zote za dini ya kiislamu kwenye makaburi ya familia. Kwa maana hiyo maneno ya mwanasiasa Tundu Lissu kuhusu chanzo cha kifo cha baba yake ni ya kuokoteza na hayana ukweli wowote. Aliliambia gazeti la Zanzibar Leo.
Pia Juma Hanga amesema amepanga kwenda mahakamani kumshtaki mwanasiasa Tundu Lissu kwa upotoshaji wake kwa umma juu ya kifo cha baba yake kwa kuwa ana amini akiacha maneno hayo ya uongo yaendelee kusemwa yanaweza kuzua uchochezi utakao vuruga amani.
My take,
Ni wakati sasa kwa Lissu kuandaa ushahidi wake juu ya kauli yake ya kuuwawa kwa mwasisi huyo na kuonyesha kaburi hilo la pamoja analodai mwanasiasa huyo pamoja na wenzake wamezikwa. Hili suala halitaki porojo.
Lissu utamshitaki kwa kosa lipi??? Hajasema serikali ndio iliyowauwa watuhumiwa amenakili tu vitabu ambavyo mpaka sasa vipo ila kwa uvivu wetu wakusoma ndo maana hatujui au tunaogopa kusema yeye alichosema anaiomba serikali ituambie ukweli kuhusu watu hawa basi lakini kinachotokea ni kumshabulia Lissu. swali kwani Mzee karume aliuawa na nani? na kwa sababu gani vile?