Iramba Junior
Member
- Apr 2, 2012
- 98
- 26
Hili linatakiwa lifanywe na Zitto atakapohitimisha hoja yake. Aweke motion ya kutokuwa na imani na serikali kisha wabunge wa CDM wasibweteke wasimame kuunga mkono tuone kama magamba wataunga mkono? na wananchi waone nani kweli anawatetea.
Alichosema Mh.Lissu ni kuwa kila mwaka
Kamati za Bunge za hesabu za serikali zimejaa
Ubadhirifu na wizi mkubwa lakini serikali
Ya CCM iko kimya na haichukui hatua stahili ama
Haichukui hatua kabisa. Hivyo amewaomba wenyeviti
Wa kamati hizo 3 wa move motion ya kupiga
Kura ya kutokuwa na imani na serikali. Pia
Kawaambia wabunge wa CCM kwa kuwa wao wako
Wengi waunge mkono jambo hilo ili serikali
Iwajibishwe kwa manufaa ya nchi.
mambo yanazua mambo. Kama kweli wabunge wa CCM ambao ni wengi zaidi bungeni wanaona uchungu jinsi fedha za uma zinavyotafunwa, na jinsi ambavyo serikali haijamuwajibisha hata mtendaji mmoja, basi wapitishe motion ya kutokuwa na imani na mtendaji mkuu ambaye ni waziri mkuu.
source; bunge
Nakubaliana na taarifa za kamati zote kwa kuibua madudu ya ubadhilifu katika serikali na taasisi zake.Ambayo yamekua yakiibuliwa mwaka nenda mwaka rudi bila kuwawajibisha wahusika,kwa vile imekua kawaida wakati wote pesa nyingi zinatumika kuibua madudu haya lakini hakuna hatua zote zinazochukuliwa.Malalamiko ya wabunge ni siasa wao wanachopashwa kufanya nikuibana serikali kuhusiana na madudu haya.Hivyo kushinikiza serikali kujiuzulu kwa mapungufu yake kushindwa kuchukua hatua kwa madudu haya mwaka nenda miaka rudi.Hii itatoa mfano kwa wahusika kuchulia mambo kwa makini na sio porojo.Vininevyo hatutafika popote MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Nashauri mmoja wa wabunge wa CHADEMA aanzishe hoja ya kutokuwa na imani na serikali ili tupembue mchele na chuya kutoka wabunge wa CCM kama hasira wanazoonyesha ni za kweli au wanatupiga changa la macho?