johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,976
Maendeleo hayana chama.
Nitoe tu ushauri kwamba ni heri Tundu Lisu ambaye ni mwanafunzi wa mwanasheria nguli kabisa duniani Prof Kabudi aachwe ajitetee mwenyewe kuhusu kuvuliwa ubunge.
Utetezi unaoendelea kutolewa na makamanda wa Chadema wakiwemo Dr Mashinji na yule Mrema unaweza kumharibia zaidi.
Kwa mfano Dr Mashinji anaamini Joshua Nassari bado ni mbunge halali na kwamba jimbo la Arumeru mashariki lina wabunge wawili kwa sababu kuondolewa kwa Nassari hakujatangazwa kwenye gazeti la serikali. Sasa utajiuliza katiba ya JMT inaruhusu jimbo kuwa na wabunge wawili wa kuchaguliwa? Kadhalika anaamini Tundu Lisu ni mbunge halali kwa sababu kama hizo.
Mrema anadai Lisu alikuwa kwenye coma kwa muda wa miezi minne ndio maana hakuandika barua na hata kama angeandika baada ya kuzinduka Spika angemuambia alikuwa mtoro kwa ile miezi 4 aliyokuwa hajitambui.
Yaani ni utetezi wa ajabu kabisa.
Tundu Lisu jitetee mwenyewe kamanda hawa wapambe wataharibu.
Kila la kheri kamanda!
Nitoe tu ushauri kwamba ni heri Tundu Lisu ambaye ni mwanafunzi wa mwanasheria nguli kabisa duniani Prof Kabudi aachwe ajitetee mwenyewe kuhusu kuvuliwa ubunge.
Utetezi unaoendelea kutolewa na makamanda wa Chadema wakiwemo Dr Mashinji na yule Mrema unaweza kumharibia zaidi.
Kwa mfano Dr Mashinji anaamini Joshua Nassari bado ni mbunge halali na kwamba jimbo la Arumeru mashariki lina wabunge wawili kwa sababu kuondolewa kwa Nassari hakujatangazwa kwenye gazeti la serikali. Sasa utajiuliza katiba ya JMT inaruhusu jimbo kuwa na wabunge wawili wa kuchaguliwa? Kadhalika anaamini Tundu Lisu ni mbunge halali kwa sababu kama hizo.
Mrema anadai Lisu alikuwa kwenye coma kwa muda wa miezi minne ndio maana hakuandika barua na hata kama angeandika baada ya kuzinduka Spika angemuambia alikuwa mtoro kwa ile miezi 4 aliyokuwa hajitambui.
Yaani ni utetezi wa ajabu kabisa.
Tundu Lisu jitetee mwenyewe kamanda hawa wapambe wataharibu.
Kila la kheri kamanda!