Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aijibu NEC kutishia baadhi ya wagombea "wanaohatarisha amani" kwenye kampeni zao

lissu ameshachoka
badala ya kujikita kwenye kampeni anawarukia tume,kwani wamemtaja?
hiyo ni kazi ya mnyika,yupo tu ofisini anaratibu michango ya Tigo pesa
 

Hata uchaguzi ukifanyika na Magufuli na genge lake la ccm wakafanikiwa kuchakachua matokeo, lakini atakuwa amejua kabisa hajafanikiwa kuua upinzani kama yeye binafsi na wapambe wake walivyojidanganya. Na amejua kabisa wanaomkubali ni wanaccm wenzake na watanzania kadhaa, lakini sio watanzania wote.
 
Huyu jamaa yenu anawalisha matango pori tu Tena ya kwasababu anapiga kelele tu mitandaoni badala ya kufuata utaratibu nimesoma kanuni za maadili ya Uchaguzi zinasema unatakiwa kutoa taarifa ya maandishi ktk sehemu husika ndani ya masaa 72 toka ukiukwaji wa maadili ulipofanyika.sasa kulalama tu Kama hayawani bila kutekereza hayo ni kazi bure.
 
Imeadikwa WAACHENI WATOTO WADOGO WAJE KWANGU.
 

Unakanusha au unakubaliana na Tundu Lissu?

Nilivyokuelewa, ni wazi kuwa umekubaliana na Tundu Lissu kuwa asemacho ni kweli...

Na ni kweli kabisa kwa sababu wote tunaona kwa macho yetu, tumesikia kwa masikio yetu kwamba mgombea wa CCM na NEC yenyewe wanakiuka na kuvunja kanuni na maadili ya uchaguzi mkuu 2020 waziwazi na hatua hazichukuliwi..., au siyo bwana?

Unasema walalamike ndani ya masaa 72;

Hebu tuambie hawajakata rufaa kwa wagombea wao wa ubunge na udiwani walioenguliwa "kishenzi" na NEC?

Na alichokisema Dr Mahera Charles jana, alilalamikiwa na nani? Mgombea wa CCM?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…