Baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa kuzungumza na Wanahabari jana. Wakili Msomi ndugu Tundu Lissu aliibukia Voice of America Idhaa ya Kiswahili akijibu Hoja za Slaa kwa style ile ile iliyozoeleka na Chama chake ya KUCHAFUANA.
Wengi mnajua alichoongea hasa hasa akimuingiza mchumba wa Dr. Slaa kuwa anahusika na move aliyoifanya Dr jana. Ninaamini kuwa kwa Chama makini kama CHADEMA walipaswa kuzipangua hoja za Slaa kuliko walivyomtuma Lisu kuongezea hoja juu ya hoja na kuibua interest za wadadisi kujua uadilifu wao.
Katika suala la Josephine kuhusishwa imefikia hata kumdhalilisha Dokta kwa kusema alitupiwa virago vyake nje akalazimika kulala ndani ya gari. Ina maana CHADEMA wanafuatilia mpaka mahusiano ya unyumba baina ya members wake!
Unashangaa nini?
Si yeye mwenyewe alitamka na kukana kushiriki kumleta Lowassa?
Mbaya zaidi amekwenda mbali kwa kuongeza mambo mengi yasiyo ya lazima.Kutofautiana katika jambo ni sehemu ya hulka ya Binadamu.yeye kadai ameleza ukweli mtupu na lisu kaeleza Ukweli mpaka kiasi chake na kaacha swali nyuma kwa Dr.Kumalizia majibu.
Kusema kweli kama mtu mzima kutolea maelezo kuachana kwake na Siasa ilikuwa jambo lake mwenyewe na Mwenyekiti kusema kuwa Dr.kaomba kupunzika ilikuwa Kauli yenye staha kubwa. Sasa yeye kutumia Kauli za vijana ya majukwani kujibu Chama as if Matusi na kejeli zilikuwa zimetoka kwa Viongozi wa Chama si haki hata Kidogo.
Ndiyo maana sisi wengine tulishauri Dr.akae kimya au angeishia kwenye kueleza Ukweli kuwa walishindwa kuelewana na yeye sasa Siasa Basi-na Kama anataka na kuamini atafanikisha jambo kupitia Uanaharakati basi ajikite huko kwa namna ambayo haitaonekana yuko kwenye siasa.